Wakuu,
Mwaka 2017 Dkt. Nchimbi alipewa onyo kali huku wanachama wengine wakivuliwa uachama kutokana na utovu wa nidhamu kwenye chama baada ya kumkataa Magufuli na kumsapoti Lowasa kwenye Uchaguzi Mkuu 2015 -
Sophia Simba, Madabida wavuliwa uanachama CCM. Emmanuel Nchimbi apewa onyo kali
Nchimbi alipomkataa Magufuli automatically alikuwa amemkataa Samia pia. Leo hii Samia baada ya kuwa Rais kutokana na kifo cha Magufuli, amepitishwa kuwa mgombea uchaguzi mkuu, huku Nchimbi akichaguliwa kama mgombea mweza?
Pia soma: Pre GE2025 - CCM yamchagua Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza katika Uchaguzi wa Oktoba 2025
Kwanini? Ni kumkomesha alambe matapishi yake? Mchawi kapewa mwana alee? Au ni vile alivyosema Sarungi, kuwa amewekwa hapo kuuliwa kabisa kisiasa, akiwekwa hapo shughuli hakuna, kazi ni kutumwa tu kwenda kutabasamu kwenye mikutano akitoka hapo tunasikia amechoka sana "Ameomba kupumzika", shughuli imeisha?