NDOA: Zamani vs Siku hizi

NDOA: Zamani vs Siku hizi


....kwahiyo tunakubaliana ili ndoa zidumu inabidi kurudisha na kuzisimamia mila, desturi na tamaduni zetu za asili
(mwj1 jana alinikumbusha jando baada ya mie kusisitizia unyago) ....tuwakataze mabinti zetu haya ma kitchen party ya khanga moja sijui laki si pesa....,

...vile vile tuvikumbatie vifuani mwetu vitabu vyenye miongozo ya kiimani badala ya waraka wa Beijing ambao haujatafsirika vyema kwenye jamii yetu, ama?
 
Kuna wanawake wengine hata ufanyaje yeye ni mtu wa kukulaumu tu kana utimizi majukumu yako nyumbani, na anataka wewe ufanane na nyani ngabu kisa nyani ngabu ni mbeba mabox maarufu basi anataka na wewe uwe na ujiko huo!

Awali ya yote, majina yangu yanaandikwa kwa kutumia herufi kubwa kwa herufi ya kwanza - kama hivi Nyani Ngabu.

Na mimi si mbeba mabox maarufu. Mimi ni Raisi wa Wabeba Mabox. Usisahau hiyo, ni Raisi. Okay my friend?
 
Kuna wanaoowa na bado wanakaa kwa Baba na mama, je huyu atakuwa ni mke wako au ni mke wa familia?
Na kuna walioolewa lakini kila baada ya siku mbili kiguu na njia kwa mama yake, je huyu anaweza akawa wife material?
Na kuna wazazi wanaotaka watoto waishi maisha yao wao wazazi, je inawezekana mtu kuishi maisha ya mtu mwingine?
Na kuna mawifi wao ndio wamejipa jukumu la kuverify kwamba mkeo anafaa au hafai, unadhani hapa bila mume kuwa strong kuna ndoa imara?
Kuna wanawake wengine hata ufanyaje yeye ni mtu wa kukulaumu tu kana utimizi majukumu yako nyumbani, na anataka wewe ufanane na nyani ngabu kisa nyani ngabu ni mbeba mabox maarufu basi anataka na wewe uwe na ujiko huo!

Kuna wanawake ukiwa unatumia kilevi kidogo basi ndio nongwa, ni lawama zisizoisha kana kwamba pesa yako yote unapigia mtungi, anataka umiliki kigari huku akisahau hata yeye anapaswa kununuwa gari maana wapo wanawake wenzake wanamiliki mpaka Ferari bila kuhongwa na mwanaume!
How can you build broken relationship when feeling is no longer there?

Matola ongezea wale ambao kaugomvi kadogo ukoo na mashoga zake wote watajua.

Mapungufu ya mume/mkewe kila mtu anayafahamu.

Tatizo ni kwamba watu hawaoani kwaajili yao bali wanaoana kwaajili ya familia na jamii.Hivyo inakua ngumu kujitoa mazima. Matokeo yote vijitatizo vyote vidogo vidogo lazima vifike kwa mama na baba, maamuzi yote amabyo yanatakiwa yawe kati ya mune na mke lazima yapitie kwa wazazi ama waangalie jamii inaoneje. Hao wanaojali jamii ndo hao wanaotaka ferrari ili wasifike mjini wakati bado wanaishi kwenye nyumba ya kupanga.
 
Awali ya yote, majina yangu yanaandikwa kwa kutumia herufi kubwa kwa herufi ya kwanza - kama hivi Nyani Ngabu.

Na mimi si mbeba mabox maarufu. Mimi ni Raisi wa Wabeba Mabox. Usisahau hiyo, ni Raisi. Okay my friend?
Okey, Nyani Ngabu Rais wa Wabeba Mabox, i hope waziri Mkuu atakuwa MM Mwanakijiji
 
Mbu kuna mtu anapigwa kwa kuwa kachelewa kuipokea simu yake hata kama sababu ilikuwa ni kumuattend mtoto!!!

...lol....sasa haya ndiyo aliyoyasema AshaDii, mambo ya utandawazi nayo yanaathari kubwa kwenye ndoa za kisasa, ...mobile phones, emails, facebook, sms nk nk....yaani imekuwa ni kasheshe juu ya kasheshe lakini ipo njia kuyakabili haya iwapo mwenzako hapendi, au?

