Nchi kubwa kama DR Congo na Msumbiji hazipaswi kuwa na makao makuu ya nchi pembezoni

Nchi kubwa kama DR Congo na Msumbiji hazipaswi kuwa na makao makuu ya nchi pembezoni

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Nchi kuwa kubwa, na dhaifu halafu kuwa na makao makuu pembezoni ni hatari sana kwa usalama wake.

Kwa nchi zetu hizi kadri unavyozidi kuwa mbali na Capital City ndivyo unavyozidi kusahaulika. Na watu waliosahaulika ni rahisi kuasi.

Hawa wameweka mji mkuu Kinshasa. Kilomita zaidi ya 2500 kufika Goma. Wangetafuta mji hapo katikati.

dr_congo_map.jpg


Msumbiji wameweka mji mkuu kwenye kona kabisa. Ndiyo maana inakuwa ngumu kudhibiti maeneo ya kaskazini. Yanaishia kudhibitiwa na waasi na sasa magaidi. Walau makao makuu yangekuwa Beira.

Mozambique_map.jpg


Pengine Nigeria wasingehamisha makao makuu kutoka Lagos wangepata shida sana na watu wa kaskazini, walio wengi.
Nigeria-map-boundaries-cities-locator.gif


Nchi zingine zilizoona umuhimu wa kuweka makao makuu ya nchi katikati ni Pamoja na Tanzania na hivi karibuni Indonesia.

DRC ingekuwa na Capital City katikati ya nchi ingeweza saidia kuepuka machafuko inayoyakabili miaka na miaka?
 
Capital City ndivyo unavyozidi kusahaulika. Na watu waliosahaulika ni rahisi kuasi.

Ujenzi wa taifa au dola ili thabiti hutegemea vyombo vya dola kuwepo kila eneo la nchi na siyo kurudikana ofisi zote makao makuu ya nchi mfano Dodoma

Kusambaza keki ya taifa, viwanda, makao makuu ya mashirika sehemu au kanda za nchi badala ya kurundikana Dodoma husaidia keki ya taifa kugusa maisha ya watu na vyombo vya dola sehemu zote za nchi.

Kwa mfano makao makuu ya Shirika la Reli na karakana kuu yangewekwa Tabora, pia makao makuu ya TAZARA na karakana kuu mjini Mbeya, Dar es salaam ibaki na Bandari huku ATC AirTanzania makao Kilimanjaro na Mahakama Kuu makao yawe Arusha, Mwanza iwe masuala yote ya Pamba na Bodi yake, Kigoma ifanywe mji kitovu cha magodown na biashara za kusambaza bidhaa, ugavi kwa nchi za DR Congo, Burundi. Njombe Makambako iwe makao ya makaa ya mawe, viwanda vitakavyotumia nishati ya vinu vya umeme wa makaa ya mawe.

Nchi za Russia, China, Japan, Ukraine, USA wamesambaza viwanda kisekta katika miji na kanda mbalimbali ili keki ya taifa, ajira, biashara na mzunguko wa fedha uenee maeneo mengi badala ya kila kitu kuwa sehemu moja mfano makao makuu Dodoma hadi TPA Mamlaka ya bandari inalazimishwa ihamie Dodoma waziri wa uchukuzi ajisikie bosi.
 
View attachment 3220653
Mji mkuu Beijing taifa la China
Ndiyo maana pale juu nikasema "na dhaifu."

Pia ukiangalia China na Russia unaweza sema makao makuu yapo pembezoni, lakini ukija kuangalia mtawanyiko wa watu utaona hayo maeneo ni kama center. Zaidi ya nusu ya wachina wanaishi pwani. Warussia wengi wanaishi Russia ya Ulaya. Hata Canada imekaa muondo huo.
 
Ndiyo maana pale juu nikasema "na dhaifu."

Pia ukiangalia China na Russia unaweza sema makao makuu yapo pembezoni, lakini ukija kuangalia mtawanyiko wa watu utaona hayo maeneo ni kama center. Zaidi ya nusu ya wachina wanaishi pwani. Warussia wengi wanaishi Russia ya Ulaya. Hata Canada imekaa muondo huo.

Kubwa sambaza shughuli za viwanda, viwanda vya usindikaji, viwanda vya kufua chuma, kufuatana na mpango maalum sehemu za utalii mkubwa n.k

Hizo nchi za Canada, Russia zote zimefuata mtindo wa kusambaza shughuli za kiviwanda, kijeshi, mashirika ya umma kwa jinsi hiyo bila ugonjwa wa nchi zetu kama Tanzania kila kitu kikawa DSM sasa kila kitu mwelekeo Dodoma ni udhaifu wa kidola na kupelekea udhaifu wa utawala na mwishowe udhaifu wa kijeshi.

