Ndoa halali, ndoa batili na ndoa batilifu. Je, wajua pia kuna msamaha halali wa kweli, msamaha batili na msamaha batilifu? Msamaha ule ni batilifu!

Ndoa halali, ndoa batili na ndoa batilifu. Je, wajua pia kuna msamaha halali wa kweli, msamaha batili na msamaha batilifu? Msamaha ule ni batilifu!

Najua jamaa alikuita kwenye ile kamati yake enzi za utukufu wake, lakini asamehewe tu kama alivyoomba. Amekosa jamani, amekosa sana, wazanzibari ..... I mean watanzania tumsamehe.
 
Pascal leave the speaker alone...usitumie hii kama fimbo ya kumuadhibu, hata kama hukustahili kuhojiwa wakati ule msamehe tu.
 
Kwa kinachoendelea hapa ikulu busara kwa Ndungai ni kujiuzuru tu hakuna kingine anaweza fanya kurekebisha mambo
 
Kilichomtoa mayala kwenye ramani ni hizi riwaya zake za kutetea waovu na kujipendekeza kwa watawala.

Wewe Mayala utafika mbinguni unachachamaa
 
.
Je, Wajua Kuna Msamaha wa Kweli, Msamaha Batili na Msamaha Batilifu?
Sasa kama ilivyo kwenye ndoa, si wengi wanaojua kuwa kwenye msamaha, pia kuna msamaha wa kweli, msamaha batili na msamaha batilifu.
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amewaomba radhi wananchi na wapenda demokrasia nchini kutokana na kauli aliyoitoa kuwa si lazima CCM ishinde kura kwenye boksi, bali kuna njia nyingine zikiwemo alizosema za haramu.

Akizungumza kupitia video aliyorekodi, leo Jumatano Julai 17, 2024 Nape ameomba radhi wote walikerwa na kauli yake.

“Nimeuona mjadala kwenye mitandao, lakini kama nilivyosema kauli ile ilikuwa utani lakini naona umekuwa mjadala mrefu wakati huu kwa sababu tunaelekea katikia uchaguzi. Nawapa pole ambao wamesumbuliwa na kuteseka na huu mjadala, nawapa pole na naomba radhi, nasisitiza haikuwa serious,”amesema Nape.

Nape aliyewahi kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi na Uenezi, alitoa kauli hiyo iliyoibua mjadala juzi Julai 15, 2024 usiku alipotembelea soko la Kashai mkoani Kagera na kuzungumza na wananchi.

Muktadha wa kauli hiyo ilikuwa ni kuwahakikishia ushindi wa Mbunge wa Bukoba Mjini, Stephen Byabato katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2025, Nape ambaye kwa sasa ni Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye alisema:

“Unajua nyie sikilizeni, matokeo ya kura sio lazima yawe ya kwenye boksi, inategemea nani anahesabu na kutangaza. Na kuna mbinu nyingi kuna halali, nusu halali na kuna haramu na zote zinaweza kutumika ilimradi tu mkishamaliza, unamwambia Mwenyezi Mungu nisamehe pale nilipokosea,” alisema.

Kauli hiyo ya Nape, ilipingwa jana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla ambaye alisema kauli hiyo haitokani na msimamo wa chama hicho.

“Kuna kiongozi nimemsikia huko mitandaoni anasema eti ushindi wa uchaguzi hautokani na kura za kwenye boksi, mimi nataka nimwambia hiyo kauli isitazamwe kuwa inatokana na CCM,” alisema Makalla.

Hii si mara ya kwanza kwa Nape kutoa kauli tata zenye kuzua mjadala katika kipindi cha kuelekea uchaguzi, hata Juni 2015, akiwa ziarani Sengerema alisema “CCM ingeshinda uchaguzi mwaka huo hata kwa bao la mkono.”

Pia soma
  1. Kuelekea 2025 - Nape Nnauye: Kauli ya "Matokeo ya kura inategemea nani anahesabu na nani anatangaza" ilikuwa ni ya utani
  2. Kuelekea 2025 - Nape Nnauye: Matokeo ya kura inategemea nani anahesabu na nani anatangaza, ili mradi ukimaliza unasema Mungu nisamehe!
Hata msamaha huu ni msamaha batili!, kwasababu kilichosemwa ni kitu cha ukweli kabisa, kimesemwa kwa kudhamiriwa, kitendo cha kusema it was a joke, ni uongo just to pay lip services

P
 
Hata msamaha huu ni msamaha batili!, kwasababu kilichosemwa ni kitu cha ukweli kabisa, kimesemwa kwa kudhamiriwa, kitendo cha kusema it was a joke, ni uongo just to pay lip services

P
Pole wahanga wote wa kauli hizi na jua hata aliyekuwa mbunge tarajiwa wa kawe alikuwa mhanga pengine wa bao la mkono ama kunyolewa kichwa na waishimiwa wajumbe.
 
Pole wahanga wote wa kauli hizi na jua hata aliyekuwa mbunge tarajiwa wa kawe alikuwa mhanga pengine wa bao la mkono ama kunyolewa kichwa na waishimiwa wajumbe.
Kwenye kura za maoni za CCM, kule hakuna bao la mkono, kule ni kila mbuzi kula urefu wa kamba yake kuwafikia wajumbe. Mimi ni Nyerere type, siku reach out kwa mjumbe hata mmoja kwa kumshika mkono!, matokeo yake, niliambulia kura moja, ya mtu aliyeshikwa mkono na wengine!.

Hili la wanasiasa kudhaminiwa na chama cha siasa, nimelipigia kelele sana humu jukwaani, nimepandisha threads zaidi ya 100!

Sikuishia kuandika tuu, pia nimezungumza mara 3 kwenye mikutano

View: https://youtu.be/PBpjDhH2XiA?si=3tg5GfB_6beRY2iv

View: https://youtu.be/3a4SjkV46JY?si=K6gaScq6TXBCbJBE

View: https://youtu.be/lBC3xKODSvY?si=cnJxysMJUVkXxhB-
Naamini kuna siku kilio hiki kitasikika!.
P.
 
Back
Top Bottom