...kuna haja gani kumuonyesha mumeo umefanikiwa kuwa add ex boyfriends wako wote kwenye facebook? au sms zisizotulia usiku kucha ...muda ambao ulitakiwa kuwa na mumeo kwenye udugu wa shuka? haya ndio ninayoyasema kama kwenye issue ya makaburini huyo anayejitia 'samaritan' na kuja kumsuta mwanaume mwenziwe jamiiforums...unaona sasa?


Mbu unaongelea kupiga/pigana physically?
Hiyo wapo wanaopiga wake zao kisa tu chumvi imezidi ama imepelea kidogo kwenye mboga. Kuna watu hua hawafikirii, mkono unainuka tu.

Ila mimi nilikua naongelea ile ya mtu kumtenda mwenzake hovyo (kucheat, kumtukana, kutomjali, kumdharau na hata kumpiga kama hapo juu) kisa tu anajua anapendwa.

...hiyo sasa nayo hila weye, iweje umjazie chumvi mumeo bana? utamuua....!
au ati umeacha kumtilia chumvi kwenye mboga, lazima uchapwe kidogo, kofi lisiloumiza....lol
 

...lol....sasa haya ndiyo aliyoyasema AshaDii, mambo ya utandawazi nayo yanaathari kubwa kwenye ndoa za kisasa, ...mobile phones, emails, facebook, sms nk nk....yaani imekuwa ni kasheshe juu ya kasheshe lakini ipo njia kuyakabili haya iwapo mwenzako hapendi, au?

...kuna haja gani kumuonyesha mumeo umefanikiwa kuwa add ex boyfriends wako wote kwenye facebook? au sms zisizotulia usiku kucha ...muda ambao ulitakiwa kuwa na mumeo kwenye udugu wa shuka? haya ndio ninayoyasema kama kwenye issue ya makaburini huyo anayejitia 'samaritan' na kuja kumsuta mwanaume mwenziwe jamiiforums...unaona sasa?




...hiyo sasa nayo hila weye, iweje umjazie chumvi mumeo bana? utamuua....!
au ati umeacha kumtilia chumvi kwenye mboga, lazima uchapwe kidogo, kofi lisiloumiza....lol

Kwanza Mbu tusilaumu teknolojia pekee, kama asingepigwa kwa kuchelewa kupokea simu angepigwa kwa kuchelewa kufungua mlango au kuleta maji ya kunywa.Mtu mwenye visa haihitaji sababu, yeye chochote kwake anaona kinastahili kichapo.

Hahahahaha, sasa jamani bahati mbaya siinatokea wakati mwingine?Ukizingatia na jinsi wamama wengine wanavyokua na mambo mengi ya kufanya, wala mimi sioni ajabu. Ila angalau wewe umesema shurti achapwe kofi lisilouma, wenzako wanapiga mpaka kesho yake mama akiinua kujiko aweke sukari kwenye chai mkono unatetemeka.
 
Hii mada imenivutia na nimesoma michango ya wote. Wote kwa njia moja au nyengine tunakubaliana kuwa mmomonyoko wa maadili, kutofuata mila na desturi zetu, kung'ang'ania haki na kusahau/kuepuka wajibu...pamoja na sababu nyingi tu, zinazofanya ndoa za kisasa kutodumu (kwa muda mrefu).

Kama angalizo tu, ningependa kwanza kukumbushia kuwa hata zamani zilikuwepo ndoa zilizoshindikana (jamaa yangu wa karibu aliwahi kuolewa mara 16, mara 3 aliolewa na mume huyo huyo). Pia wapo wanaume waliooa mara zisizo hesabu. Tafauti ya zamani sasa, ni kuwa zamani kesi za kuvunjika kwa ndoa zilikuwa zinahesabika, wakati sasa ndoa zinazodumu ndio zinazohesabika.

Kwa kuongezea kidogo katika mengi yaliyokwishasemwa, nitagusia nukta mbili:

1.- Kujuana saaana kabla ya ndoa" kunachangia. Hii inatafautiana na wazazi wetu waliokuwa wanaoa/wanaolewa/wanaoana hata bila ya kujuana. Nimeweka kwenye vifungo "kujuana sana" kwa sababu hivyo ndivyo tunavyojidai, eti kwa sababu tu wamelala kitanda kimoja miaka mingi kabla ya kuoana. Katika kipindiki hiki cha kubanjuana, kila mmoja huwa anaficha makucha yake na baada ya ndoa yanafichuka yale yote yaliyokuwa yamefichika.

