Ndugai avuliwe U-spika wa Bunge, kutokana na kuikanyaga Katiba ya nchi kwa kung'ang'ania kuwakumbatia wabunge wa viti maalum wa Chadema

Yeye hawezi fuata katiba bali katiba itamfuata yeye.
 
Tunakemeaje mkuu Mystery?! Tunakemeaje?! Na sasa kuna wizara mpya ya kupambana na ‘freedom of speech’, Mawasiliano na Teknologia ya Habari!’ Hiki ‘kijiwe’ tu hapa, tutafutana, wee subiri tu!
santesandy
Ndiyo maana yake hao wanaowaita mabeberu wamegoma na tutazisikia kwenye bomba tu hizo shilingi trillion 2 zao kwa ajili ya kukuza Demokrasia nchini............

Hivi wazungu wanaleta hela zao kwa ajili ya kukuza Demokrasia, halafu wanagundua kuwa sisi tunaendelea kuiminya Demokrasia, hivi kweli hata kama pesa yao haina kazi, wataendelea kweli kutuletea hayo mapesa?
 
Ndugai anajivunjia heshima sana na kulidhalilisha bunge, kila mbunge anamizizi yake, mizizi imekatwa unashikiliaje huko juu,
Akifukuzwa wa CCM, kimya, cuf ya Lipumba kimya na unatekeleza taratibu, akifukuzwa wa chadema unajifanya unakingia kifua na ufuati taratibu, tabia hii hadi lini? Au kwa kuwa inampendeza jiwe, maana jiwe upenda uonevu na kuabudiwa!
 
t
TATIZO LA KUPEANA "VYEO"! Ndugai hana sifa za kuwa "spika"(mkuu wa mhimili" wa nchi.Alitakiwa awe mkuu wa kitengo cha utafiti wa maumbile nyeti ya wanyama pori ktk chuo kinachotoa taaluma kiwango cha cheti! Alipo ni ngekewa ya ajabu sawa na jamaa aliyetajirika kwa kuangukiwa na jiwe la thamani ughaibuni!
 
Hakika kwa kuwa anaicheza "tune" ya Jiwe ya kuvidhalilisha vyama vya upinzani, hususani Chadema, ndiyo hivyo tena Jiwe anachekelea hafi jino la mwisho............

Na huyo Spika anafuata nyayo za Bosi wake Jiwe kwa kuiona Katiba ya nchi kama takataka na hataki tena kuisimamia Katiba ya nchi aliyoapa kuitii na kuiheshimu...........

Lakini haya yote yana mwisho, hayataweza kudumu milele na milele
 
Inategemea na mazingira na tafsiri ya sheria kwa mahitaji ya wakati huo. Huwezi kuitafsiri sheria kwa mrengo wa kumbeba adui.

Ndio maana hata Chadema wanapoogelea kutolewa kwa Hanje gerezani saa 1 usiku hawawaambii wanachama wao kuwa waliotolewa ni wengi akiwemo Twaha Mwaipaya. Usidhani ni wajinga, wanajua wanachokifanya.

Sasa hapa kuwa mpole kila mbuzi ale kwa urefu wa kamba yake.
 
Ebu mnijuze. Katiba ya Chadema inasemaje kama mwanachama atakiburuza chama mahakamani?
Hata kama inazuia mwanachama kwenda mahakamani bado mahakama itasikiliza na kutoa hukumu kwani ndio mhimili pekee unaoweza kutoa maamuzi katika mambo yanayohitaji tafsiri ya sheria kwa taasisi mbalimbali na watu binafsi. Ila katika kutoa maamuzi itajikita katika katiba, kanuni na utaratibu wa chama.

Kwa hiyo hakuna katiba inaweza kuzuia mwanachama wake kwenda mahakamani.
 


Hivi hilI bunge lilowekwa la kumwaga damu ni bunge halali ??
 
Hadi hapo rufaa yao itakapokubaliwa wao si wanachama wa chama chochote cha siasa na kwa hiyo si wabunge. Rejea kesi ya Sophia Simba na wabunge wa CUF kambi ya Maalim za mwaka 2017 zilizoamuliwa na huyuhuyu Ndugai ambae leo anaamua kuisigina katiba.
 
