Ndoa za kikristo ni kituko, wakristo wengi wanakimbilia sheria za mahakamani ndoa zinaposumbua hawataki kufuata sheria zao za kikristo

Kanisa linatumia vyeti vya ndoa vya serikali, hakuna ndoa yoyote mpaka kifo, ndoa ikishindikana inavunjwa mahakamani, kama hujui jambo ni bora uombe kuelimishwa kuliko kulazimisha maoni yako ndio yawe fact.
Hata mahakama ikivunja ndoa kanisa katoliki halitambui na Wala hutaweza kuoa au kuolewa kanisa kisa ulipewa talaka au ndoa imevunjwa mahakamani. Kanisa halitambui talaka.

Kanisa katoliki Lina mahakama zake zinaitwa tribune zinashughulika na case hizo, Kuna process za ku nullified marriage, ila hatuiti talaka, na mchakato wake ni mrefu na lazima kuwe na sababu za msingi sana.
 
Founder wa Wasabato si ndio huyu mwanamke Hellen G White?

Agano jipya ndio injili ya Yesu Kristo Sasa kama hutumii agano jipya huo Ukristo wako unatoka wapi?

Wasabato ni dini inayojitegemea na siyo Wakristu.
Sio kweli mkuu wasabato ni wakristo kwa sababu wamemkiri yesu kuwa bwana na mwokozi wa maisha yao. Rejea usemi wa "Maranatha" na jibu likiwa "Yesu anakuja". Pia rejea Yesu mwenyewe akisema yeye ndiye bwana wa sabato. Usabato umejengwa katika misingi mikuu ya kristo kuliko hata unavofikiria wewe. Kwa mfano hata pasaka ya kisabato iko katika misingi ambayo Yesu alifanya na wanafunzi wake nikimaanisha kuoshana miguu kama kiwakilishi cha ushirika mmoja katika bwana lakini pia mkate na divai kama tunavojua. Pia wasabato wanasali sala ile alioacha Yesu ya roho mtakatifu tunayoijua. Jpo tofauti ni moja tu ( Sikuja kulitangua torati bali kulitimiliza ni msingi mkuu wa ushirika wa wasabato kwa Yesu kristo na pia msingi wa imani umeundwa kwa mitume na manabii maneno ya Yesu mwenyew)
Asante.

Sent from my SM-G955U using JamiiForums mobile app
 
Founder wa Wasabato si ndio huyu mwanamke Hellen G White?

Agano jipya ndio injili ya Yesu Kristo Sasa kama hutumii agano jipya huo Ukristo wako unatoka wapi?

Wasabato ni dini inayojitegemea na siyo Wakristu.
Pia Ellen G White sio founder maan founder ni Mungu mwenyew. Ila huyo mama ni mhimili moja wapo katika modernized world na ndo maan yeye alipewa maoni ya kutafsiri bible kama ilivokuwa kwa martin luther wa kilutheri

Sent from my SM-G955U using JamiiForums mobile app
 
We jamaa ni msabato gani ambae unasema wasabato hawasomi agano jipya?

Sent from my SM-G955U using JamiiForums mobile app
 
Wewe kama ni mkatoliki ni zao la misale ya waumini.

Uhuni unaofanywa na kanisa katoliki ni kuwafunga kitambaa cheusi machoni waumini wake wasijuwe lolote wamsikilize paroko tu.

Kanisa katoliki lina sheria zake zinaitwa Canon law, wasomi wa canon kama Dr Slaa ndio maana hawakubanwa na ujinga huu walipotaka kuacha nadhiri ya upadre na kuoa.

Nakupa mfano Mdogo tu hapa chini, mtu kama huyu Freddy Maston hata kama alioa kanisani kwa hali hii kanisa katoliki linavunja hiyo ndoa mchana kweupe na mwanamke anaruhusiwa kuolewa Tena kanisani.
 

Attachments

  • Screenshot_20220901-132519_1.jpg
    55.9 KB · Views: 4
  • Screenshot_20220901-132539_1.jpg
    60.1 KB · Views: 3
  • Screenshot_20220901-132349_1.jpg
    45.2 KB · Views: 3
  • Screenshot_20220901-132339_1.jpg
    59.6 KB · Views: 3
Ndoa nyingi za siku hizi zinageuka kuwa ndoano! Ee Mola tunakuomba ukinusuru kizazi hiki cha .com.
KWANINI ZIMEKUWA NDOANO?
KWANINI HAZIDUMU?

Ukisoma maandiko ktk Biblia utaona kuwa ndoa zilifungwa katika jamii hiyohiyo.
Mfano Yakobo alienda oa kwa mjombae.

Angano la kale Mungu aliwaangiza waisrael wasiwatoe binti zao kuolewa na makabila nje ya Israel au vijana wao kuoa nje ya Israel.
PALIKUWA NA MAANA NYINGI KUBWA.

Kuanzia karne ya 19, mngoni alioa mngoni kadharika makabila mengine.
Kuoa kulihusisha sana wazazi,ambao walitafuta mchumba ndani ya jamii yao.

Ilikuwa hata uhawala, ngumu sana kulala na binti wa kabila lingine.
Kila kabila ina tamaduni zake hivyo wanandoa waliendana na tamaduni moja.
Mfano mzuri Masai,huwezi sikia ameoa kabila lingine,zaidi sana Masai ataoa mwanamke wa kigogo,ambae kidogo wanafanan tamaduni.

