Hakuna kitu kisichotegemea kingine; nyie wenyewe mikutano yenu ya siasa mnafanya mda ambao watu wengi wamemaliza kazi, yaani jioni.
Sasa huko uingereza unakosema ushajiuliza kwa nini hawachezi asubuhi? Unadhani wanakuwa wamechoka? Au kwa nini FIFA haikupanga michezo hii ifanyike asubuhi?
Jibu utakalopata litaendana na sababu za kibiashara.
Na nikwambie upendeleo upo tu kila sehemu. Ingekuwa haupo, basi kwenye kupanga makundi ya mpira timu kubwa zingekuwa zinakutana tangu hatua ya awali ya makundi au kuwekwa kundi moja, lakini wataziweka makundi tofauti tofauti. Unadhani kwa nini? Kwa sababu hizi timu kubwa ambazo ndizo zenye mashabiki zikipangwa pamoja zikatoka mapema wenye TV rights za kurusha matangazo watapata hasara na vilabu hali kadhalika vitakosa baadhi ya mapato.
Likewise hapa kwetu, vibanda umiza huwa vinajaa watu pale simba au yanga zinapocheza. Sasa kwa nini mechi hizo zipangwe mda wa kazi? Nani anataka hasara?
Hapa suala sio haki tu, suala ni faida kwa vilabu na wadau wengine.