Ndoa na Mirathi: Nafasi ya Mahakama ya Kadhi kwa Wanawake

Ndoa na Mirathi: Nafasi ya Mahakama ya Kadhi kwa Wanawake

Status
Not open for further replies.
Haya wewe tuoneshe hii mahakama isiyo ya kadhi imeleta maendeleo yepi? labda ya rushwa iliyokithiri mahakamani.

SUALA LA RUSHWA TANZANIA NI KAMA CANCER ILIYOENEA KILA PAHALA.
MI SIDHANI KAMA RUSHWA NI SUALA LA DINI FULANI BALI NI LA WATU FULANI.
SASA HIVI JAJI MKUU WA Tanzania ni Mwislam, je imabadili mwelekeo wa rushwa?
Tusijitukanishe wenyewe kwa kupambanisha tabia na dini zetu. Tujenge hoja mahususi katika kudai haki zetu.
 
Kwanza, Mtazamo wako kuwa kuna jamii ya wanaume waislamu hawawatendee haki wanawake wao ni sahihi kabisa, lakini napenda nikufahamishe kuwa hayo ni makosa yao wanaume wa kiislam na si makosa ya uislamu na mahakama ya kadhi haiwezi kunyimwa kwasababu kuna wanaume wa kiislamu wanawatesa wanawake kinyume cha mafundisho ya dini.

Pili nafikiri mahakama ya kadhi iliyo na waadilifu itasaidia kutoa hukumu kama hizo ulizosema, sidhani kama ni sawa kidini kwa mwanaume asiye na uwezo kuoa wake zaidi ya moja mfano kuwalaza wake zake kwenye chumba kimoja kama ulivyosema. sharia inaufafanuzi wa kutosha kuhusu nani anaruhusiwa kuoa, sababu za kuoa nk. imetoa mfano mzuri ni kwanini mtume alioa hizo sababu za mwanamume muislamu kuoa na si vinginevyo..

Tatu, sisi tunaotaka mahakama ya kadhi si kwa ajili ya kunyanyasa wanawake bali kwa ajili ya kufanya ibada zetu, kuona kuwa mali zetu na maisha yetu yanakuwa katika hukumu ya Allah, mahakama itasaidia kutoa ufumbuzi wa mirathi za mali zetu ..above all ni choice kwako kama unaona bado uzito kufuata hukumu hiyo unaweza kutumia sheria za nchi..

Nafikiri swala hili ni la imani hakuna kulazimishana katika imani

Angalia hizo red halafu zingatia mahojiano yetu kwenye thread ya MS na yako ya Maandamano:
1. Leo unakiri kuwa hili ni suala la IBADA ZENU. Kwa hiyo nafikiri sasa umeshaelewa kuwa lina tofauti na huduma za jamii kwa hiyo ni jambo binafsi na halihitaji ushiriki wa wasio wa ibada hizo kwa hali wala mali. (Asante)
2.Hukumu ya Allah! Ukimaanisha kuwa Allah ametoa mwongozo na naamini ndani ya Quran kitakuwepo kifungu kinachoelezea nini adhabu ya mtu asiyefuata maagizo ya Allah. Kwa hiyo hapa nachoona ni kuwa hakuna haja ya mtu kujifanya kuwa yeye ni zaidi ya Allah, kiasi atoe adhabu kwa watu kwa niaba ya Allah ilhali ukamilifu wa nafsi yake hauna uhakika.
3. Unataka kuniambia kuwa, hata baada ya kuundwa kwa mahakama ya kadhi bado litakuwa ni chaguo la mtu kupeleka mambo yake kwa kadhi au mahakama ya sheria. Sasa juzi ulisema unataka mahakama ya kadhi itambulike kikatiba na ipewe nguvu ya kisheria ya kuenforce hukumu itakazozitoa. What if marehemu alitaka mambo yake yazungumziwe kwa kadhi lkn mjane hataki, mtamwacha mjane aende LC au ndio zitatumika zile nguvu ulizokuwa unazipigia debe kumlazimisha?
4. Unasema unafikiri swala la imani hakuna kulazimishana, Then what is the concept of having a Kadhi court for?

Mimi nachokiona hapa, unam-sweettalk BR kwa kuwa kaja na hoja za msingi. Ni unafiki kuyageuka yote uliyoyasema juzi kwa kuogopa kujibu hoja na hiyo ni daili kuwa hujui unachozungumza. Mrejee aliyekutuma mwambie umeshindwa kazi.
 