2.- Wakati zamani kuacha/kuachika kulikuwa aibu na mjane alikuwa anaonekana vibaya katika jamii, leo mtu kujidai ni mjane imekuwa fesheni. Tumekutana na wangapi wanawake kwa wanaaume ambao wamo katika ndoa lakini wakitoka tu nje ya nyumba zao wanavua pete na/au kujitangaza ni wajane? Tumefikia mahali kujitaja kuwa umeoa/umeolewa tunaogopa kuoneka wa "zamani". Nina wasiwasi watu wa aina hiyo hata humu JF wamo. Na kama anecdote tu, nimeona majuu watu wanaandaa sherehe za kuacha/ kuwachwa. Sijui lini na hili nalo litafika kwetu, ikiwa bado halipo.

Kwa kuchangia tu mawazo kuhusu nini tufanye ili ndoa za vizazi vijavyo zidumu, nahisi njia pekee ni sisi tulioko ndani ya ndoa sasa kuzidumisha ndoa zetu na kuwa mfano mwema kwa vizazi vyetu, vyenginevyo hata tukaweka mitaala na silibasi mashuleni, ikiwa tunawafunza kile ambacho sisi tulishindwa kukitekeleza, wao hawataweza.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
images
....wakati nikijiandaa kuwasha mishumaa kusubiria mwaka 2012, hebu tutafakari na kujadiliana hili. Wazee wetu walidumu kwenye viapo vya ndoa zao kwa kuzingatia misingi ya mila na tamaduni zao, imani za kidini na mitazamo ya kijamii tofauti na kasi ya kuvunjika kwa ndoa kwa miaka hii ya sasa. Nini mtazamo wako kuhusiana na janga hili la kitaifa na kimataifa...

mfano; haijalishi mmeoana kijijini, mnapokuja mjini na mke anapoacha msingi wa ndoa aliyokuzwa nayo, ndoa itayumba, ...na hili pia lishawakumba hata wale waliokwenda ng'ambo na wake zao..." kipofu kaona mwezi, au alalaye usimwamshe?"....



Je, mporomoko wa NDOA ZA KISASA unachangiwa na wanawake kujua haki zao dhidi ya mifumo dume iliyotawala tangu enzi za mababu, na misingi ya imani za kidini, au?

Jadili

Mkuu Mbu mimi kwa maoni yangu mporomoko wa NDOA ZA KISASA unachangiwa na haya yafuatayo:

ELIMU:

Wanawake wa siku hizi wengi wamesoma sana ukilinganisha na wale wa miaka ile ambao asilimia kubwa walikuwa wameishia madarasa ya chini sana au hawakusoma kabisa. Elimu hii waliyoipata hawa wanawake katika ndoa za kisasa imewasaidia kwanza kujua haki zao ndani ya ndoa na pia kujua nini watakacho ndani ya ndoa. Si rahisi hawa kuwaburuza kama gari bovu kama walivyokuwa wanafanyiwa Wanawake katika ndoa za enzi zile ambao walikuwa wanayavumilia mengi sana ndani ya ndoa ili mradi watunze ndoa zao. Hawa wa kisasa wana kisomo cha hali ya juu, kazi nzuri na kipato kikubwa ambacho kinawawezesha kabisa kuishi wenyewe bila matatizo na hivyo kutohitaji kumtegemea mume katika mahitaji yao muhimu ikiwemo makazi, chakula n.k. Kwa maoni yangu si kweli hawa wana dharau au kiburi kama ambavyo Wanaume wengi tunavyodhani bali tu wanahitaji kuheshimiwa kama wake, kuonyeshwa mapenzi ya kweli, na kuthaminiwa kwa mchango wao ndani ya ndoa. Kunapotokea tatizo katika ndoa ambazo Wanawake wake ni wasomi mara nyingi hitimisho la Wanaume ni kwamba huyu ana kiburi kwa sababu kasoma, kwa sababu ana kazi nzuri na mshahara mzuri vitu ambavyo mara nyingi havina ukweli wowote. Unaweza kukuta tatizo dogo sana likawa kubwa kupita kiasi kwa dhana potofu kabisa na hata kuvunja ndoa.

