Ndege zilizotengenezwa Tanzania, zinauzwa milioni 500, Kwa bei hii wewe tu 'Upae au daladala'

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Thamani ya ndege moja aina ya Skyleader 600 ambayo imetengenezwa nchini Tanzania, imetajwa kuwa ni zaidi ya Dola za kimarekani 220,000 sawa na shilingi milioni 500 za Kitanzania.

Gharama Thamani ya ndege moja aina ya Skyleader 600 ambayo imetengenezwa nchini Tanzania, imetajwa kuwa ni zaidi ya Dola za kimarekani 220,000 sawa na shilingi milioni 500 za Kitanzania,

Bei inayolinganishwa na gari zenye gharama kubwa zaidi kama vile V8 land cruiser, defender na Range rover.

Afisa Mawasiliano kwa umma katika kampuni ya utengenezaji wa ndege hizo ya Airplanes Africa Limited, Bw. Freddie Monento ametoa ufafanuzi huo katika kipindi cha "Wekeza Tanzania" ambapo ameweka wazi kuwa kwa sasa ndege hizo zinavibali na zimethibitishwa kuruka.
Your browser is not able to display this video.
 
Vibali nitapata je?
Wanakaa watu wangapi

Nimeona kama rubani tu

Nafikiria nilitaka kwenda kijijini nitashukia wapi?

Serikali watatoa kibali cha kutengeza runway yangu shambani kwangu

Watoe info zaidi sio eti kama una gari fulani basi mtu ununue tu ndege yao..

Yalitojificha gharama aseme kiuwazi

Natumaini wana tangazo zaidi ya hii ya kama taarifa ya habari. Maana hawjaonyssha kitu bali sura na ndege zimelala..
 
Ukienda kijijini utashuka na parachute, lakini hata kwenye njia ya waendesha baiskeli ndege yetu inaweza kutua
 
Tokea uneacha kushabikia ccm umeanza kuwa na akili kichwani.
 
Kununua hiyo ndege naamini wapo wengi tu wanaoweza. Hata humu JF. Lakini gharama za kuimiliki (mafuta, servicing, matengenezo, vibali, rubani, parking nk) ndivyo vyaweza kuwa changamoto kubwa kwa asiye na mabilioni mengi.
 
Hivi ni vishada na siyo ndege.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…