SUALA LA RUSHWA TANZANIA NI KAMA CANCER ILIYOENEA KILA PAHALA.
MI SIDHANI KAMA RUSHWA NI SUALA LA DINI FULANI BALI NI LA WATU FULANI.
SASA HIVI JAJI MKUU WA Tanzania ni Mwislam, je imabadili mwelekeo wa rushwa?
Tusijitukanishe wenyewe kwa kupambanisha tabia na dini zetu. Tujenge hoja mahususi katika kudai haki zetu.

Jaji Muislaam anahukumu kwa Sharia au kwa hukumu zisizo za dini? Uozo aliokuta hapo unafikiri bila kuwa na sharia ataumaliza kwa mwaka wake mmoja au miwili aliokuwepo? maawe!
 
Jaji Muislaam anahukumu kwa Sharia au kwa hukumu zisizo za dini? Uozo aliokuta hapo unafikiri bila kuwa na sharia ataumaliza kwa mwaka wake mmoja au miwili aliokuwepo? maawe!

Kwani kabla ya Jaji Chande ( JM) unataka kusema hawakuwepo Majaji waislam? Je huko ZNZ ( kwenye Kadhi courts) unataka kusema mambo ni shwari hakuna rushwa wala uozo?
Unajua Faiza, nchi yote ina uozo wa namna moja ama nyingine.
Sharia itawezaje kumaliza matatizo? Nchi yenyewe ina imani za kila aina.Huwezi hata kuthubutu kuwazia kutumia Sharia hapa. Wananchi wenyewe wenye imani zao, hata hawazitii ndio itakuwa kutumia Sharia?Assuming kuwa Tanzania inatumia Sharia, nani atapona?Its such a mixed up society!
 
Kwani kabla ya Jaji Chande ( JM) unataka kusema hawakuwepo Majaji waislam? Je huko ZNZ ( kwenye Kadhi courts) unataka kusema mambo ni shwari hakuna rushwa wala uozo?
Unajua Faiza, nchi yote ina uozo wa namna moja ama nyingine.
Sharia itawezaje kumaliza matatizo? Nchi yenyewe ina imani za kila aina.Huwezi hata kuthubutu kuwazia kutumia Sharia hapa. Wananchi wenyewe wenye imani zao, hata hawazitii ndio itakuwa kutumia Sharia?Assuming kuwa Tanzania inatumia Sharia, nani atapona?Its such a mixed up society!

Usichanganye Muislaam na Uislaam,

Jaji hata akiwepo Muislaam kwani anahukumu kwa sharia? Ya Kenya siyajuwi kwa hiyo sina uwezo wa kuyaongelea. Mahakama zetu zinanuka uozo wa rushwa, na hiyo haihusiani na uwepo wa majaji wa Kiislaam.
 
BlackRose vs Faizafoxy mpaka sasa anayeshusha point za msingi BlackRose wewe ndio muislam safi huoshi kikombe kwa nje ,mpe vitu huyo huwa anatudanganya sana humu sisi ambao hatujui quran!
 
salute Blackie R.
Tunataka wanawake wa kiislamu wanaoongelea swala hili kwa uwazi bila ushabiki. Hatutaki sentensi kama ''wasio na dini wana mahakama yao, kwa nini sisi tulio na dini tusiwe na mahakama zetu na wote tunalipa kodi''.
This is a very very poor statement kutoka kwa mwanamke wa kiislam kama ff.
 
Hivi ikiwa unashindwa kujiondoa wewe mwenyewe kwenye umaskini unategemea nani akuondoe? Kanisa limeshakutoa kwenye umaskini?

Umaskini hauko kwenye mali au kipato chako umaskini upo ndani ya damu yako. Hata uletewe Papa hatokuondolea umaskini uliokuwa nao.

Uwepo wa kadhi ni kuhakikisha kuwa Muislaam ana haki kama yule asie na dini. Au mwenye haki nchi hii ni yule ambae hana dini?

Kodi za Waislaam na wasio Waislaam zinalipia Mahakama za wasio na dini. Jee hiyo ni haki? Ambae ana dini yake hana haki? Mnanshangaza.

Na wewe hueleweki, au wewe ni mke wa nne nini? unadai mahakama ya kadhi ili utambulike kwenye mirathi.
 
Usichanganye Muislaam na Uislaam,

Jaji hata akiwepo Muislaam kwani anahukumu kwa sharia? Ya Kenya siyajuwi kwa hiyo sina uwezo wa kuyaongelea. Mahakama zetu zinanuka uozo wa rushwa, na hiyo haihusiani na uwepo wa majaji wa Kiislaam.