Kuwashirikisha watu wa nje katika matatizo ya ndani ya ndoa:

Hapa ninamaanisha marafiki, mashoga, colleagues n.k. Zamani matatizo ya ndani ya ndoa yalikuwa yanajulikana kwa wanafamilia tena wale wa karibu sana. Hawa tatizo lilipotokea na wao kufahamishwa walijitahidi kwa hali na mali ili kuyamaliza matatizo katika ndoa husika na wakati mwingine hata majirani wasijue kwamba Mr & Mrs A walikuwa na matatizo makubwa katika ndoa yao. Siku hizi si hivyo kabisa mume/mke akiwa na matatizo basi watu wote anaowafahamu wakiwemo marafiki, majirani, colleagues, wasusi/vinyozi kule saloon atawaelezea matatizo katika ndoa yake. Hawa wengi wao huwa haiwatakii mema ndoa husika. Na wengine si ajabu wataweka matatizo hayo mtandaoni (hapa JF tumeshaona mifano chungu nzima siku za nyuma). Haya matatizo kujulikana na watu wengi kiasi hicho tena wengine wanasubiri kwa hamu kuona ndoa inasambaratika hayasaidii kwa kweli katika kudumisha ndoa. Wengine walioombwa ushauri wa nini mume/mke afanye kufuatia tatizo lilitokea ndani ya ndoa mfano mke/mume kutembea nje bila hata ya kufikiria athari kubwa sana labda kwa watoto katika ndoa ile hutoa ushauri, "Achana naye, wanawake/wanaume wa maana wako chungu nzima siku hizi." badala ya kujaribu kuwasaidia wana ndoa wale wamalize matatizo yao bila kuisambatarisha ndoa yao.

Utandawazi:

Miaka ya nyuma ilikuwa humtongozi mwanamke mpaka umemuona akakuvutia labda kwa sura yake, tabasamu lake, miguu yake, miondoko yake (kama Naomi Campbell au Tyra Banks 🙂🙂) wowowo lake n.k. Sasa hili lilihitaji muda kwa kweli ili uweze kumfuatilia binti huyo mpaka uweze kukubaliwa kama mpenzi, lakini siku hizi ni tofauti kabisa. Unaweza ukamtongoza binti yeye yuko bara tofauti na ulilopo wewe kupitia mtandao na huku hujawahi hata kumtia machoni. Na ikitokea akakubali basi mnaweza kujenga penzi la nguvu sana tena la kweli kabisa.

Pia mtandao na hata TV zimechangia kuwafanya wanandoa wasiwe karibu karibu kama ilivyokuwa miaka ya nyuma. Miaka hii utakuta nyumba nyingi zina TV mbili mbili mama anaangalia vipindi vyake na baba anaangalia vipindi vyake kila mmoja hapendi vipindi vya mwenzake. Pia utakuta kila mtu ana laptop yake mume yuko JF kwenye siasa na mke yuko MMU 🙂🙂 hawa hawapati muda kabisa wa kukaa kama mume na mke na kama wote ni waajiriwa basi hali ndio inazidi kuwa mbaya sana katika ndoa yao hata linapotokea tatizo dogo sana basi kwao huwa ni kubwa sana kwa sababu kwanza hawajuani kila mtu yupo kivyake vyake tu (MBL Married but lonely, MBA Married but available & MBU Married but unsatisfied) hahahahaha lol! watu kama hawa pamoja na kuwa wamo kwenye ndoa lakini hawajuani kabisa hivyo ni rahisi mno kufikia maamuzi ya kuachana kwa sababu hawana uchungu wowote na ile ndoa yao maana wanaishi kama strangers tu wanalala kitanda kimoja lakini ukiondoa kulala pamoja kila mtu yuko kivyakevyake. Tatizo dogo tu ndani ya ndoa basi mume/mke hata kabla ya kukaa chini kuongea na mwenzie kishakimbilia kwa marafiki kuelezea kilichotokea au kishaandika MMU 🙂🙂 kuomba ushauri bila hata ya ndugu wa karibu kwa wanandoa hao kutaarifiwa chochote kile kuhusiana na tatizo husika.

Nadhani kwa maoni yangu mambo haya yanachangia sana katika mporomoko mkubwa uliopo katika ndoa za kisasa ukilinganisha na zile za enzi zile na sidhani kama kuna uwezekano wa kurekebisha hali hii.




 
Hii mada imenivutia na nimesoma michango ya wote. Wote kwa njia moja au nyengine tunakubaliana kuwa mmomonyoko wa maadili, kutofuata mila na desturi zetu, kung'ang'ania haki na kusahau/kuepuka wajibu...pamoja na sababu nyingi tu, zinazofanya ndoa za kisasa kutodumu (kwa muda mrefu).

