Ndugu wanataka tuuze nyumba yenye Hati ya jina langu baada ya mzee kufariki

Ndugu wanataka tuuze nyumba yenye Hati ya jina langu baada ya mzee kufariki

MR KUO

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2016
Posts
2,678
Reaction score
3,818
Ndugu wadau

Poleni na majukumu ya ujenzi wa Taifa.

Naomba niende moja kwa moja kwenye shida yangu, tarehe 24/2/2020 Kama familia tulipata msiba wa kuondokewa na MZEE wetu aliyetangulia mbele za haki kwa kifo Cha ghalfa.

Sasa kilichonifanya nije hapa mbele yenu kuomba msaada wa ushauri ni kwamba, enzi za mzee alifanikiwa kuwa na watoto nane na wote wa tumbo moja kwa maana ya mama mmoja, huku akiwa na mali ambazo ni nyumba nne, tatu akiwa kaandika majina yake kamili huku nyingine moja akaandika hati ya jina langu kwa sababu Mimi ndo mzaliwa wa mwisho.

Baada ya mzee kufariki na hakuacha wosia wowote maana ilikuwa ghafla ndo wameibuka kaka zangu wakubwa wawili wanataka nyumba yenye hati yangu iuzwe pesa igawanywe pasu kwa pasu ili waweze kufanya Mambo mengine ikiwemo kumalizia ujenzi wa nyumba zao ambao umesimama. nimejaribu kumuuliza mama ili nijue hii imekaaje kaishia kunipa majibu ya kawaida Sana kwamba (yeye hana mamlaka na mali alizoacha mzee maana ni zenu watoto mkiamua kuuza mali yoyote ni sawa).

Wakuu kilichonileta hapa ni kutaka kujua hii imekaaje kwa mujibu wa sheria ili nijue mapema isije ikawa shida huko siku za mbele kutuhumiana dhuluma au kujaribu kuvuruga mahusiano ya familia kwa Jambo la kawaida.
.....................

Kwamba nyumba ina hati ya jina langu..

Ndugu wanataka tuuze nyumba yenye hati ya jina langu badala ya hizi nyingine zenye majina ya baba.

"Mama anasema hana mamlaka na mali alizoacha mzee maana ni za watoto, wakiamua kuuza sawa wakiamua kuacha sawa".

Hapa naona kama kakwepa kujibu swali langu la msingi nililotaka kujua kama kuandikwa kwenye hati ya nyumba ina maana nyumba ni yangu ama sio yangu.


Shukrani
 
Hapo tu kutaka hiyo nyumba iwe yako lazima ukubali umetangaza vita na ndugu zako na ugomvi wa mali inabdi ujiandae kwa mbinu zote kama sio sheria bhasi hata kauchawi utatupiwa mzee achana na kitu inaitwa mali za urithi yani hiyo ni vita..!
 
Vita ya mali haijawahi kuacha mtu salama, hapo apatikane mzee mwenye busara tu, kwakua nyinyi n ndugu, mko nane nyumba ziko 4, gawaneni wawili wawili, na umiliki mbadilishe
ooh
 
hayo mambo ya mirathi nikiyasoma naona kichwa kinaniuma.
yanatesa sana.

Hapo tayari ni uadui,visa,na visasi. Ambao hawajawahi kupitia hilo tatizo hawawezi kukuelewa.
hapo mwisho wa siku mtapelekana mahakamani.

Wengine wataenda kwa waganga ili washinde kesi ili mradi ni tafrani
 
Hapo kuna maswali ya kujiuliza

1. Japo marehemu baba anajua ana watoto 8 na ana nyumba 4, kwanini aliamua kukupa wewe nyumba yako kwa kuandikisha Hati ya nyumba yenye jina lako? Hili swali mama anaweza kulijibu, wazee wa karibu na mzee wanaweza kulijibu, kaka/dada wa mzee wanaweza kulijibu, babu na bibi zako wanaweza kulijibu, hata na wewe kutokana na mazingira mliyoishi hapo nyumbani unaweza kulijibu

Kwa uelewa wangu kuna Mila za baadhi ya makabila (kama watu wa kaskazini) , mtoto wa mwisho ndiye anayeachiwa mji wa mzee. Hivyo kama baba ameamua kukuachia nyumba kwa jina lako ina maana hapo ni NYUMBANI, sasa nyumbani hapawezi wala hapatakiwi kuuzwa.