Mwanzo | TRC
https://www.trc.co.tz
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Shirika la Reli Tanzania

14 Mar 2023 — Shirika la Reli ni miongoni mwa taasisi za Serikali zinazotarajiwa kuhamia makao makuu ya Nchi jijini Dodoma katika...

Mwananchi
https://www.mwananchi.co.tz
Safari ya Serikali kuhamia Dodoma kukamilika mwakani

21 May 2024 — Jumla ya watumishi 25039 kutoka Serikali kuu, Bunge, Mahakama, vyombo vya ulinzi na usalama, pamoja


X · MabalaMakengeza
680+ likes · 2 years ago

Richard Mabala


Kuhamisha shughuli nyingine za bandari Dodoma ni dalili ya tatizo kubwa zaidi. Ufanisi wa shughuli nyingi umeathirika sana na ofisi kuhamia..
 
Kubwa sambaza shughuli za viwanda, viwanda vya usindikaji, viwanda vya kufua chuma, kufuatana na mpango maalum sehemu za utalii mkubwa n.k

Hizo nchi za Canada, Russia zote zimefuata mtindo wa kusambaza shughuli za kiviwanda, kijeshi, mashirika ya umma kwa jinsi hiyo bila ugonjwa wa nchi zetu kama Tanzania kila kitu kikawa DSM sasa kila kitu mwelekeo Dodoma ni udhaifu wa kidola na kupelekea udhaifu wa utawala na mwishowe udhaifu wa kijeshi.

Mwanzo | TRC
https://www.trc.co.tz
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Shirika la Reli Tanzania

14 Mar 2023 — Shirika la Reli ni miongoni mwa taasisi za Serikali zinazotarajiwa kuhamia makao makuu ya Nchi jijini Dodoma katika...

Mwananchi
https://www.mwananchi.co.tz
Safari ya Serikali kuhamia Dodoma kukamilika mwakani

21 May 2024 — Jumla ya watumishi 25039 kutoka Serikali kuu, Bunge, Mahakama, vyombo vya ulinzi na usalama, pamoja

X · MabalaMakengeza
680+ likes · 2 years ago
Richard Mabala

Kuhamisha shughuli nyingine za bandari Dodoma ni dalili ya tatizo kubwa zaidi. Ufanisi wa shughuli nyingi umeathirika sana na ofisi kuhamia..
Kwa nchi dhaifu kama DRC na Msumbiji zinazotegemea kilimo zitasambaza nini?
 
Hiyo sio sababu, DRC na Mozambique ni shida tu watawala wa KiAfrica waliowabinafsi zaidi ya maslahi mapana ya mataifa yao.

Ukiweka usawa na kushirikisha Taifa zima kwenye utawala huwezi kupata hizi shida, weka uchaguzi huru, weka mfumo wa Sheria unaofanya kazi nk.
 
hapa kwenye kujadili mambo siriaz huwezi kuwaona watumiaji wa JF wanaojinasibu ni MAGREAT THINKER😁😁😁😁😁.

📌📌📌WACHANGIAJI WENGI WAPO NA MADA ZA UDINI,NGONO,UCHAWA KUSIFU NA KUABUDU NA MAMBO MEPESI MEPESI KUASHIRIA UPEO MDOGO WA AKILI,UDUMAVU WA AKILI,CHANGAMOTO YA AFYA YA AKILI,LISHE DUNI ILIYOPELEKEA KUWA NA MAZEZETA WENGI NA PIA ELIMU DUNI WALIYONAYO KUTOKA VYUO VYA KATA.

SASA TAASISI YA BANDARI IKAFANYE NINI DODOMA!!!!

📌SHITHOLE COUNTRIES NEED TO BE COLONIZED FOR THE 2ND TIME AND EVEN 3RD TIME.GADEMBICH!!!!
 
Wewe mtoto wa mwaka 2000 nakukumbusha RDF imewahi kutoka kigali hadi kinshasa straight away kipindi RDF inafanya OPERATION KITONA.
Aiseee,watu wanapambana,pamoja na jiografia ya congo kuwa mbaya kimiundombinu ya usafir lakin wanaume walifika bila kipingamiz
 
Moja ya Vitu huwa Najiuliza Ni Hili la Maka makuu ya Bandari kuwa Dodoma!!
Hivi Viongozi wetu huwa Wanakaa Na kufikiria Kweli
Dodoma Haina Hata Gati la Mtumbwi Mnaweka Makao makuu ya Badari!!?
Kingine Ni Tabora
Sasa Kilimo cha Tumbaku Nchi hii Kinalimwa Sana Tabora Lakini Kiwanda Kipo Morogoro!!
 
Kwani mzee Kabila alifika je...Congo hawana jeshi madhubuti hiyo miji ya kati kati ndo kabisaa...
 
Kwani hujui mzee kabila safari yake ilianzia Goma mpk kishansa?..kwenda kumtoa Mobutu?
 
Back
Top Bottom