Ndio Maana Wanaume Tunakufa Mapema

Ndio Maana Wanaume Tunakufa Mapema

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
6,514
Reaction score
15,247
Tangu tukiwa wadogo tumekuwa tukiambiwa wewe ni mtoto wa kiume Acha Kulialia jikaze, tangu lini umeona mtoto wa kiume analalamika hovyo! Haya na mengine mengi yamemjenga mtoto wa kiume kumeza machungu yake yeye mwenyewe pasina kuomba msaada Kwa watu wengine,kumemfanya kupambana na mitihani mbali mbali pasina kupata ushauri au muongozo toka Kwa watu wengine.

Na Hali hii tunakutana nayo huku ukubwani na kuendelea na mambo Yale Yale ambayo tumekuwa tukiambiwa tangu tukiwa wadogo. Matokeo yake vifua vyetu vimejaa mizigo mizito ivunjayo mbavu zetu,tumejawa na misongo ya mawazo,na hatujui wapi PA kupata msaada na ushauri,kwasababu nafsi zetu zinatusuta Kwa kutuambia Sisi ni wanaume hatupaswi kuomba msaada wala ushauri toka Kwa watu wengine.

Matokeo yake tunapata maradhi ya moyo na mengineyo kutokana na mizigo ambayo tumeibeba katika vifua vyetu,tunajikuta kutwa kucha Sisi ni watu WA stress Tu.

Sasa ukikuta mwanaume anaomba ushauri WA changamoto Fulani ambayo anakutana nayo basi jua kweli anahitaji msaada,kwahiyo sio Busara na sio vizuri kumwambia wewe ni mwanaume tatua changamoto zako mwenyewe au huo sio uanaume pambana na Hali yako.

Hapa tunakosea Sana,ifike kipindi tujue nasi ni wanadamu pia tuna hisia na tunapata changamoto pia,hivyo tuachane na zile fikra za kusema kuwa mwanaume inabidi ugangamale,mwanaume unatakiwa ukomae na shida zako,hapana tuna feli Sana tena Sana.

Ukiona mwanaume ima anatuma post humu na kuomba ushauri basi ujue yupo ktk changamoto kubwa Sana na kapambana mwenyewe na hakupata suluhu,kwahiyo na wewe usiwe sehemu ya kumuongezea tatizo.

Tofauti na wanawake wao ni watu ambao wanashea Sana mambo Yao na hivyo kuwafanya vifua vyao viwe vyepesi na kupata msaada pia,unajua wakati mwingine unacho hitaji ni kusikilizwa Tu,Kwa kufanya hivyo unakuwa umepunguza stress kiasi Kikubwa,sasa wanaume mambo hayo hatuna na ndio yanayo tupelekea kupata msongo WA mawazo na hatimaye kufa kabisa.

Kuwa wanaume haimaanishi kuwa tuishi kama robot au tupambane wenyewe Tu Bila kuomba au kupata msaada toka Kwa wengine laa hasha!
Nasi pia inafika kipindi data kichwani zinazima na kushindwa kutatua changamoto mbali mbali.

Nimekuwa inspired kuandika haya maudhui baada ya kuona baadhi ya wanaume humu kuwasemea kauli mbovu wanaume wenzao pale wanapokutana na changamoto mbali mbali nakutaka ushauri .

Tubadilike na kumfanya mwanaume aondokane na Mila na desturi mbaya ambayo huchangia anguko lake hapa duniani.

Ni hayo Tu!
 
Sasa tajiri, unakuta mwanaume anaomba ushauri kwa wanaume sisi sisi ambao pia tuna matatizo na tunakufa nayo mioyoni, unahisi tutamwambia nin zaidi ya kukomaa nayo?
 
Sasa tajiri, unakuta mwanaume anaomba ushauri kwa wanaume sisi sisi ambao pia tuna matatizo na tunakufa nayo mioyoni, unahisi tutamwambia nin zaidi ya kukomaa nayo?
Ni kweli kabisa usemayo,lakini wakati mwingine kama tungeshea matatizo yetu huenda Kwa pamoja ima tungefarijiana au kupata njia ya kupata suluhisho

We angalia hata watu wengi ambao wanajiua ni Wale ambao wamejifungia Tu chumbani wenyewe na kuugulia maumivu Yao,Lau wangeshea huenda wangeona solution mapema Sana,unajua ukiwa umebanwa Sana na changamoto hata fikra zako zinagota lkn ukishea na mtu WA karibu anakusaidia kutafakari upya na kuliangalia Jambo katika mtazamo chanya zaidi
 
Hasa huku JUU wanaume wanapambana sna na kutafuta maisha mpk wanakufa kwa presha, sugar n.k
Tofauti na huko PWANI, huku JUU amini na kwambia familia nyingi wamebaki wajane
 
Ni kweli kabisa usemayo,lakini wakati mwingine kama tungeshea matatizo yetu huenda Kwa pamoja ima tungefarijiana au kupata njia ya kupata suluhisho

We angalia hata watu wengi ambao wanajiua ni Wale ambao wamejifungia Tu chumbani wenyewe na kuugulia maumivu Yao,Lau wangeshea huenda wangeona solution mapema Sana,unajua ukiwa umebanwa Sana na changamoto hata fikra zako zinagota lkn ukishea na mtu WA karibu anakusaidia kutafakari upya na kuliangalia Jambo katika mtazamo chanya zaidi
Shida wabongo ni masnichi sana kwa kias kikubwa. Ukienda kueleza mashida zako unakua unajiweka uchi sokoni.
Kungekua na wale matherapist wengi zaidi ingekua nafuu maana watu wangeenda for counselling.
Na pia hakuna awareness kwa ajili ya afya ya akili, ukimwambia mtu alipe lets say 30k for 1 hour of therapy atakuona uko unga maana 30 hyo hyo inanunua serengeti lite kreti nzima. Do u think mtu wa kawaida atachagua nin?
 
Kuna mambo nasikitisha sana kwa upande wetu tunapitia changamoto mno..unaweza Kuta mtoto wa kiume ni watatu ila ana dada zake wakubwa wawili wamemtangulia basi hawa wadada wanajifanya kama mambo ya kuwasaidia wazazi wamejitoa mapema maana akili yao wakifeli shule na kimaisha wataolewa...basi wanaanza kumpa mizigo huyo dogo yao utasikia "soma sana kwa juhudi uje kukomboa familia wewe ndo mtoto wa kiume ""

Dogo wa kiume unajikita unapambana hata kama utafeli shule unaingiza mtaani ..miaka kadhaa mbele unapata angalau pesa ya kula na unaendesha Maisha ,sasa wale dada zako unakuta waliolewa wakaachwa na watoto hawana mishe kama elimu walichezea ,wanakuja kuwe mzigo kwako mtoto wa kiume Tena watakupiga vizinga ,hapo wewe ndo mdogo kisa tu mwanaume.
 
Kuna mambo nasikitisha sana kwa upande wetu tunapitia changamoto mno..unaweza Kuta mtoto wa kiume ni watatu ila ana dada zake wakubwa wawili wamemtangulia basi hawa wadada wanajifanya kama mambo ya kuwasaidia wazazi wamejitoa mapema maana akili yao wakifeli shule na kimaisha wataolewa...basi wanaanza kumpa mizigo huyo dogo yao utasikia "soma sana kwa juhudi uje kukomboa familia wewe ndo mtoto wa kiume ""

Dogo wa kiume unajikita unapambana hata kama utafeli shule unaingiza mtaani ..miaka kadhaa mbele unapata angalau pesa ya kula na unaendesha Maisha ,sasa wale dada zako unakuta waliolewa wakaachwa na watoto hawana mishe kama elimu walichezea ,wanakuja kuwe mzigo kwako mtoto wa kiume Tena watakupiga vizinga ,hapo wewe ndo mdogo kisa tu mwanaume.
Hii Generation ya hovyo

Dada zetu wanatia huruma Sana na wapo depressed Sana
 
Wanaume hawafi mapema kwa sababu ya kuficha machungu moyoni ! Tunakufa kwa sababu ya shughuli hatarishi tunazofanya !
Asilimia kubwa ya watu jeshini ni wanaume , kazi za ujenzi (saidia fundi) , wazibua vyoo ni wanaume ! Mieleka 90% wanaume , wezi na majambazi 99% ni wanaume ! Magaidi wote duniani ni wanaume , Madictator wote waliowahi kutikisa dunia ni wanaume !!
Haya malizia wanaosomesha wachumba 99% ni wanaume ! 😃😃 Life expectancy lazima iwe ndogo !!
 