Twende point by point

A) Kuchanganya MUISLAM na UISLAM - Muislam ni yule anayamini uislam iwe kamili au nusunusu.Unafikiri hao majaji utakaowapata ambao ni waislam kwa standard zako watatoka wapi kwa nchi kama Tanzania?Na kama unataka Uislam tu bila waislam, basi Tanzania mbona siyo pahala pake!

B) Umezungumzia kutumia SHARIA -
Unauliza kama Jaji muislam anahukumu kwa Sharia. Kwani tatizo wewe unadhani ni nini? kwa Tanzania bara, unafikiri hili linawezekana? Tanzania bahati mbaya ni nchi "isiyo na dini" ila watu wake wana dini zao ikiwepo Uislam.Taratibu zinazofuatwa ni za nchi na siyo za wenye dini zao.Sharia zetu ni zetu siyo za Watanzania wote.Kwa msingi huu, ni muflisi kulilia kwanini Sharia haitumiki, au kutarajia Sharia itumike.

C) Mambo ya Kenya - Nimetoa mfano wa Kenya kwa sababu:
1. Kenya na Tanzania zinachangia mengi - historia, kwa maana zote ni nchi za kiafrika, zilizoingiliwa na wageni ( wazungu na waarabu) walioleta hizi dini zinazotuchanganya na kutugonganisha vichwa hadi tunajadili haya tunayoyajadili.
2. Nchi hizi mbili zina sheria zinazofanana ( common law, religious ( Islamic and other)laws and customary laws
3. Wananchi wake hawajajiondosha kwenye mila na desturi zao kiasi ambacho hili linaleta conflict of laws. Mtu ni Muislam lakini utashangaa hajaacha mambo ya mila zake za kimakua, kinyamwezi, kingoni etc. Kama akitaka kufunga ndoa anachanganya mila na dini, maisha yake anaishi kwa mtindo unaomtambulisha zaidi na mila badala ya dini utasema huyu ni mdini au mkabila? Kumbuka mtu anaweza badili dini lakini hawezi kamwe kubadili kabila hata angetamani vipi.Kadhalika, huwezi kubadili race.Hizi ni facts.Kwa msingi huu utaona tatizo liko wapi kwenye ishu tunayojadili.
4. Waislam wa Tanzania wanapenda kurejea kinachofanyika Kenya hasa kwenye kuanzisha Kadhi courts


 
Mimi hii kitu ya watoto nje ya ndoa kutotambulika kwenye mirathi inanitia huzuni maana ndiyo inasababisha sana uduni wa maisha ya watu wengi. Lakini mwisho wa siku utasikia ni 'mfumo kristo' ndiyo unaleta ufukara ...kumbe ukweli ni kuwa ufukara unasababishwa na viidume vingi vilivyokosa maadili na kujaa zinaa.

Mkuu hapo kwenye red; kwa kweli inatia simanzi na huzuni kubwa lakini ndio dini inavyota, basi tena. Hili tatizo (la kuzaa nje ya ndoa) liko kwa watu wote, wenye dini na wasio na dini, ila Uislamu umeharamisha kuwatambua hao "WANAHARAMU". Yaani in short unawa-regard kama "mbwa koko" ilhali waliowazaa pengine wakiwa ni watu wenye "heshima" kubwa kwenye dini yenyewe.

Kimsingi, hili tatizo la kuzaa ovyo ovyo nje ya ndoa ni tatizo la kitaifa na nadhani linatakiwa kutafutiwa dawa kitaifa nje ya mipaka ya dini. Ni kwa bahati mbaya, pengine tangu Uhuru, hatujawahi kuwa na kitu kama sheria au maadili thabiti ya familia. Ni muhimu, tena liwe suala la kikatiba, kwamba familia ziweje, wajibu wa wazazi/mzazi waliozaa nje au kabla ya ndoa ni upi na akishindwa kutimiza wajibu wake nini kifanyike, haki za watoto wa nje ya ndoa ni zipi, n.k.