Kama angalizo tu, ningependa kwanza kukumbushia kuwa hata zamani zilikuwepo ndoa zilizoshindikana (jamaa yangu wa karibu aliwahi kuolewa mara 16, mara 3 aliolewa na mume huyo huyo). Pia wapo wanaume waliooa mara zisizo hesabu. Tafauti ya zamani sasa, ni kuwa zamani kesi za kuvunjika kwa ndoa zilikuwa zinahesabika, wakati sasa ndoa zinazodumu ndio zinazohesabika.

Kwa kuongezea kidogo katika mengi yaliyokwishasemwa, nitagusia nukta mbili:

1.- Kujuana saaana kabla ya ndoa" kunachangia. Hii inatafautiana na wazazi wetu waliokuwa wanaoa/wanaolewa/wanaoana hata bila ya kujuana. Nimeweka kwenye vifungo "kujuana sana" kwa sababu hivyo ndivyo tunavyojidai, eti kwa sababu tu wamelala kitanda kimoja miaka mingi kabla ya kuoana. Katika kipindiki hiki cha kubanjuana, kila mmoja huwa anaficha makucha yake na baada ya ndoa yanafichuka yale yote yaliyokuwa yamefichika.

2.- Wakati zamani kuacha/kuachika kulikuwa aibu na mjane alikuwa anaonekana vibaya katika jamii, leo mtu kujidai ni mjane imekuwa fesheni. Tumekutana na wangapi wanawake kwa wanaaume ambao wamo katika ndoa lakini wakitoka tu nje ya nyumba zao wanavua pete na/au kujitangaza ni wajane? Tumefikia mahali kujitaja kuwa umeoa/umeolewa tunaogopa kuoneka wa "zamani". Nina wasiwasi watu wa aina hiyo hata humu JF wamo. Na kama anecdote tu, nimeona majuu watu wanaandaa sherehe za kuacha/ kuwachwa. Sijui lini na hili nalo litafika kwetu, ikiwa bado halipo.

Kwa kuchangia tu mawazo kuhusu nini tufanye ili ndoa za vizazi vijavyo zidumu, nahisi njia pekee ni sisi tulioko ndani ya ndoa sasa kuzidumisha ndoa zetu na kuwa mfano mwema kwa vizazi vyetu, vyenginevyo hata tukaweka mitaala na silibasi mashuleni, ikiwa tunawafunza kile ambacho sisi tulishindwa kukitekeleza, wao hawataweza.

...kwa kiwango kikubwa nimecheka sana na mchango wako kwenye thread hii, mengi uliyoyaelezea ni kweli tupu na uniruhusu ku quote haya ambayo nitaendelea kuyatumia mara nyingi maishani mwangu;


....
zamani kesi za kuvunjika kwa ndoa zilikuwa zinahesabika, wakati sasa ndoa zinazodumu ndio zinazohesabika.
Tumefikia mahali kujitaja kuwa umeoa/umeolewa tunaogopa kuoneka wa "zamani"
....classic!

...ila hilo la huyo aliyeolewa mara kumi na tano dahh?, miongoni mwa hizo kaolewa mara tatu na mume huyo huyo? ...anafaa kungizwa kwenye Guiness Book of Records...
 
Mkuu Mbu mimi kwa maoni yangu mporomoko wa NDOA ZA KISASA unachangiwa na haya yafuatayo:

ELIMU:

Wanawake wa siku hizi wengi wamesoma sana ukilinganisha na wale wa miaka ile ambao asilimia kubwa walikuwa wameishia madarasa ya chini sana au hawakusoma kabisa. Elimu hii waliyoipata hawa wanawake katika ndoa za kisasa imewasaidia kwanza kujua haki zao ndani ya ndoa na pia kujua nini watakacho ndani ya ndoa. Si rahisi hawa kuwaburuza kama gari bovu kama walivyokuwa wanafanyiwa Wanawake katika ndoa za enzi zile ambao walikuwa wanayavumilia mengi sana ndani ya ndoa ili mradi watunze ndoa zao. Hawa wa kisasa wana kisomo cha hali ya juu, kazi nzuri na kipato kikubwa ambacho kinawawezesha kabisa kuishi wenyewe bila matatizo na hivyo kutohitaji kumtegemea mume katika mahitaji yao muhimu ikiwemo makazi, chakula n.k. Kwa maoni yangu si kweli hawa wana dharau au kiburi kama ambavyo Wanaume wengi tunavyodhani bali tu wanahitaji kuheshimiwa kama wake, kuonyeshwa mapenzi ya kweli, na kuthaminiwa kwa mchango wao ndani ya ndoa. Kunapotokea tatizo katika ndoa ambazo Wanawake wake ni wasomi mara nyingi hitimisho la Wanaume ni kwamba huyu ana kiburi kwa sababu kasoma, kwa sababu ana kazi nzuri na mshahara mzuri vitu ambavyo mara nyingi havina ukweli wowote. Unaweza kukuta tatizo dogo sana likawa kubwa kupita kiasi kwa dhana potofu kabisa na hata kuvunja ndoa.

