Ndugai: Lishe duni ya wachezaji wetu imechangia Taifa Stars kufungwa

Hivi hao wachezaji wakisema nchi yetu inayumba kwasababu bunge ni dhaifu, wataitwa mbele ya kamati ya maadili?
 

Kwa hiyo Jiwe wa West????!!! Sasa hiyo 9 spika mwenyewe mdumavu na anamjua Diego, Mesi au Salah??? Mengine yaacheni yapite tu
 
Katoa point ,kwenye masuala ya michezo ,subwoofer yake ina password.
 
Kwa hiyo Jiwe wa West????!!! Sasa hiyo 9 spika mwenyewe mdumavu na anamjua Diego, Mesi au Salah??? Mengine yaacheni yapite tu
Jiwe awe wa west kwani mrefu? Si ndio common type za kibongo?
Nachokataa ufupi kwa wabongo iko related na specie na genes kuliko lishe duni,ingekuwa ni lishe basi warefu wote wangekuwa smart kichwani na wafupi wote wangekuwa dungaembe sasa haiko hivyo
Kingine hata utumwa ulikuwa zaidi West Africa ambako kuna giants people kuliko east Afrika ambako waarabu waliiga tu,kule watu ni wakubwa ila hawana akili ile miili ni kukabiliana na harsh conditions
 

Namaanisha tumefungwa na timu bora kuliko sisi sasa sababu za kijinga ndio hatutaki. Timu yetu na maandalizi yetu bado yanafanya tusiwe washindani wazuri sie tunawekeza katika maombi na zari sasa sababu za Ndugai ndio kaongea ujinga.
 
Acha upimbi kuwa na mwili ambao umeshiba sio lazima uwe na kitambi wewe.Umemuona Samatta alivyo na nguvu kuliko hata john Bocco ambae mwili mkubwa tu lakini nguvu hana.
Nawe unaungana na sabufa?
 
..nilivyouangalia ule mchezo sikuona kama Wasenegali walituzidi kwasababu tuna maumbo madogo kulinganisha na wao.

..Kwa maoni yangu, wachezaji waliokuwa uwanjani wana miili inayowawezesha kushindana ktk mechi za kiwango chochote kile.

Kweli kbs najaribu kuwatafakari wachina wana umbo dogo lkn wapo World Cup
 
Wachezaji wetu hawajapitia misingi ya mpira wamejikuza wenyewe tu,tukiwekeza ndiyo tulaumu saizi hakuna mtu wa kumnyoshea kidole mwenzake
 
Ni Kweli.
Wachezaji wetu wana tatizo la Lishe Duni.
Mishahara wanayopata haikidhi kupata chakula kinacho kidhi kwa mchezaji wa Soka.
Pia hawali kutokana na maagizo ya wataalamu wa afya ya Soka.
 
Ni Kweli.
Wachezaji wetu wana tatizo la Lishe Duni.
Mishahara wanayopata haikidhi kupata chakula kinacho kidhi kwa mchezaji wa Soka.
Pia hawali kutokana na maagizo ya wataalamu wa afya ya Soka.
Chips oyeeeeee....
 
Spika wa bunge kwa hili umekosea sana. Huwezi kuwa kiongozi wa Serikali ukatumia kodi yetu vibaya kwamba unaenda kuwapa support wachezaji, matokeo yake wewe unaanza kuwaponda. Eti tumefungwa kwa sababu hatuli.

Hivi ni kweli hatuli au ni maumbo yetu? Hivi kessy hata akila usiku na mchana kama mchwa atarefuka ili apambane na Senegal.

Jambo la pili unasema tumefungwa kwa sababu ya viongozi wabaya wa mpira. Pale viongozi ulitaka wafanyeje? Au ulitaka wamwingile kocha majukumu yake kama unavyofanya mara zote.

Nimekusikia tena unasema kuna kiongozi mdogo hajitambui bila shaka huyu ni makonda kutokana na alichomwambia Rais.

Makonda yuko sahihi ndiyo maana umeona watanzania hawawalalamikii wachezaji bali kocha maaana yeye alipaswa kufanya zaidi ya hicho alichofanya kama fiziki hiyo ni kazi ya kocha.

Mheshimiwa tambua wewe ni kiongozi hupaswi kuwa na maoni binafsi kwa namna yoyote ile unapoongea na public.

Maoni tuachie sisi wadau wengine. Inabidi kama kiongozi ujitafakali. Naona utaanza kupambana na huyo kiongozi kijana kwa sababu amekuchallange na kukonyesha wazi ulichokosea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…