Kuendelea kutegemea "huruma" ya dini kwenye suala sensitive kama hili ndio linachangia kwa asilimia kubwa baadhi ya matatizo tuliyo nayo. Kuendelea kuwaachia watu wajizalie ovyo ovyo nje ya ndoa haikubaliki hata ndani ya ndoa ni lazima ieleweke sio kuzaa ali mradi umezaa. Nina jirani yangu, kipato chake kiduchu kama changu, yeye karibu kila mwaka mkewe ni mjamzito na (mkewe) ana watoto saba akiwa pungufu ya umri wa miaka 34! Japo dini yake hairuhusu kuoa zaidi ya mke mmoja, lakini bado nadhani hii haikubaliki.
 
Black Rose nimekupenda. Umeongea point ingawa wameshindwa kukujibu kwa point husika. Tunahitaji kama wewe muwe wengi kusaidia upotoshaji humu.
 
Black Rose nimekupenda. Umeongea point ingawa wameshindwa kukujibu kwa point husika. Tunahitaji kama wewe muwe wengi kusaidia upotoshaji humu.

Asante.
Nakuhakikishia tuko wengi wenye kutaka ukweli ufahamike.
 
Twende point by point

A) Kuchanganya MUISLAM na UISLAM - Muislam ni yule anayamini uislam iwe kamili au nusunusu.Unafikiri hao majaji utakaowapata ambao ni waislam kwa standard zako watatoka wapi kwa nchi kama Tanzania?Na kama unataka Uislam tu bila waislam, basi Tanzania mbona siyo pahala pake!

B) Umezungumzia kutumia SHARIA -
Unauliza kama Jaji muislam anahukumu kwa Sharia. Kwani tatizo wewe unadhani ni nini? kwa Tanzania bara, unafikiri hili linawezekana? Tanzania bahati mbaya ni nchi "isiyo na dini" ila watu wake wana dini zao ikiwepo Uislam.Taratibu zinazofuatwa ni za nchi na siyo za wenye dini zao.Sharia zetu ni zetu siyo za Watanzania wote.Kwa msingi huu, ni muflisi kulilia kwanini Sharia haitumiki, au kutarajia Sharia itumike.

C) Mambo ya Kenya - Nimetoa mfano wa Kenya kwa sababu:
1. Kenya na Tanzania zinachangia mengi - historia, kwa maana zote ni nchi za kiafrika, zilizoingiliwa na wageni ( wazungu na waarabu) walioleta hizi dini zinazotuchanganya na kutugonganisha vichwa hadi tunajadili haya tunayoyajadili.
2. Nchi hizi mbili zina sheria zinazofanana ( common law, religious ( Islamic and other)laws and customary laws
3. Wananchi wake hawajajiondosha kwenye mila na desturi zao kiasi ambacho hili linaleta conflict of laws. Mtu ni Muislam lakini utashangaa hajaacha mambo ya mila zake za kimakua, kinyamwezi, kingoni etc. Kama akitaka kufunga ndoa anachanganya mila na dini, maisha yake anaishi kwa mtindo unaomtambulisha zaidi na mila badala ya dini utasema huyu ni mdini au mkabila? Kumbuka mtu anaweza badili dini lakini hawezi kamwe kubadili kabila hata angetamani vipi.Kadhalika, huwezi kubadili race.Hizi ni facts.Kwa msingi huu utaona tatizo liko wapi kwenye ishu tunayojadili.
4. Waislam wa Tanzania wanapenda kurejea kinachofanyika Kenya hasa kwenye kuanzisha Kadhi courts



Yaani unaweza kuamini nusunusu bado ukawa muislam labda hii dini ya babu yako!
 
Yaani unaweza kuamini nusunusu bado ukawa muislam labda hii dini ya babu yako!

Usikurupuke wewe!
Umekurupushwa na mafuriko au ??
Umefuatilia mada au unakuja na "ignorance"?
Umesoma FF kasema nini kuhusu U
ISLAM NA MWISLAM? NA JINSI JAJI MWISLAM ASIVYOWEZA KUSIKILIZA KESI AKATOA HAKI KUFUATA NA MATARAJIO ya SHARIA?

Tena wewe unaweza ukawa mmoja wa hao wasikuwa na "aa" wala "bee" kuhusu nini maana ya kuwa Muislam!

Ndugu yangu, hii mada siyo yale malumbano ya kidini. Hapa ni facts na points na siyo hekaya.Huna point za nguvu kaa pembani uwaache wanaojua nini kinaendelea.
 
Usikurupuke wewe!
Umekurupushwa na mafuriko au ??
Umefuatilia mada au unakuja na "ignorance"?
Umesoma FF kasema nini kuhusu U
ISLAM NA MWISLAM? NA JINSI JAJI MWISLAM ASIVYOWEZA KUSIKILIZA KESI AKATOA HAKI KUFUATA NA MATARAJIO ya SHARIA?

