Ndugai awaponda wana Mwanza kwa kuezeka nyumba zao na Mabati ya kizamani, Masufuria

instagram

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
2,118
Reaction score
4,863
Akitoa salamu zake mbele ya Rais Samia kwenye sherehe za wafanyakazi, spika wa bunge Job Ndugai amesema Mwanza ingependeza kama wangeacha kuezeka nyumba zao kwa masufuria, akisema

"Mwanza kunapendeza lakini kwanini mnafunika nyumba zenu na masufuria? ,Ingependeza kama mngeezeka nyumba zenu na mabati ya kijani".

Hii ni dharau kubwa sana kwa mtu mkubwa kama Spika kutoa dharau kwa watu ambao kipato chao ni kidogo na ndiyo maana nyumba zao wameezeka na mabati ya sufuria.

Kweli viingozi wetu wakipata uwezo mkubwa wa fedha wanasahau kabisa kwamba kuna wengine hawana uwezo kama wa kwao .
 
kuna mtu alitabir huyu dingi atanyooka..naona kmy
 
Hujui hata maana ya utani!!??
utatapika nyongo bure....
Tek it easy
 
Huyo mgonjwa achana naye. Kule kwao Wanaezeka kwa udongo
 
Kwani wagogo wameacha lini kula panya?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…