Kuwashirikisha watu wa nje katika matatizo ya ndani ya ndoa:

Hapa ninamaanisha marafiki, mashoga, colleagues n.k. Zamani matatizo ya ndani ya ndoa yalikuwa yanajulikana kwa wanafamilia tena wale wa karibu sana. Hawa tatizo lilipotokea na wao kufahamishwa walijitahidi kwa hali na mali ili kuyamaliza matatizo katika ndoa husika na wakati mwingine hata majirani wasijue kwamba Mr & Mrs A walikuwa na matatizo makubwa katika ndoa yao. Siku hizi si hivyo kabisa mume/mke akiwa na matatizo basi watu wote anaowafahamu wakiwemo marafiki, majirani, colleagues, wasusi/vinyozi kule saloon atawaelezea matatizo katika ndoa yake. Hawa wengi wao huwa haiwatakii mema ndoa husika. Na wengine si ajabu wataweka matatizo hayo mtandaoni (hapa JF tumeshaona mifano chungu nzima siku za nyuma). Haya matatizo kujulikana na watu wengi kiasi hicho tena wengine wanasubiri kwa hamu kuona ndoa inasambaratika hayasaidii kwa kweli katika kudumisha ndoa. Wengine walioombwa ushauri wa nini mume/mke afanye kufuatia tatizo lilitokea ndani ya ndoa mfano mke/mume kutembea nje bila hata ya kufikiria athari kubwa sana labda kwa watoto katika ndoa ile hutoa ushauri, "Achana naye, wanawake/wanaume wa maana wako chungu nzima siku hizi." badala ya kujaribu kuwasaidia wana ndoa wale wamalize matatizo yao bila kuisambatarisha ndoa yao.

Utandawazi:

Miaka ya nyuma ilikuwa humtongozi mwanamke mpaka umemuona akakuvutia labda kwa sura yake, tabasamu lake, miguu yake, miondoko yake (kama Naomi Campbell au Tyra Banks 🙂🙂) wowowo lake n.k. Sasa hili lilihitaji muda kwa kweli ili uweze kumfuatilia binti huyo mpaka uweze kukubaliwa kama mpenzi, lakini siku hizi ni tofauti kabisa. Unaweza ukamtongoza binti yeye yuko bara tofauti na ulilopo wewe kupitia mtandao na huku hujawahi hata kumtia machoni. Na ikitokea akakubali basi mnaweza kujenga penzi la nguvu sana tena la kweli kabisa.

Pia mtandao na hata TV zimechangia kuwafanya wanandoa wasiwe karibu karibu kama ilivyokuwa miaka ya nyuma. Miaka hii utakuta nyumba nyingi zina TV mbili mbili mama anaangalia vipindi vyake na baba anaangalia vipindi vyake kila mmoja hapendi vipindi vya mwenzake. Pia utakuta kila mtu ana laptop yake mume yuko JF kwenye siasa na mke yuko MMU 🙂🙂 hawa hawapati muda kabisa wa kukaa kama mume na mke na kama wote ni waajiriwa basi hali ndio inazidi kuwa mbaya sana katika ndoa yao hata linapotokea tatizo dogo sana basi kwao huwa ni kubwa sana kwa sababu kwanza hawajuani kila mtu yupo kivyake vyake tu (MBL Married but lonely, MBA Married but available & MBU Married but unsatisfied) hahahahaha lol! watu kama hawa pamoja na kuwa wamo kwenye ndoa lakini hawajuani kabisa hivyo ni rahisi mno kufikia maamuzi ya kuachana kwa sababu hawana uchungu wowote na ile ndoa yao maana wanaishi kama strangers tu wanalala kitanda kimoja lakini ukiondoa kulala pamoja kila mtu yuko kivyakevyake. Tatizo dogo tu ndani ya ndoa basi mume/mke hata kabla ya kukaa chini kuongea na mwenzie kishakimbilia kwa marafiki kuelezea kilichotokea au kishaandika MMU 🙂🙂 kuomba ushauri bila hata ya ndugu wa karibu kwa wanandoa hao kutaarifiwa chochote kile kuhusiana na tatizo husika.