Tena wewe unaweza ukawa mmoja wa hao wasikuwa na "aa" wala "bee" kuhusu nini maana ya kuwa Muislam!

Ndugu yangu, hii mada siyo yale malumbano ya kidini. Hapa ni facts na points na siyo hekaya.Huna point za nguvu kaa pembani uwaache wanaojua nini kinaendelea.

Umeishaona muislam anasifiwa na wasio waislam? Ahahahaha! Endelea na porojo zako za Kipepe!
 
Kwanza, Mtazamo wako kuwa kuna jamii ya wanaume waislamu hawawatendee haki wanawake wao ni sahihi kabisa, lakini napenda nikufahamishe kuwa hayo ni makosa yao wanaume wa kiislam na si makosa ya uislamu na mahakama ya kadhi haiwezi kunyimwa kwasababu kuna wanaume wa kiislamu wanawatesa wanawake kinyume cha mafundisho ya dini.

Pili nafikiri mahakama ya kadhi iliyo na waadilifu itasaidia kutoa hukumu kama hizo ulizosema, sidhani kama ni sawa kidini kwa mwanaume asiye na uwezo kuoa wake zaidi ya moja mfano kuwalaza wake zake kwenye chumba kimoja kama ulivyosema. sharia inaufafanuzi wa kutosha kuhusu nani anaruhusiwa kuoa, sababu za kuoa nk. imetoa mfano mzuri ni kwanini mtume alioa hizo sababu za mwanamume muislamu kuoa na si vinginevyo..

Tatu, sisi tunaotaka mahakama ya kadhi si kwa ajili ya kunyanyasa wanawake bali kwa ajili ya kufanya ibada zetu, kuona kuwa mali zetu na maisha yetu yanakuwa katika hukumu ya Allah, mahakama itasaidia kutoa ufumbuzi wa mirathi za mali zetu ..above all ni choice kwako kama unaona bado uzito kufuata hukumu hiyo unaweza kutumia sheria za nchi..

Nafikiri swala hili ni la imani hakuna kulazimishana katika imani

Du! Mtoto wako, kwenye mali unambagua kisa dini? kuna haja ya kufiKilia mara mbili.
 
Umeishaona muislam anasifiwa na wasio waislam? Ahahahaha! Endelea na porojo zako za Kipepe!


Kwa mtizamo na ujinga wako ndio tutaendelea kudharauliwa tu.
Amka wewe!! Inferiority complex is not my nature and it will never be.


Bahati mbaya sana waislam waelewa na wasomi mara nyingi wanakaa kimya hawasemi wanaachia wajinga kama wewe wakurupuke na kutufanya siye wote tuonekana mazuzu.
Muda umefika to put a stop to this nonsense! itafika siku watu kama wewe tutawazuia kufungua midomo yenu msiendelee kutuaibisha.

Mod mmoja humu JF ana signature inasema hivi:

FICHA UPUMBAVU WAKO, USIIFICHE HEKIMA YAKO!
 
Faiza Foxy said:
Watoto nje ya ndoa wakiwemo kwenye mirathi wataleta matatizo zaidi. Kumbuka Uislaam unasisitiza ndoa na hausisitizi zinaa na kama mtu aliteleza na kuzaa nje ya ndoa basi ampe mali (kama anayo) huyo mtoto nje ya ndoa na kabla hajafa na si kuleta rabsha baada ya kufa.

Faiza Foxy,

..ushauri wangu ni kwamba, ikibainika kwamba marehemu Muislamu alikuwa na watoto wa nje ya ndoa, basi mirathi yake ishughulikiwe na mahakama ya ki-secular.

..kwa mtizamo wangu kitendo cha kuzaa nje ya ndoa kinapaswa kumpokonya Muislamu haki ya mirathi yake kushughulikiwa kwa kuzingatia taratibu za Kiislamu.

..labda weledi wa masuala haya mtueleze kama kuna utaratibu wowote ule ktk Uislamu unaohakikisha kwamba watoto walozaliwa nje ya ndoa wanarithi mali za wazazi wao.


 
Umeishaona muislam anasifiwa na wasio waislam? Ahahahaha! Endelea na porojo zako za Kipepe!

kwa hiyo siruhusiwi kumsifia mwislam kwa kuwa mimi sio muislam??!!! Hata kama anaongea vitu sensible??!!!

Hii ni problem hii!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom