Ndege ya Tanzania yakamatwa nje, Taifa ladaiwa bilioni 380 kwa kuvunja mkataba bila utaratibu

Ngoja mtaalamu wa negotiations Prof Kabudi aende akaikomboe

Kuna maamuzi yanafanywa na Serikali utasema haina Mwanasheria Mkuu wa Kuishauri.

At the end tunaingia hasara Kubwa kama hivyo
 
Hili balaa lililetwa na yule mzalendo uchwara katika jitihada zake za kusaka political millage.
 
Hatuna kitu, tunajaribu kukopa kwao napo shida tu bado hata kidogo kilichopo kinapitiwa.

Mi nadhani wawekezaji wa nje mikataba yao iwe wazi hadi kwa wananchi ili tujue kilichomo. Sio waziri na katibu wanasainishana huko ofisi matokeo yake upande flani ukimkwaza mwingine mwananchi ndo anakipata cha moto.

Sasa ona makubaliano yafanyike kimya kimya na huyo mwekezaji bila mwananchi kujua ila likitokea gogoro lo lote suluhu inafanyikia nje ya nchi.
Haya ndege imekamatwa ndo sasa mwananchi anajulishwa! Upuuzi mtupu!

Swali:
Huyo muwekazaji alikuja utawala upi au awamu ipi?

N.B
Ujengwe utaratibu wa viongozi kuwajibishwa!
 
Ngoja mtaalamu wa negotiations Prof Kabudi aende akaikomboe

Kuna maamuzi yanafanywa na Serikali utasema haina Mwanasheria Mkuu wa Kuishauri.

At the end tunaingia hasara Kubwa kama hivyo

Huyo si aliwekwa pembeni
Labda ila sidhani kama atakubali wana hasira hao kwa sasa!
 
Tatizo kwa uongozi wa Magufuli, nikiambiwa kwamba huo mkataba ulivunjwa bila hata kuangalia uvunjaji strategically sitashangaa. Yani kama umevunjwa kwa "amri kutoka juu" tu, sitashangaa.

Na kwa sheria zetu mambo ya ardhi, rais ndiye muhifadhi wa mwisho, kwa hiyo ana haki hiyo, kikatiba.

Lakini, kama mkataba una clause inayosema kwamba kama kuna dispute, arbitration iwe mahakama za kimataifa, na mahakama za kimataifa hazitambui habari za "amri kutoka juu" kutoka serikali ya Tanzania, hapo imekula kwetu.

Tatizo si tu mikataba inavunjwa. Kuna namna ya kuvunja mikataba na kushinda kesi ya arbitration, kwa sababu unavunja mkataba kwa kutumia clauses za mkataba.

Mimi miaka fulani mzee wangu alishiriki kuongoza kutetea kesi moja kubwa sana ya arbitration ya Tanzania London, ni kati ya kesi chache ambazo Tanzania imeshinda arbitration. Alisema hii mikataba ikifikia international arbitration, ni vigumu sana nchi kushinda, kwa wakati huo, ilikuwa kama 9 times out of 10 arbitration za London Court of International Arbitration zinaishia kwa wafanyabiashara kushinda.

Lakini, kwa uvunjaji wa Magufuli ambao sasa kamrithisha Samia habari za "mkitubana kwa sehria za nje, tutawabana kwa sheria za ndani", tunavunja mikataba kijinga.

So, tatizo si tu tunavunja mikataba. Hata tunapovunja mikataba hatuvunji strategically. Inakuwa kama rais anaamini nguvu zake za kikatiba kuwa last custodian of the land zinakubalika mpaka London!

Mimi nafikiri ni wakati sasa wananchi wa Tanzania watumie international arbitration clauses katika mikataba na serikali, kuondokana na usumbufu na uonevu wa maamuzi ya "amri kutoka juu".
 


Hii Ndege Nayo Ilifuata Nini Uholanzi

Ni Kiherehere Kimeiponza Mpaka Ishikiriwe Huko
Aliyeipeleka Airudishe Home Chao
 
Huyo si aliwekwa pembeni
Labda ila sidhani kama atakubali wana hasira hao kwa sasa!
Shida ya Viongozi wetu ni Bendera fuata Upepo.

Huyu Kabudi amebadirika mtazamo baada ya late JPM kututoka.

Ingawa katika watu wa kulaumiwa kuhusu hili huyo Prof ni wa Kwanza, alikuwa Mshauri Mkuu wa JPM kuhusu Masuala mengi ya Nchi
 
Hii nchi sabotage zinaanzia ndani! Wapiga deal wanaumiza Taifa ...
Tumewapa dhamana ya kulinda Taifa letu matokeo yake wamekuwa ndio mawakala wa kuuza ramani kwa majambazi.
 
Na bado!,

Kuna zingine zitadakwa kwa mikono ya mafisadi ya CCM kupitia mgongo wa mabeberu!
Kumbe ni njama za wizi wa kodi zetu

Haya madeni yalisababishwa na yule kiongozi muovu aliyeko motoni.
 
Ou

Iuzwe
 
ATCL hawana ndege hata 1, zote wamekodi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…