UTANDAWAZI,

Zamani mwanamke akiwa mfanyakazi, Mme akimwambia aache kazi anafanya ivo. Mwanaume hata akiwa hana pesa heshima ilikuwepo.

MUNGU ALIPOWALAANI ADAM NA EVA PALE EDEN,ALIMWAMBIA EVA, TAMAA YAKE ITAKUWA JUU YA MMEWE.

Wanawake wa sasa hawana heshima,wamesoma,wanakazi na mishahara,wanabiashara. Wanakidhi mahitaji yao, atakachohitaji kwako ni utamu tu na ukimzingua anaenda nje.

Kijana wasasa mwanamke anampatia chuo,kwenye mabasi,kwenya mziki nk.
POLENI SANA NDOA YA KIKRISTO NI MADHUBUTI SANA YANAYOTOKEA NI UKENGEUFU TU
 
naona umeshindwa kujenga hoja umeenda kwenye personal attack. kwanza paroko hawezi kufundisha mambo ya canon law kwa waumini. pili kama unaelewa lolote kuhusu sheria, iko hivi sheria za nchi haziwezi kutengua SHERIA ZA KANISA ( CANON LAW) tafuta wanasheria wakueleweshe vizuri. Mahakama ikitowa talaka kwa ndoa iliyofunga ndani ya kanisa katoliki hukumu hiyo haifanyi kazi ndani ya kanisa na kanisa haliwezi kuruhusu mtu aliyepewa talaka mahakamani kuja kufunga ndoa kanisa hilo halitambuliki ndani ya kanisa. kanisa katoliki ni taasisi sio kanisa tu kw uelewa wa makanisa mengine.

papa francis ni kiongozi wa kanisa na kiongozi wa state at the same time. ndio maana papa anapoenda nchi yoyote hupokelewa na kiongozi wa nchi ile. nimeshakueleza huko nyuma kanisa lina mahakama zake zinazoshughulika na kubatalisha ndoa na kuna process zake na kuna vigezo vyake.
 
Hizi ndo Sheria nzuri zinataka watu wawe makini katika uchaguzi
 
Ukiona ndoa inavunjika basi aliyekuwa na dhamira ya Ndoa kutoka moyoni ni m'moja tu mwingine alikuwa anamchota mwenzake akili au pengine ni wote wawili hawakuwa na dhamira ya Ndoa walikuja na matarajio binafsi ambayo yanapatikana ndani ya Ndoa.

Kuna watu wanaingia katika mahusiano kutafuta mitaji ya biashara, kutafuta watoto tu, ngono kama ngono, kuprove kwenye jamii kuwa wanaweza kuolewa na kuwa na ndoa, wamekosa pa kwenda so ndoa inawapa hifadhi sehemu ya kuishi.

So kimsingi ukiona Watu wanakorofishana then jua m'moja wapo au wote waliingia kimasilahi na wameshapata.
 
Ndoa zote zinavunjwa mahakamani kwa sheria za bara. Zanzibar sijajua maana wao sijui wana kadhi. Bakwata hawana mamlaka ya kuvunja ndoa, kazi yao ni kusuluhisha. Ikishindikana wanawapa barua kwenda mahakalani
Kosa Kubwa sana walilofanya Waislam baada ya Uhuru kukubali kutumia Sheria za Kizungu kwenye ndoa za Kiislam na Kiafrika Kwa Ujumla. Wazungu walileta Sheria za Mila uzao na kuziingiza kwenye Ukristo. Mapadri na Wazungu walizikubali Sheria za Kizungu Kwa SABABU Walijua kuwa hazina madhara Kwa wakubwa hasa Wakoloni. Mkoloni alijua kuwa Mwafrika hawezi kamwe Kupata fursa ya kuzini na MKE Wa Governor au Bosi Wa Kizungu Lakini Wazungu Walikua wanawachezea wanawake Wa Kiafrika kama wanavyotaka na waume zao hawakuwa na fursa ya kushitaki kama jinai Bali waliambiwa wafungue Kesi ya madai.

Sheria hiyo ya Kizungu kwenye masuala ya Ndoa Kwa Karine Hii ya utandawazi ni mbovu mana watu wanapata taarifa za kuchepuko Kwa haraka sana Jambo linalosababisha mauaji MENGI mana Suala la fumanizi linapandisha wazimu na kusababisha MTU kuua.

Waislam pamoja na Sheria Yao nzuri ya kulinda Heshima ya Ndoa na kuwapa wanawake fursa ya kuolewa na kuachana Kwa wema wamejikuta wakiingia kweye Mila za Kizungu zisizoenda kabisa na Mila na Sheria za kiislam.
 

1. Hakuna sheria ya Kikristo.
2. Sheria ni ya serikali na haina dini.
3. Asiyefuata imani ya kikristo, Sio mkristo hata kama ana jina ka kikristo!
 
Hahahaha majuzi tu hapa rafiki yangu mmoja ndoa imevinjika na kwenye harusi yake nilimchangia pesa ndefu sana
 
Wakibadilo hiko kipengele Cha kutoachsna hadi kifo Kila jumamosi matarumbeta yatakuwa mengi kitaani.
 
Kwanza tuonyeshe hiyo sheria imeandikwa wapi, uifafanue. Si vema kuleta ubunifu wako na kuuita sheria ya Kikristo. Haya tuonyeshe hiyo sheria
 
Hizo sheria zinapatikana kwenye kitabu kipi? Nimesoma Biblia yoote sijakutana na sheria za ndoa. Hebu nionyeshe ulikozipata
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…