Nadhani kwa maoni yangu mambo haya yanachangia sana katika mporomoko mkubwa uliopo katika ndoa za kisasa ukilinganisha na zile za enzi zile na sidhani kama kuna uwezekano wa kurekebisha hali hii.






hahahahahahahahaha!....kaka asante sana kwa mchango wako japo hilo dongo hapo juu duuhhh!?
soulmate wangu akilisoma naomba asikuelewe...hehehe
 
  • Thanks
Reactions: BAK


hahahahahahahahaha!....kaka asante sana kwa mchango wako japo hilo dongo hapo juu duuhhh!?
soulmate wangu akilisoma naomba asikuelewe...hehehe


....Hahahahahah lol! madongo yote yatakayorushwa nitaomba yaelekezwe kwa muanzisha thread lol!
 
Ukiona tuko kimya ujue ni Conservative, siamini katika haki za wanawake.

labda na yeye ni wa hivyo.
Nakimbia nisije pondwa mawe bure.

Mmomonyoko wa ndoa umeanzia kwenye haki za wanawake.

Kwa mara ya kwanza nakuona Dada Mkuu ukiweka mpira kwapani...

Njoo bwana useme yanayokukereketa..

Au umeamua kuzira hata ndoa yenyewe??

Babu DC
 

....Hahahahahah lol! madongo yote yatakayorushwa nitaomba yaelekezwe kwa muanzisha thread lol!

Hapana Kaka,

Sheria za JF zinasema kuwa mwenye dhamana ni mwandishi!!

Nimeupenda sana mchango wako.....Hizo MBs, ....hakuna ambayo inawaelezea wale wachache ambao wanasikia hizo hadithi nje??
 
Kwa mtazamo wangu na jinsi nilivyo expirience ndoa yangu (zaidi ya miaka 30) na jinsi nilivyoamua na kusikiliza kesi nyingi sana zinazohusiana na wana ndoa, tatizo si "mfumo dume".

Tatizo nnaloliona mimi kubwa zaidi katika ndoa ni "incompatibility". Kwa maana halisi ya neno la Kiswahili "kuoana", chukulia mfano wa viatu, viatu ili uvivae ni lazima "Vioane" huwezi kuvaa "stiletto" mguu mmoja na ukavaa "kanda mbili mguu mwingine" ni simply havioani. Inabidi watu waelewe maana halisi ya neno "kuoana" na si kuoa au kuolewa. Zamani wazee wetu walikuwa wanaijuwa namna ya "kuoana" na si kuowa au kuolewa. Ndoa za zamani nyingi zilikuwa ni arranged, na mchumba huchunguzwa na ndugu au wazee wa pande zote na wakiona hawa "wanaoana" ndio hutimiza mambo ya ndoa.

Siku hizi ni "different", tunataka kutafuta wenyewe tuolewe au tuowe na tuliyemtafuta. Hii hupelekea kila mmoja kuwa "actor" au "actress" kwa mwenzie, lakini inapofikia "reality" inabidi "acting" ife, na hapo ndipo huanza matatizo yote.
safi sana FF kumbe kwny haya mambo unaakili namna hii tofauti na kulee kwenye siasa........u made ur points very clear n loud.:violin:
 
Nimeshasikia siku hizi hata wasichana hawataki kuolewa na wao wanataka kuoa! Siri hapo ipo kwenye Kuoana, kuoa au kuolewa?.

Watakaodumu ni wale wanao oana na si wanao olewa wala kuoa. Huo ni mtazamo wangu, na mimi binafsi yangu ni "proof" ya hilo. tume oana na Gozi langu. Hajanioa wala Sikumuoa. Nadhani vijana wa sasa na wajao wanatakiwa waelewe maana ya kuoana.
unazidi kunifungua akili FF ,natamani na mm nipate wa kuoana naye lol.:busu
 
Hapana Kaka,

Sheria za JF zinasema kuwa mwenye dhamana ni mwandishi!!

Nimeupenda sana mchango wako.....Hizo MBs, ....hakuna ambayo inawaelezea wale wachache ambao wanasikia hizo hadithi nje??