2. Je baba alikuwa anamiliki nyumba tu, je mgawanyo wa mali zake nyingine upoje, je hao watoto wengine hawajapata zaidi mgawo wa mali nyingine ukilinganisha na wewe? Inawezekana kuna viwanja, mashamba n.k. yana Hati zenye majina ya ndugu zako

Usikurupuke kukubali kuuza kabla hujapata majibu ya maswali hayo
 
Nisivyopenda migogoro ya mali na familia ningeuza tu, maana hata kama umeandikwa wewe ila nao ni baba yao.

Uzeni ili udumishe mahusiano mazuri na wenzie
 
nashukuru Sana kwa mwongozo. Kama nilivyotangulia kusema kuwa mzee alikufa ghafla.

kuhusu Mali nyingine ninazojua nje ya nyumba hizo nne Ni pikipiki Moja na bajaji Moja tu
Hapo kuna maswali ya kujiuliza

1. Japo marehemu baba anajua ana watoto 8 na ana nyumba 4, kwanini aliamua kukupa wewe nyumba yako kwa kuandikisha Hati ya nyumba yenye jina lako? Hili swali mama anaweza kulijibu, wazee wa karibu na mzee wanaweza kulijibu, kaka/dada wa mzee wanaweza kulijibu, babu na bibi zako wanaweza kulijibu, hata na wewe kutokana na mazingira mliyoishi hapo nyumbani unaweza kulijibu...
 
Hapo tu kutaka hiyo nyumba Iwe yako lazima UKUBALI UMETANGAZA VITA NA NDUGU ZAKO na ugomvi wa mali inabdi ujiandae kwa mbinu zote kama sio sheria bhasi hata kauchawi utatupiwa mzee achana na kitu inaitwa mali za urithi yani hiyo ni vita..!
ooh Mungu anisaidie kwa kweli daaaah.
 
Mzee alikuwa mjanja aliiweka hiyo nyumba katika jina lako kwa vile wewe ni wa mwisho ili umtunze mama yenu. Kitinda mimba kazi yake kuishi na kumtunza mama yake Uzeeni. Hiyo ni ya kwako personal usiiuze.

Asante Sana Sasa wanaibuka Hawa mabro wanataka iuzwe tugawane hela. mama nae Kama hajui kitu ndo nabaki njiapanda mzima mzima.
 
Mzee aliona mbali hadi akakuachia wewe nyumba, usimlaumu mama kwanza bado yupo kwenye majonzi pili ana maumivu kuona hao ndugu zako wameanza kutolea macho mali mapema,

Kama hati unayo waambie huuzi nyumba hiyo ni kumbukumbu ya jasho la baba yenu, wao wakitaka wauze zingine.

Jiandae kwa vita kali lakini usikate tamaa, simama imara pia muangalie mama kwa upendo.

Msaada wa kisheria utahitajika endapo watafanya ukorofi.

Boost your Immune System to fight a Covid-19.
 
Dah nashukuru Mungu sijawahi kuiwazia nyumba yetu japo mie ndo last born na kwa mila zetu mtoto wa mwisho ndie mrithi wa mjengo.

Kwa sasa mshua anauboresha mjengo kila uchao nawaza tu zogo lake kati ya first borne brother na mama wa kambo litakuwaje japo sidhani kama ntashiriki kugombania. Nataka nijenge kwangu tu ili ile nyumba niipangishe huko mbeleni.
 
Nisivyopenda migogoro ya mali na famili ningeuza tu, maana hata kama umeandikwa wewe ila nao ni baba yao.

Uzeni ili udumishe mahusiano mazuri na wenzie
lakini swali la kujiuliza kwa Nini wapate mawazo ya kuuza hii yenye jina langu?.

nyingine hawazioni?

hakuna Nia ovu kweli hapa?
 
Mzee aliona mbali hadi akakuachia wewe nyumba, usimlaumu mama kwanza bado yupo kwenye majonzi pili ana maumivu kuona hao ndugu zako wameanza kutolea macho mali mapema,

Kama hati unayo waambie huuzi nyumba hiyo ni kumbukumbu ya jasho la baba yenu, wao wakitaka wauze zingine...
Asante Sana kwa ushauri mzuri wenye mwanga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom