Mkuu Mbu mimi kwa maoni yangu mporomoko wa NDOA ZA KISASA unachangiwa na haya yafuatayo:
ELIMU:
Wanawake wa siku hizi wengi wamesoma sana ukilinganisha na wale wa miaka ile ambao asilimia kubwa walikuwa wameishia madarasa ya chini sana au hawakusoma kabisa. Elimu hii waliyoipata hawa wanawake katika ndoa za kisasa imewasaidia kwanza kujua haki zao ndani ya ndoa na pia kujua nini watakacho ndani ya ndoa. Si rahisi hawa kuwaburuza kama gari bovu kama walivyokuwa wanafanyiwa Wanawake katika ndoa za enzi zile ambao walikuwa wanayavumilia mengi sana ndani ya ndoa ili mradi watunze ndoa zao. Hawa wa kisasa wana kisomo cha hali ya juu, kazi nzuri na kipato kikubwa ambacho kinawawezesha kabisa kuishi wenyewe bila matatizo na hivyo kutohitaji kumtegemea mume katika mahitaji yao muhimu ikiwemo makazi, chakula n.k. Kwa maoni yangu si kweli hawa wana dharau au kiburi kama ambavyo Wanaume wengi tunavyodhani bali tu wanahitaji kuheshimiwa kama wake, kuonyeshwa mapenzi ya kweli, na kuthaminiwa kwa mchango wao ndani ya ndoa. Kunapotokea tatizo katika ndoa ambazo Wanawake wake ni wasomi mara nyingi hitimisho la Wanaume ni kwamba huyu ana kiburi kwa sababu kasoma, kwa sababu ana kazi nzuri na mshahara mzuri vitu ambavyo mara nyingi havina ukweli wowote. Unaweza kukuta tatizo dogo sana likawa kubwa kupita kiasi kwa dhana potofu kabisa na hata kuvunja ndoa.
Kuwashirikisha watu wa nje katika matatizo ya ndani ya ndoa:
Hapa ninamaanisha marafiki, mashoga, colleagues n.k. Zamani matatizo ya ndani ya ndoa yalikuwa yanajulikana kwa wanafamilia tena wale wa karibu sana. Hawa tatizo lilipotokea na wao kufahamishwa walijitahidi kwa hali na mali ili kuyamaliza matatizo katika ndoa husika na wakati mwingine hata majirani wasijue kwamba Mr & Mrs A walikuwa na matatizo makubwa katika ndoa yao. Siku hizi si hivyo kabisa mume/mke akiwa na matatizo basi watu wote anaowafahamu wakiwemo marafiki, majirani, colleagues, wasusi/vinyozi kule saloon atawaelezea matatizo katika ndoa yake. Hawa wengi wao huwa haiwatakii mema ndoa husika. Na wengine si ajabu wataweka matatizo hayo mtandaoni (hapa JF tumeshaona mifano chungu nzima siku za nyuma). Haya matatizo kujulikana na watu wengi kiasi hicho tena wengine wanasubiri kwa hamu kuona ndoa inasambaratika hayasaidii kwa kweli katika kudumisha ndoa. Wengine walioombwa ushauri wa nini mume/mke afanye kufuatia tatizo lilitokea ndani ya ndoa mfano mke/mume kutembea nje bila hata ya kufikiria athari kubwa sana labda kwa watoto katika ndoa ile hutoa ushauri, "Achana naye, wanawake/wanaume wa maana wako chungu nzima siku hizi." badala ya kujaribu kuwasaidia wana ndoa wale wamalize matatizo yao bila kuisambatarisha ndoa yao.
Utandawazi:
Miaka ya nyuma ilikuwa humtongozi mwanamke mpaka umemuona akakuvutia labda kwa sura yake, tabasamu lake, miguu yake, miondoko yake (kama Naomi Campbell au Tyra Banks 🙂🙂) wowowo lake n.k. Sasa hili lilihitaji muda kwa kweli ili uweze kumfuatilia binti huyo mpaka uweze kukubaliwa kama mpenzi, lakini siku hizi ni tofauti kabisa. Unaweza ukamtongoza binti yeye yuko bara tofauti na ulilopo wewe kupitia mtandao na huku hujawahi hata kumtia machoni. Na ikitokea akakubali basi mnaweza kujenga penzi la nguvu sana tena la kweli kabisa.
Pia mtandao na hata TV zimechangia kuwafanya wanandoa wasiwe karibu karibu kama ilivyokuwa miaka ya nyuma. Miaka hii utakuta nyumba nyingi zina TV mbili mbili mama anaangalia vipindi vyake na baba anaangalia vipindi vyake kila mmoja hapendi vipindi vya mwenzake. Pia utakuta kila mtu ana laptop yake mume yuko JF kwenye siasa na mke yuko MMU 🙂🙂 hawa hawapati muda kabisa wa kukaa kama mume na mke na kama wote ni waajiriwa basi hali ndio inazidi kuwa mbaya sana katika ndoa yao hata linapotokea tatizo dogo sana basi kwao huwa ni kubwa sana kwa sababu kwanza hawajuani kila mtu yupo kivyake vyake tu (MBL Married but lonely, MBA Married but available & MBU Married but unsatisfied) hahahahaha lol! watu kama hawa pamoja na kuwa wamo kwenye ndoa lakini hawajuani kabisa hivyo ni rahisi mno kufikia maamuzi ya kuachana kwa sababu hawana uchungu wowote na ile ndoa yao maana wanaishi kama strangers tu wanalala kitanda kimoja lakini ukiondoa kulala pamoja kila mtu yuko kivyakevyake. Tatizo dogo tu ndani ya ndoa basi mume/mke hata kabla ya kukaa chini kuongea na mwenzie kishakimbilia kwa marafiki kuelezea kilichotokea au kishaandika MMU 🙂🙂 kuomba ushauri bila hata ya ndugu wa karibu kwa wanandoa hao kutaarifiwa chochote kile kuhusiana na tatizo husika.
Nadhani kwa maoni yangu mambo haya yanachangia sana katika mporomoko mkubwa uliopo katika ndoa za kisasa ukilinganisha na zile za enzi zile na sidhani kama kuna uwezekano wa kurekebisha hali hii.