Hadi hapo rufaa yao itakapokubaliwa wao si wanachama wa chama chochote cha siasa na kwa hiyo si wabunge. Rejea kesi ya Sophia Simba na wabunge wa CUF kambi ya Maalim za mwaka 2017 zilizoamuliwa na huyuhuyu Ndugai ambae leo anaamua kuisigina katiba.
Mkuu hebu rejea post yangu namba 26 hapo juu maana hicho unachosema nimeshakieleza.

Haijalishi nini, sheria ina tafsiri zake na ndio maana unaweza ukakuta Hakimu kamhukumu mtu lakini akikata rufaa anashinda.

Kwa hiyo sheria hutafsiriwa wakati mwingine kulingana na mazingira yaliyopo. Ndio maana hata wewe unarejea mazingira ya akina Sofia Simba na wale wa CUF.

Hata hivyo Chadema ikiwaacha wabunge 19 wakaendelea haina cha kupoteza kwani Chadema haina mpango wa kuteua wabunge Viti maalumu 🤣🤸‍♂️
 
Spika akili yake imeshaoza,ngoma imekimbilia kichwani.
 
Suala siyo CHADEMA kupoteza ama kutopoteza bali ni kuheshimu katiba ambayo ni wajibu wa kila mtanzania.
 
Bunge limetokana na uchaguzi haramu na ndio maana kumesusiwa kupeleka majina ya viti maalum kwa sababu kuwa na wabunge katika hilo bunge ni sawa na kuhalalisha haramu. Ila hapo hapo kunalalamikiwa kwa kutofuatwa katiba katika bunge hilohilo lililo susiwa kwa sababu si halali.
 
Suala siyo CHADEMA kupoteza ama kutopoteza bali ni kuheshimu katiba ambayo ni wajibu wa kila mtanzania.
Katiba inasemaje?
Sheria na kanuni zilizoweka kutekeleza matakwa ya katiba zinasemaje?

Labda tuanzie hapo maana tunaweza kuwa tunabwabwaja tu katiba katiba kumbe hata kujua matakwa ya katiba hatujui.
 

Kipi kinaharamisha uchaguzi wa 2020.

Weka ushahidi, kama viongozi wenu hawaamini polisi na serikali ushahidi upelekwe jumuiya za kimataifa. Mnaleta porojo za unfunded claims on election fraud wakati mnajua kabisa wamepigwa kweupe. Mnaokoteza makaratasi mnayachoma. Mnatangaza mmekamata gari lina kura, gari lina usajili wa namba gani na mmiliki wake ni nani na kama mmelikamata ina maana lipo kwenye milki yenu, mmelipeleka wapi?

Hiki ni kichaa kama vichaa vingine unaletewa jambo unabeba tu hata hauongezi na za kwako.
 
Mkuu mbona hili la wabunge wanawake 19 ni la kawaida sana. Kuna uwezekano CHADEMA bado hawajaandika barua ya kumfahamisha speaker kwamba wamewavua uanachama. Mimi naamini barua haijaandikwa ndio maana Mwenyekiti Mbowe kawafungulia milango na akawasihi waje waombe msamaha wayamalize

Jambo la ajabu kwangu ilikua ni yule Mbunge Mwambe ambaye mwenyewe alitangaza hadharani kuhama CHADEMA lakini spika akaendelea kumtambua kama mbunge halali
 
Ndizo hizo ninazosema "double standards" ambazo kama mhimili mmojawapo wa dola, Spika wa Bunge hapaswi ateleleze majukumu yake kiaona hiyo, kwa hiyo hakuna namna nyingine ya kulinda heshima yake na heshima ya Bunge la nchi, isipokuwa ni kujiuzulu tuuuuu
 
Hunijui sikujui,sasa nakushangaa unaongea kama unamungelea mtu unayemjua.

Mie sio hao unaowazungumzia hata hivyo pia huwezi kuwa na akili timamu ukasema et "mmepigwa kweupe" yani kwako wewe uchaguzi unaona ulikuwa sawa kabisa?
 
Tumpuuze huyu mtu kwani ni mwaharibifu wa kodi zetu huku akisigina katiba na sheria mbalimbali kiasi kwamba bunge limekuwa kijiwe cha porojo na umbea wakike kila kukicha! wabaki kama bunge la kamati ya ccm waamue watakavyo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…