Pre GE2025 Ndugai huna chako Jimbo la Kongwa, Hersi Said wa Yanga ni Mbunge ajae Kongwa

Pre GE2025 Ndugai huna chako Jimbo la Kongwa, Hersi Said wa Yanga ni Mbunge ajae Kongwa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Labda useme huyo Hersi anaanza campaign mapema dhidi ya wenzake, pengine nyuma yake yupo huyo-huyo Ndugai maana ana-unazi kwenye ushabiki wa mpira nae.

Vinginevyo Kongwa 2025 ni gombania goli, Ndugai alishasema huu ni muhula wake wa mwisho kabla hata ya sakata la kuvuliwa ubunge, yeye hatogombea tena ubunge 2020 ni mara yake ya mwisho.
 
Mzee akisoma hii mada atakufa Kwa presha...injinia anaweza kugombea Jimbo lolote Tanzania na akashinda SAA 4 asubuhi
Yeye alishasema anastaafu pia jua kuwa ataendelea kupata mshahara na marupurupu ya uspika mpaka kifo. Sasa shida iko wapi hapo!
 
Nilipopata tetesi hizi za Rais wa Yanga kuwa mwaka 2025 atakwenda kugombea ubunge Jimbo la Kongwa nilibisha na sababu iliyonifanya nibishe ni sijawai kumuona Enjinia Hersi Said akijiusisha na Siasa kivile, lakini jana ndio nimepata uthibitisho kuwa Rais huyu wa Yanga 2025 atavuta Fomu ya Ubunge Kongwa

Siku ya jana ilikuwa na Siku ya Kuzaliwa Mwenyekiti wa Makampuni ya GSM Gharib Said ambapo alitumia siku hii kusheherekea kwa kutoa misaada ya kijamii kwenye mji mdogo wa kibaingwa hii maana yake ni nini?

Kilichofanyika jana ni akili kubwa katika kuanza kampeni za kulichukua jimbo ilo la kongwa kutoka mikono mwa Spika mtaafu Na Mbunge anamaliza Muda wake Job Ndugai, ambae yeye binafsi alitangaza kuachana na ubunge lakini kama kawaida wanasiasa wa afrika tabia ya kuachia madaraka awana bali upandikiza warithi, ambapo Job Ndugai Toka uchaguzi wa ndani wa Ccm alianza kupanga Safu ya Viongozi ambayo watakuja kumuunga mkono mlithi wake ambae ni Mkewe Bi Fatuma Mganga ambae ni Katibu tawara wa Mkoa wa Singida.

Hersi ametumia medani za Kivita kuingia Jimbo La Kongwa kwa kuitumia Taasisi ya Gsm na pamoja na Siku ya Kuzaliwa kwa Gharib Said Kuchiti maneno kuwa ameenza kampeni mapema, na kudhilisha ilo kuwa Hersi ameanza Mahesabu ya Ubunge Kongwa, ameanzia harakati zake Mji Mdogo wa Kibaingwa ambapo Kata Hii Ndio Utoa uamuzi Mbunge wa Kongwa awe nani.

Pamoja na Kata ya Kibaingwa kuwa sehemu ya maamuzi ya Ubunge wa Kongwa, Kibaingwa ni Eneo ambalo Job Ndugai wakati wote wa Ubunge wake amekuwa akipata upinzani mkubwa kuanzia kwa wanaccm wenyewe na vyama vya upinzani, kwa maana nyingine unaweza kusema Injinia Hersi Said ameanzia kumpiga Ndugai kwenye Donda Ndugu lake kuelekea kuchukua Jimbo La Kongwa Ambalo Ndugai alishakuwa anamuandaa Mkewe kuwa Mbunge 2025.

Ikumbukwe Injinia Hersi ndio anasimamia Uendeshaji wa Makampuni Ya GSM kwaiyo akili kubwa ya Hersi imetumika kuanza kampeni kwa kuitumia GSM FOUNDTION.

Unaweza ukajiuliza kwanini Hersi said anaenda kugombea ubunge kongwa endelee kunifatilia mzee code nitakuja na uzi kipi kimesababisha Hersi kusaka ubunge tena kongwa unaweza ukajiuliza Hersi na Kongwa wapi na wapi amekuwa mkazi wa Kariakoo, amesoma dar Tulia uzi unakuja soon.
Ajiandae kupigwa gongo la kichwa hadi azimie sawa na yule mgombea wa miaka ile!.
 
Yeye alishasema anastaafu pia jua kuwa ataendelea kupata mshahara na marupurupu ya uspika mpaka kifo. Sasa shida iko wapi hapo!
Kwani wanafuatiliaga siasa za Tanzania basi, Ndugai alishatangaza hadharani 2020 ndio mwisho.
 
  • Thanks
Reactions: UCD
Nilipopata tetesi hizi za Rais wa Yanga kuwa mwaka 2025 atakwenda kugombea ubunge Jimbo la Kongwa nilibisha na sababu iliyonifanya nibishe ni sijawai kumuona Enjinia Hersi Said akijiusisha na Siasa kivile, lakini jana ndio nimepata uthibitisho kuwa Rais huyu wa Yanga 2025 atavuta Fomu ya Ubunge Kongwa

Siku ya jana ilikuwa na Siku ya Kuzaliwa Mwenyekiti wa Makampuni ya GSM Gharib Said ambapo alitumia siku hii kusheherekea kwa kutoa misaada ya kijamii kwenye mji mdogo wa kibaingwa hii maana yake ni nini?

