Uchaguzi 2020 Ndani ya mwezi mmoja tu Tundu Lissu ameweza kufanya aliyoshindwa Magufuli kwa miaka mitano

Uchaguzi 2020 Ndani ya mwezi mmoja tu Tundu Lissu ameweza kufanya aliyoshindwa Magufuli kwa miaka mitano

fazili

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2011
Posts
16,427
Reaction score
22,418
Tunajua kwamba hata Magufuli anaposema "Nitajenga barabara" haimaanishi kwamba yeye ndiye mwenye hela au kwamba atakuwa saiti akijenga. Anatumia vyombo vilivyopo kujenga barabara n.k.

Tundu Lissu amefanikiwa kwa ushawishi wake na umahiri mkubwa wa kujenga hoja zinazowafanya waliopo madarakani kuamka usingizini na kuanza kutekeleza mara moja maono ya Lissu kwani wanajua ndio matakwa ya wananchi. Kwa hili, Lissu amefanikiwa kufanya aliyoshindwa kufanya Magufuli kwa miaka mitano:

1. Walimu 13,000 ambao serekali imetangaza kuwapa ajira mpya wiki juzi

2. Wamachinga ambao Magufuli kawaambia si lazima tena kulipia elfu 20 kupata kitambulisho wiki jana

3. Kuanzia mwezi huu mshahara kima cha chini serekalini umepanda

4. Watu kujisikia huru tena na kuthubutu hata kumkosoa Rais hadharani

5. Chama cha Mapinduzi kutambua kuwa hakijafanya wanayotaka wananchi na kwamba matatizo ya msingi ya wananchi hayajaguswa

6. Lissu ameifanya CCM kugundua kuwa ni chama kisichopendwa na wengi na hakina hati miliki ya siasa za Tanzania

7. Kwamba hakuna mtu anayeweza kuuwa upinzani na harakati za kisiasa isipokuwa wanachi wenyewe.

8. Serikali kugundua kwamba kujaribu kuuzima upinzani ndio kuufanya uwe imara na wenye nguvu zaidi

9. Watu wameelewa kuwa vyama vya upinzani ni muhimu hata kama chama tawala kinaongozwa na "malaika".

10. Kwa mara ya kwanza baada ya kuwa anawafokea tu kwa miaka 5, watanzania wamemwona mgombea urais wa CCM akiongea nao kwa kuwabembeleza, haya ni mafanikio makubwa kwa Lissu ndani ya mwezi mmoja tu.
 
Yan within a month maji safi everywhere.. umeme, lami, all graduate wanaajiriwa wa elimu ya juu na wakati.

Guys ur overrating him its not fair kwake pia.
 
Lissu akiwa mgombea tu amedhihirisha kuwa sera za Chadema zina hoja na mashiko na amemfanya Meko kutekeleza baadhi ya ahadi/sera zake ili kupunguza kishindo cha kampeni, sasa tumuunge mkono Lissu kwa kura 28 oct 2020.
 
*"Kwa mara ya kwanza baada ya kuwa anawafokea tu kwa miaka 5, watanzania wamemwona mgombea urais wa CCM akiongea nao kwa kuwabembeleza"
 
Spana za Lissu si mchezo! Si walikuwa wanapiga kelele eti maendeleo ya vitu!! Kiko wapi sasa??😂😂😂😂

Ndo mana tukisema Lissu ni mteule wa Mungu mataga inabidi wawe wanatuelewa saaana!

Ndani ya miezi mwezi mmoja tu wa kampeni za Lissu, wamachinga wameambiwa vitambulisho si lazima, ajira za walimu 13000 zimetoka, madaktari 1000 wameitwa kazini , watumishi wameanza kulipwa malimbikizo na kupandishwa madaraja na huko mikoani amri ya kujenga barabara zinatolewa.

Watanzania tuna kila sababu ya kumchagua Tundu Antiphas Lissu mwaka huu!!!

Ni yeye 🔥
 
*"Kwa mara ya kwanza baada ya kuwa anawafokea tu kwa miaka 5, watanzania wamemwona mgombea urais wa CCM akiongea nao kwa kuwabembeleza"
Sasa hivi anatamani hata apige magoti kuomba kura , urais mtamu jamani lakini ndio hivyo watu wamechoka utawala wa kihutu .
 
Back
Top Bottom