RIGHT MARKER
Senior Member
- Apr 30, 2018
- 129
- 473
Mhadhara - 34:
Tukizungumzia msiba ni tukio la ghafla - msiba hutokea ghafla. Kwa watu ambao wana maisha ya kawaida matukio ya misiba yanawakuta wafiwa kwenye hali mbaya ya kiuchumi. Hivyo ni muhimu kumchangia hela mfiwa za kumsaidia.
Kuhusu ndoa/harusi:
Siku hizi matukio ya harusi yamekuwa ni madeni kama madeni mengine yanayohitaji marejesho. Ndoa/harusi si tukio la ghafla ni tukio la kupangwa. Muowaji, muolewaji na waozeshaji ndio wanapanga hilo tukio kwa matakwa yao. Kwa mtazamo wangu ndoa/harusi ni tukio la hiari.
MASWALI MATANO:
1. Je, unapangaje tukio la hiari bila kuwa na hela?
2. Je, unapangaje tukio la hiari kwa kutegemea pesa za ndugu, jamaa, marafiki na majirani?
3. Je, ni lazima kufanya tukio la hiari ambalo litahitaji pesa nyingi kuliko uwezo wako?
4. Je, mtu ambaye anahitaji kufunga ndoa ya gharama kuliko uwezo wake, ana utofauti gani na mtu ambaye atahitaji msaada wa kuchangiwa pesa ya kwenda kutalii (kula bata) nje ya nchi?
5. Je, kanisani na msikitini hawafungishi ndoa ambayo haitokuwa na sherehe yoyote?
Kama unaamua kuoa, kuolewa au kuozesha mtoto wako kwanini usiwekeze hela zako kisha uoe/uolewe bila kuwasumbua watu wengine wakuchangie hela. Nadhani hii pia itasaidia vijana kutokuvunja ndoa zao kiholela (bila sababu za msingi) hasa wakikumbuka machungu pesa zao.
Watu wanahangaika kuchanga pesa, wengine wanakopa hela wananunua magodoro, mabeseni, vitanda, makosheni, TV, makabati na makolokocho kibao wanakwenda kuwatunza wanandoa ukumbini, baada ya miezi mitatu mbele wanaambiwa ndoa imevunjika kwasababu mke alichelewa kurudi nyumbani.
Wapo watanzania ambao kwa mwezi anaweza kuwa hata na kadi 4 za michango ya harusi na kila kadi anatakiwa kuchangia si chini ya Tsh 100,000, bado kushonesha sare. Mtu huyu ukikutana nae barabarani amevurugwa unaweza kudhani ana madeni ya benki au Vicoba.
Tukizungumzia msiba ni tukio la ghafla - msiba hutokea ghafla. Kwa watu ambao wana maisha ya kawaida matukio ya misiba yanawakuta wafiwa kwenye hali mbaya ya kiuchumi. Hivyo ni muhimu kumchangia hela mfiwa za kumsaidia.
Kuhusu ndoa/harusi:
Siku hizi matukio ya harusi yamekuwa ni madeni kama madeni mengine yanayohitaji marejesho. Ndoa/harusi si tukio la ghafla ni tukio la kupangwa. Muowaji, muolewaji na waozeshaji ndio wanapanga hilo tukio kwa matakwa yao. Kwa mtazamo wangu ndoa/harusi ni tukio la hiari.
MASWALI MATANO:
1. Je, unapangaje tukio la hiari bila kuwa na hela?
2. Je, unapangaje tukio la hiari kwa kutegemea pesa za ndugu, jamaa, marafiki na majirani?
3. Je, ni lazima kufanya tukio la hiari ambalo litahitaji pesa nyingi kuliko uwezo wako?
4. Je, mtu ambaye anahitaji kufunga ndoa ya gharama kuliko uwezo wake, ana utofauti gani na mtu ambaye atahitaji msaada wa kuchangiwa pesa ya kwenda kutalii (kula bata) nje ya nchi?
5. Je, kanisani na msikitini hawafungishi ndoa ambayo haitokuwa na sherehe yoyote?
Kama unaamua kuoa, kuolewa au kuozesha mtoto wako kwanini usiwekeze hela zako kisha uoe/uolewe bila kuwasumbua watu wengine wakuchangie hela. Nadhani hii pia itasaidia vijana kutokuvunja ndoa zao kiholela (bila sababu za msingi) hasa wakikumbuka machungu pesa zao.
Watu wanahangaika kuchanga pesa, wengine wanakopa hela wananunua magodoro, mabeseni, vitanda, makosheni, TV, makabati na makolokocho kibao wanakwenda kuwatunza wanandoa ukumbini, baada ya miezi mitatu mbele wanaambiwa ndoa imevunjika kwasababu mke alichelewa kurudi nyumbani.
Wapo watanzania ambao kwa mwezi anaweza kuwa hata na kadi 4 za michango ya harusi na kila kadi anatakiwa kuchangia si chini ya Tsh 100,000, bado kushonesha sare. Mtu huyu ukikutana nae barabarani amevurugwa unaweza kudhani ana madeni ya benki au Vicoba.
Right Marker
Dar es salaam.