Hasa huku JUU wanaume wanapambana sna na kutafuta maisha mpk wanakufa kwa presha, sugar n.k
Tofauti na huko PWANI, huku JUU amini na kwambia familia nyingi wamebaki wajane
Kweli mkuu nakubaliana na wewe kabisa,hakika Hali inatisha Sana mkuu
 
Shida wabongo ni masnichi sana kwa kias kikubwa. Ukienda kueleza mashida zako unakua unajiweka uchi sokoni.
Kungekua na wale matherapist wengi zaidi ingekua nafuu maana watu wangeenda for counselling.
Na pia hakuna awareness kwa ajili ya afya ya akili, ukimwambia mtu alipe lets say 30k for 1 hour of therapy atakuona uko unga maana 30 hyo hyo inanunua serengeti lite kreti nzima. Do u think mtu wa kawaida atachagua nin?

Umeongea mambo ya msingi Sana mkuu

Kwanza ni Hilo la kutotunziana Siri,kweli kuna watu ambao hufarahia matatizo ya wengine na kutaka kutangaza

Ndio maana Tunatakiwa tuangalie ni watu gani WA kushea nao mambo yetu na wapi WA kuwa epuka,hili ni Jambo la msingi sana kabla huja Shea chochote na mtu.

Lakini naamini kabisa katika watu 20 hutakosa mmoja ambaye atakuwa msiri wako

Lingine ni Hilo la wataalamu WA maswala ya afya ya akili,ni kweli kabisa watu hawa ni muhimu Sana lakini bahati mbaya katika inchi zetu hizi bado hawajapewa kipaumbele Sana,Ila kuna umuhimu Sana WA kuwa na watu kama hawa ili jamii yetu iweze kupona kutokana na changamoto hizi ambazo kila kukicha zinaongezeka
 
Kuna mambo nasikitisha sana kwa upande wetu tunapitia changamoto mno..unaweza Kuta mtoto wa kiume ni watatu ila ana dada zake wakubwa wawili wamemtangulia basi hawa wadada wanajifanya kama mambo ya kuwasaidia wazazi wamejitoa mapema maana akili yao wakifeli shule na kimaisha wataolewa...basi wanaanza kumpa mizigo huyo dogo yao utasikia "soma sana kwa juhudi uje kukomboa familia wewe ndo mtoto wa kiume ""

Dogo wa kiume unajikita unapambana hata kama utafeli shule unaingiza mtaani ..miaka kadhaa mbele unapata angalau pesa ya kula na unaendesha Maisha ,sasa wale dada zako unakuta waliolewa wakaachwa na watoto hawana mishe kama elimu walichezea ,wanakuja kuwe mzigo kwako mtoto wa kiume Tena watakupiga vizinga ,hapo wewe ndo mdogo kisa tu mwanaume.


Mkuu we Acha Tu! Kuwa mwanaume ni Jambo lingine kabisa

Ndio maana familia ambayo hawaja jaliwa kijana wa kiume huwa Wana stress Fulani hivi,wanaweza kukomaa kuzaa mpaka apatikane kidume.

Kifupi wanaume tuna changamoto nyingi Sana,Mungu atufanyie wepesi kwakweli.

Wanaume wote waishi Maisha marefu.
 
Wanaume hawafi mapema kwa sababu ya kuficha machungu moyoni ! Tunakufa kwa sababu ya shughuli hatarishi tunazofanya !
Asilimia kubwa ya watu jeshini ni wanaume , kazi za ujenzi (saidia fundi) , wazibua vyoo ni wanaume ! Mieleka 90% wanaume , wezi na majambazi 99% ni wanaume ! Magaidi wote duniani ni wanaume , Madictator wote waliowahi kutikisa dunia ni wanaume !!
Haya malizia wanaosomesha wachumba 99% ni wanaume ! 😃😃 Life expectancy lazima iwe ndogo !!
Sawa mkuu hayo nayo ni miongoni mwa changamoto zetu
 
Back
Top Bottom