Etugrul Bey
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 6,514
- 15,247
Tangu tukiwa wadogo tumekuwa tukiambiwa wewe ni mtoto wa kiume Acha Kulialia jikaze, tangu lini umeona mtoto wa kiume analalamika hovyo! Haya na mengine mengi yamemjenga mtoto wa kiume kumeza machungu yake yeye mwenyewe pasina kuomba msaada Kwa watu wengine,kumemfanya kupambana na mitihani mbali mbali pasina kupata ushauri au muongozo toka Kwa watu wengine.
Na Hali hii tunakutana nayo huku ukubwani na kuendelea na mambo Yale Yale ambayo tumekuwa tukiambiwa tangu tukiwa wadogo. Matokeo yake vifua vyetu vimejaa mizigo mizito ivunjayo mbavu zetu,tumejawa na misongo ya mawazo,na hatujui wapi PA kupata msaada na ushauri,kwasababu nafsi zetu zinatusuta Kwa kutuambia Sisi ni wanaume hatupaswi kuomba msaada wala ushauri toka Kwa watu wengine.
Matokeo yake tunapata maradhi ya moyo na mengineyo kutokana na mizigo ambayo tumeibeba katika vifua vyetu,tunajikuta kutwa kucha Sisi ni watu WA stress Tu.
Sasa ukikuta mwanaume anaomba ushauri WA changamoto Fulani ambayo anakutana nayo basi jua kweli anahitaji msaada,kwahiyo sio Busara na sio vizuri kumwambia wewe ni mwanaume tatua changamoto zako mwenyewe au huo sio uanaume pambana na Hali yako.
Hapa tunakosea Sana,ifike kipindi tujue nasi ni wanadamu pia tuna hisia na tunapata changamoto pia,hivyo tuachane na zile fikra za kusema kuwa mwanaume inabidi ugangamale,mwanaume unatakiwa ukomae na shida zako,hapana tuna feli Sana tena Sana.
Ukiona mwanaume ima anatuma post humu na kuomba ushauri basi ujue yupo ktk changamoto kubwa Sana na kapambana mwenyewe na hakupata suluhu,kwahiyo na wewe usiwe sehemu ya kumuongezea tatizo.
Tofauti na wanawake wao ni watu ambao wanashea Sana mambo Yao na hivyo kuwafanya vifua vyao viwe vyepesi na kupata msaada pia,unajua wakati mwingine unacho hitaji ni kusikilizwa Tu,Kwa kufanya hivyo unakuwa umepunguza stress kiasi Kikubwa,sasa wanaume mambo hayo hatuna na ndio yanayo tupelekea kupata msongo WA mawazo na hatimaye kufa kabisa.
Kuwa wanaume haimaanishi kuwa tuishi kama robot au tupambane wenyewe Tu Bila kuomba au kupata msaada toka Kwa wengine laa hasha!
Nasi pia inafika kipindi data kichwani zinazima na kushindwa kutatua changamoto mbali mbali.
Nimekuwa inspired kuandika haya maudhui baada ya kuona baadhi ya wanaume humu kuwasemea kauli mbovu wanaume wenzao pale wanapokutana na changamoto mbali mbali nakutaka ushauri .
Tubadilike na kumfanya mwanaume aondokane na Mila na desturi mbaya ambayo huchangia anguko lake hapa duniani.
Ni hayo Tu!
Na Hali hii tunakutana nayo huku ukubwani na kuendelea na mambo Yale Yale ambayo tumekuwa tukiambiwa tangu tukiwa wadogo. Matokeo yake vifua vyetu vimejaa mizigo mizito ivunjayo mbavu zetu,tumejawa na misongo ya mawazo,na hatujui wapi PA kupata msaada na ushauri,kwasababu nafsi zetu zinatusuta Kwa kutuambia Sisi ni wanaume hatupaswi kuomba msaada wala ushauri toka Kwa watu wengine.
Matokeo yake tunapata maradhi ya moyo na mengineyo kutokana na mizigo ambayo tumeibeba katika vifua vyetu,tunajikuta kutwa kucha Sisi ni watu WA stress Tu.
Sasa ukikuta mwanaume anaomba ushauri WA changamoto Fulani ambayo anakutana nayo basi jua kweli anahitaji msaada,kwahiyo sio Busara na sio vizuri kumwambia wewe ni mwanaume tatua changamoto zako mwenyewe au huo sio uanaume pambana na Hali yako.
Hapa tunakosea Sana,ifike kipindi tujue nasi ni wanadamu pia tuna hisia na tunapata changamoto pia,hivyo tuachane na zile fikra za kusema kuwa mwanaume inabidi ugangamale,mwanaume unatakiwa ukomae na shida zako,hapana tuna feli Sana tena Sana.
Ukiona mwanaume ima anatuma post humu na kuomba ushauri basi ujue yupo ktk changamoto kubwa Sana na kapambana mwenyewe na hakupata suluhu,kwahiyo na wewe usiwe sehemu ya kumuongezea tatizo.
Tofauti na wanawake wao ni watu ambao wanashea Sana mambo Yao na hivyo kuwafanya vifua vyao viwe vyepesi na kupata msaada pia,unajua wakati mwingine unacho hitaji ni kusikilizwa Tu,Kwa kufanya hivyo unakuwa umepunguza stress kiasi Kikubwa,sasa wanaume mambo hayo hatuna na ndio yanayo tupelekea kupata msongo WA mawazo na hatimaye kufa kabisa.
Kuwa wanaume haimaanishi kuwa tuishi kama robot au tupambane wenyewe Tu Bila kuomba au kupata msaada toka Kwa wengine laa hasha!
Nasi pia inafika kipindi data kichwani zinazima na kushindwa kutatua changamoto mbali mbali.
Nimekuwa inspired kuandika haya maudhui baada ya kuona baadhi ya wanaume humu kuwasemea kauli mbovu wanaume wenzao pale wanapokutana na changamoto mbali mbali nakutaka ushauri .
Tubadilike na kumfanya mwanaume aondokane na Mila na desturi mbaya ambayo huchangia anguko lake hapa duniani.
Ni hayo Tu!