Ndoto 20 zinazoweza kukufunga kwenye umaskini bila kujua – Tafsiri yake itakushangaza!

Kivipi shule na umaskini they aren't related it's also a symbolic?
 
Hamnaga hayo mambo katika imani ya maisha yangu..huwa naona ni mambo ya kawaida tu
 
Namba 23 niliwai kuota sana,nikaja pata bonge la kesi utawala wa Jiwe.,kesi ya kubumba lakini ilinipurula zaidi ya uchumi wangu wote
 
Mara nyingi binadamu huota vitu anavyohisia ktk shughuli za kila siku. Hakuna mahusiano na ufukara au umadikini.
  • Njia za kufanikiwa zipo nyingi;
  • Ukitokea familia maskini harsal sana usideke;
  • Wekeza ktk vitu vitakavyoiva miaka kadhaa ijayo
 
Kivipi shule na umaskini they aren't related it's also a symbolic?
Mtu ambaye hakwenda shule hawezi kuota yupo shule, akiota basi ni lazima atakuwa alitengeneza taswira ya kutamani kuwa darasani sasa wakati wa kulala ndo ubongo ukahisi unajukumu la kukamilisha kile ambacho uhalisia ulitamani kitokee, the same na kuokota pesa mara nyingi itatokea wakati ambao unahisi ana uhitaji wa pesa ama unaziwaza sana pesa.

Mkuu umeshawahi kuota unaongea kichina?
 
Namba 23 niliwai kuota sana,nikaja pata bonge la kesi utawala wa Jiwe.,kesi ya kubumba lakini ilinipurula zaidi ya uchumi wangu wote
Ndoto ambazo zinahusiana na destiny yako huwa zinakuwa zipo symbolic kiasi cha kuhitaji taafakuri ya kina kuelewa.


Ila hizo ndoto ulizotaja hapo juu ni za kawaida .

Maana kuna rafiki yangu ni mchungaji Ila alikuwa anaota yupo uchi anatoa mahubiri
Rafiki yako mwambie hao kondoo anaowapiga pesa zao, watasanuka na kumshushia kipigo kitakatifu soon!
 
Namba 23 niliwai kuota sana,nikaja pata bonge la kesi utawala wa Jiwe.,kesi ya kubumba lakini ilinipurula zaidi ya uchumi wangu wote

Rafiki yako mwambie hao kondoo anaowapiga pesa zao, watasanuka na kumshushia kipigo kitakatifu soon!
This things ni kweli ila kutokana na ubishi wa watu watakataa
 
Mungu hutafuta njia ya kuonesha mtu kitu kwa kupitia vitu anavyo viishi
 
Si umasikini pekee, na ukikojozi juu
 

Attachments

  • ‎@umjafar422‎20250113‎_Phoenix.mp4
    747.3 KB
Sawa ila je utahakikishaje kama ni Mungu ama ni matokeo ya mawazo yako.
Mambo yanatokea ndio uthibitisho kwangu kuwa sayansi Ina aim kumpinga Mungu
It's like mfano wa haya mambo eti Dunia ndio inazinguka jua ni upuuzi mtupu wa sayansi zenu tu no such a thing
 
Ndoto zangu kuu zinazojirudia mara kwa mara:

1. Kuota napaa angani

Yaani mikono inapiga upepo kama ndege wanavyofanya kwa mbawa zao, na nikiamua kupaa juu zaidi napaa tu. Mara nyingi naota nikipaa kuepuka hatari fulani, burudani au kuwahi sehemu. Lakini imekuja miaka ya karibuni baada ya kuusikiliza sana wimbo wa I believe I can fly wa mwamba R. Kelly. Sasa sijui kama ni ishu ya kiroho au ni huo wimbo kunikaa kichwani.

2. Kuota nafanya mtihani na jahazi linazama
Mara nyingi naota nikiwa chumba cha mtihani huko shule au chuo, aidha nipo nje ya muda au maswali ni magumu sana na muda unayoyoma nikiwa sina cha kuandika. Mfano juzikati niliota nipo nafanya mtihani wa mwisho chuo nikiwa nje sana ya muda baada ya kupewa mtihani na kusinzia masaa mawili na dk15 nashtuka nimebaki na dk45 halafu maswali manne yote yana vipengele a & b vyote vikihitaji essay, na sioni hata swali ninaloliweza angalau nianze nalo. Wakati chuo nilishamaliza na sikuwahi kukutana na tabu za namna hiyo. Kila nikiota ndoto ya namna hii nabaha na kujisikia vibaya kabla ya kuamka.

3. Kuota napigana ila mapigo yangu hayafiki kwa mlengwa
Naota napigana na adui/maadui, nimejaa hasira kwelikweli, lakini kila pigo ninalorusha iwe ngumi, kichwa, teke au hata jiwe nakuwa kama kuna nguvu isiyoonekana inanivuta na kufanya mapigo yangu yasiwe na nguvu kabisa hivyo kuishia hewani.

4. Kuota nakimbizwa ila hatua hazitoki
Naota nakimbizwa na nyoka, wanyama wakali wa mwitu au wanyama hatari zaidi duniani (binadamu) wanaolenga kuniua (mara nyingi naota nyoka mkubwa), najaribu kuvuta hatua kwa nguvu na speed kali lakini kunakuwa kama kuna upepo mkali unanipush kwa nyuma hivyo siendi popote.

Hapo mtoa mada una maoni gani?

Binafsi huwa si mtaalam au mtu ninayejali mambo ya ulimwengu huo wa roho maana imani yangu huko ni haba sana, hivyo huwa sitilii maanani kabisa.

Uzuri wa ndoto hata iwe mbaya kiasi gani hautoota imekufa, bali ikifikia kiwango cha mwisho cha hatari unaamka😁
 
Kemea hizi ndoto mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…