Ndege ya ATCL number TC 106 Bomberdier, tairi moja ni kipara mpaka nyuzi zinaonekana kabisa

Ndege ya ATCL number TC 106 Bomberdier, tairi moja ni kipara mpaka nyuzi zinaonekana kabisa

Hii ni hatari kuliko wanavyodhani. Hapo Engineer aliekagua na kujaza log book ahojiwe. Rubani pia anatakiwa kuhojiwa kwanini aruhusu kuruka na tairi kama Hilo.

Nafikiri Matindi na Timu yake wajichunguze
 
Jana nimesafiri na ATCL ndege number TC 106 Bomberdier toka Dar kuja Mbeya. Hii ndege tairi moja ni kipara mpaka nyuzi zinaonekana kabisa. Hii ni hatari sana.
Nilikaa dirishani mkabala na hizi tairi. Jana tulitoka Dar na mvua, na mipira ikiloa si rahisi kuona jinsi mpira ulivyolika. Tunafika, mipira imekauka. Ilivyotoa tairi nikaona jinsi ilivyoisha. Nilikosa amani mpaka ilipo simama.
Hata kama ni tubeless, nadhani kuna kiwango kinacho ruhusiwa cha tairi kulika. Kwa namna zilivyo hapo, hata uwiano wa kubeba mzigo wakati wa kutua ni tofauti. Sababu hiyo tairi isiyolika sana ndio inaanza kugusa chini na kubebe mzigo mkubwa. Hebu fikiria ndege imetua na hiyo tairi inapiga mzinga wakati iko kwenye speed. Au iko kwente speed ya kuruka halafu ndiyo ina piga mzinga. ATCL mtatuuwa kizembe.
View attachment 2197854

View attachment 2197855

Habari hii imfikie kamanda Mkuu wa wale wabrashi viatu maarufu, kamanda Mutafungwa.
 
Labda Traffic waruhusiwe kufanya ukaguzi wa tairi za ndege la sivyo ni mwendo wa mazoea
 
Jana nimesafiri na ATCL ndege number TC 106 Bomberdier toka Dar kuja Mbeya. Hii ndege tairi moja ni kipara mpaka nyuzi zinaonekana kabisa. Hii ni hatari sana.
Nilikaa dirishani mkabala na hizi tairi. Jana tulitoka Dar na mvua, na mipira ikiloa si rahisi kuona jinsi mpira ulivyolika. Tunafika, mipira imekauka. Ilivyotoa tairi nikaona jinsi ilivyoisha. Nilikosa amani mpaka ilipo simama.
Hata kama ni tubeless, nadhani kuna kiwango kinacho ruhusiwa cha tairi kulika. Kwa namna zilivyo hapo, hata uwiano wa kubeba mzigo wakati wa kutua ni tofauti. Sababu hiyo tairi isiyolika sana ndio inaanza kugusa chini na kubebe mzigo mkubwa. Hebu fikiria ndege imetua na hiyo tairi inapiga mzinga wakati iko kwenye speed. Au iko kwente speed ya kuruka halafu ndiyo ina piga mzinga. ATCL mtatuuwa kizembe.
View attachment 2197854

View attachment 2197855
Wakirudi watakuja na spare.
 
Kibongobongo tairi mpk litoboke ndio wanareplace.

Mambo ya kufuata global standards za kureplace matairi baada ya ndege kuruka hewani idadi flani ya masaa wala ATCL hawana habari nayo.

Labda mpaka utokee mzinga ndio watapata akili. Ila as usual, tutasema ni “mipango ya Mungu”
 
Stori kama stori uwe ndani uone tairi hili ajabu jingine la dunia hongera kupanda nawe kunguru
Ajabu gani? Kutegemea na ulipokaa, mbona tairi unaziona kabisa kabla hazijakunjwa baada ya ndege kupaa; au matairi yakikunjuliwa wakatii ndege inakaribia kutua. Zaidi ya hayo, mtoa mada amekupa na picha ya hizo tairi. Sasa ubishi wa nini?
 
Badala ya kutatua Tatizo utashangaa Mtoa mada(taarifa) anatafutwa atekwe na awekwe ndani bila dhamana.

Nchi yetu ina shida
Tulishapita hizo stage za kishamba Sasa hivi tunaongea American English through the nose.
(It want tourism it show royal tour, the tourist come mwamwamwa, the us dollar twatwatwa full)
 
HUOGOPI KUTEKWA NA KUULIWA? ACHA NDEGE ZIPIGE MZIGO... PUNDA AFE MZIGO UFIKE.
 
kwani tairi za ndege zinauzwa pesa ngapi halafu kweli hili akina Zitto & Pascal Mayalla wameshindwaje kulisemea wakati wao wanapanda pipa kila week
Unapopanda ndege jua kuwa TCAA wameshajiridhisha na usalama wa ndege husika. Kuwa na amani kabisa.
Hiyo tairi bado ni nzima sana. Kuonekana hizo nyuzi siyo kigezo. Tairi hizi ni ngumu mno.
 
Tulishapita hizo stage za kishamba Sasa hivi tunaongea American English through the nose.
(It want tourism it show royal tour, the tourist come mwamwamwa, the us dollar twatwatwa full)

Haichekeshi ila acha nifurahi[emoji38][emoji38][emoji38]
 
Back
Top Bottom