Kilichofanyika jana ni akili kubwa katika kuanza kampeni za kulichukua jimbo ilo la kongwa kutoka mikono mwa Spika mtaafu Na Mbunge anamaliza Muda wake Job Ndugai, ambae yeye binafsi alitangaza kuachana na ubunge lakini kama kawaida wanasiasa wa afrika tabia ya kuachia madaraka awana bali upandikiza warithi, ambapo Job Ndugai Toka uchaguzi wa ndani wa Ccm alianza kupanga Safu ya Viongozi ambayo watakuja kumuunga mkono mlithi wake ambae ni Mkewe Bi Fatuma Mganga ambae ni Katibu tawara wa Mkoa wa Singida.

Hersi ametumia medani za Kivita kuingia Jimbo La Kongwa kwa kuitumia Taasisi ya Gsm na pamoja na Siku ya Kuzaliwa kwa Gharib Said Kuchiti maneno kuwa ameenza kampeni mapema, na kudhilisha ilo kuwa Hersi ameanza Mahesabu ya Ubunge Kongwa, ameanzia harakati zake Mji Mdogo wa Kibaingwa ambapo Kata Hii Ndio Utoa uamuzi Mbunge wa Kongwa awe nani.

Pamoja na Kata ya Kibaingwa kuwa sehemu ya maamuzi ya Ubunge wa Kongwa, Kibaingwa ni Eneo ambalo Job Ndugai wakati wote wa Ubunge wake amekuwa akipata upinzani mkubwa kuanzia kwa wanaccm wenyewe na vyama vya upinzani, kwa maana nyingine unaweza kusema Injinia Hersi Said ameanzia kumpiga Ndugai kwenye Donda Ndugu lake kuelekea kuchukua Jimbo La Kongwa Ambalo Ndugai alishakuwa anamuandaa Mkewe kuwa Mbunge 2025.

Ikumbukwe Injinia Hersi ndio anasimamia Uendeshaji wa Makampuni Ya GSM kwaiyo akili kubwa ya Hersi imetumika kuanza kampeni kwa kuitumia GSM FOUNDTION.

Unaweza ukajiuliza kwanini Hersi said anaenda kugombea ubunge kongwa endelee kunifatilia mzee code nitakuja na uzi kipi kimesababisha Hersi kusaka ubunge tena kongwa unaweza ukajiuliza Hersi na Kongwa wapi na wapi amekuwa mkazi wa Kariakoo, amesoma dar Tulia uzi unakuja soon.
Familia yake ni watu wa Njoge, Ngomai, Kibaigwa,.
Hersi asili yake ni Mtoto wa Maeneo ya Ngomae na Njoge.
Week mbili zilizopita alikuwa Msibani Kwa Babu yake mzaa Mama ambae ni Mkazi wa Njoge.
 
Sina hakika kama kweli ni Engineer, Ila hata kama lingekuwa jiwe, ningelichagua kuliko Ndungai.

Huyu Mzee hajawahi kuwa msaada wowote pale Kongwa, Ubunge na uspika miaka kumi, lami kilometa 10. What a shame!
 
Sina hakika kama kweli ni Engineer, Ila hata kama lingekuwa jiwe, ningelichagua kuliko Ndungai.

Huyu Mzee hajawahi kuwa msaada wowote pale Kongwa, Ubunge na uspika miaka kumi, lami kilometa 10. What a shame!
Sio yeye tu kwani unafikiri hao wengine huko majimboni kuna maajabu. Bongo hata ucjague nani hakuna nafuu yoyote, ni kama tumesuswa
 
Wakati wa Magufuli bwana ndugai alikuwa na makazi ikulu dsm mana kila jamaa akiitisha zile lectures zake za asubuhi, speaker alikuwa wa kkwanza kufika hapo.
Fikiria bunge linaweka/kupanga bajeti inapitishwa na bunge, kisha speaker wa bunge anarudisha CHENCH?
NYAKATI SIYO MILELE
Wakati wa dhalim Magufuli Ndungai alikuwa kama Houseboy wake.
 
Labda useme huyo Hersi anaanza campaign mapema dhidi ya wenzake, pengine nyuma yake yupo huyo-huyo Ndugai maana ana-unazi kwenye ushabiki wa mpira nae.

Vinginevyo Kongwa 2025 ni gombania goli, Ndugai alishasema huu ni muhula wake wa mwisho kabla hata ya sakata la kuvuliwa ubunge, yeye hatogombea tena ubunge 2020 ni mara yake ya mwisho.
Ndungai ni Simba lia lia.
 
Hii unafanya ni kazi ya maskini, acha

Maskini ndio huandika maandiko kama haya yako. Maskini ndio husifia na kuabudu watu namna hii
Nashauri badala wewe kutafuta habari kuja kuandika kwa mbwembwe huku, unapaswa wewe ndio uwe habari uandikwe kwa mbwembwe. Inawezekana, usijipe unyonge
ukiwa na maana mimi tajiri?
 
Mimi ningalimshauri engineer akawekeza zaidi ktk maisha yake baada ya kufa, mipira , siasa ni ya muda mfupi tu badala ya kujenga madrasa, misaada ktk misikitini ndio bora zaidi
Hakuna maisha baada ya kufa.
Ukifa unapoteza kumbukumbu, uhai wako unahama kwako unaenda kwa viumbe wengine watakao tumia mabaki yako kama chakula au kirutubisho.
You will become null and void.
Mengine ni kutishana tu ili ufuate mashariti na mafundisho ya dini.
 
Tanzania habari za nani anajipanga kugombea wapi ndizo taarifa kubwa kuliko maendeleo, katiba mpya na kadhalika.

Ndugu zangu. Huu uzombi ututoke. CCM inapaswa kupigwa chini nchi nzima
Umeandika jambo kubwa sana
 
Back
Top Bottom