Sijakupata Mkuu DC naomba ufafanue
 
Mbu kwanza kabisa naunga mkono hoja zote za waliochangia tayari. Nakubaliana na maelezo sawia aloyatoa AshaDii na wengineo ila naomba nitoe ufafanuzi kidooogo.
Kuhusu women's rights au kujitambua kwa wanawake kama ilivyosemwa na wengi waliotangulia. Kwa mtazamo wangu hiki si kitu kibaya hata kidogo. Sidhani kama ni vibaya kuwa au kuzitambua haki za kila mmoja wetu. Tatizo nilionalo hapa ni namna tulivyoyapokea haya "Mahubiri" ya Women's Rights. Wanawake wengi tumejikuta tukishabikia haki hizi kama wafungwa washabikiavyo msamaha wa rahic bila kufikiria ukitoka jela humu utaishije ili usiharibu tena. Wanawake wengi wamepotea mahubiri haya kwa ushindani ule wa ...haya sasa nasie tuna haki. Ushindani ambao umepelekea wengi wetu kujikuza na kujikweza huku tukizisahau staha zetu, heshima zetu na ustaarabu wetu.

Laiti tungeyapokea 'mahubiri' haya na kuyajazia kwenye kikapu chetu chenye staha, heshma na ustaarabu apaswao mwanamke badala ya kuzitoa staha, heshima na staarabu zetu na kuzitupa nje ili Women's rights zipate nafasi. (hapa ninayo mengi kuongea utafikiri nimelipwa na TAMWA)

Kuhusu Upendo:
Kwa mtazamo wangu mie haya mapenzi ya "Egoli" tuliyoyaiga toka kwa wazungu yamechangia kwa kiasi kikubwa udhaifu katika ndoa nyingi za siku hizi. Hii kujidai unataka kufall in love ndo uoe/olewe imetupelekea kuiumbia na kuikubali counterprt ya falling in love ambayo ni falling out of love. Siku hizi si jambo la kushangaza kujikuta unaitwa kwenye kusuluhoisha ndoa ambayo mmoja wa wanandoa hao alilala tu usiku na kuamka asubuhi akiwa ameshafall out of love na sasa anadai talaka au anataka kuvunja ndoa. Na ajabu sana kuna kila aina ya justification ya hii falling out of love ambayo mwisho wa siku tunalazimika kukubaliana na muota ndoto huyo.
Wazee wetu wa zamani hawakuwaga na falling in love bali walikuwa na Growing in love...it just keep on growing hakuna kufall out na ndio maana walikuwa wavumilivu. Kwa kuwa unaishi kwenye ndoa ambayo kadri siku ziendavyo love inajijenga, kukua na kukomaa hata ukifanyiwa kosa gani wewe unajihisi kumpenda zaidi ingawa kwa manung'uniko kwa ndani! Ndoa za siku hizi kwa kadri unavyokosea mwenzio ndivyo anavyoendelea kuizungusha door knob ya love na mwisho anaufunguua na baaam amefall out.

Samahani imekuwa ndefu.
usijali nimeisoma yote ,lol!kweli mapenzi ya tamthilia yanaharibu...jamani ya kina Alehandro tuwaachie kina Alehandro wenyewe na tamthilia zao.:ranger:
 
Sijakupata Mkuu DC naomba ufafanue

Umetaja tatu,

MBL
MBA
MBU,

Hakuna abbreviation inayotumiwa kwa wale ambao wako ecological (wanatesa kwa raha zao na kusikia hizi simuliz kwa wengine)??
 
...ila hilo la huyo aliyeolewa mara kumi na tano dahh?, miongoni mwa hizo kaolewa mara tatu na mume huyo huyo? ...anafaa kungizwa kwenye Guiness Book of Records...
Zilikuwa mara kumi na sita, na wanaume 13. Cha ajabu, mume wa mwanzo ambaye alilazimishwa na jamaa yake, mara ya mwanzo hawakukaa hata mwaka mmoja wakawachana. Badae akaolewa na waume wengine mara nne, mume wa kwanza akamwoa tena na kuishi pamoja miaka 10, wakawachana: Bibi akaendelea kuolewa tena na tena na tena hadi mara 7, mwisho akaja kuolewa na mume yuleyule wa mwanzo mpaka wakafariki wazee, kwanza bwana badae bibi. Cha ajabu, wakati bibi alikuwa anaolewa, bwana alikuwa anasubiri awachwe aoe tena. Very sad, hawakupata watoto.
 
Back
Top Bottom