Ndugu wanataka tuuze nyumba yenye Hati ya jina langu baada ya mzee kufariki

Ndugu wanataka tuuze nyumba yenye Hati ya jina langu baada ya mzee kufariki

Hapo kuna maswali ya kujiuliza

1. Japo marehemu baba anajua ana watoto 8 na ana nyumba 4, kwanini aliamua kukupa wewe nyumba yako kwa kuandikisha Hati ya nyumba yenye jina lako? Hili swali mama anaweza kulijibu, wazee wa karibu na mzee wanaweza kulijibu, kaka/dada wa mzee wanaweza kulijibu, babu na bibi zako wanaweza kulijibu, hata na wewe kutokana na mazingira mliyoishi hapo nyumbani unaweza kulijibu

Kwa uelewa wangu kuna Mila za baadhi ya makabila (kama watu wa kaskazini) , mtoto wa mwisho ndiye anayeachiwa mji wa mzee. Hivyo kama baba ameamua kukuachia nyumba kwa jina lako ina maana hapo ni NYUMBANI, sasa nyumbani hapawezi wala hapatakiwi kuuzwa...
[emoji115] [emoji115] fata huu wa kwanza
 
Okay

Basi hizo mali nyingine kama hazijaainishwa mmiliki zitafuata utaratibu wa kawaida wa kijamii na kisheria
nashukuru Sana kwa mwongozo. Kama nilivyotangulia kusema kuwa mzee alikufa ghafla.

kuhusu Mali nyingine ninazojua nje ya nyumba hizo nne Ni pikipiki Moja na bajaji Moja tu

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yenye jina lako ni ya kwako mwenyewe ndio mana wanataka muuze ili zibaki za mgao ... Nyumba zilizobaki ni za mama ako kama wote mumevuka miaka 18 ... mkitaka kuuza lazima mgawane zenye majina ya Baba ... yenye jina lako ni ya kwako ( sijui sheria za Mirathi just common senses )
 
Kama shida kuuza nyumba na kugawana hela kwanini wauze hiyo yenye hati ya jina lako waulize hivyo uskilize majibu,ila ningekuwa mimi siuzi hata wafanyaje.hawana nia nzur hao na suo watu wazur kaa nao kwa makini
 
Nisivyopenda migogoro ya mali na famili ningeuza tu, maana hata kama umeandikwa wewe ila nao ni baba yao.

Uzeni ili udumishe mahusiano mazuri na wenzie

Nyumba zote zikiuzwa.. yeye na mama yake wataishi wapi?
 
Ukishaona watu wanapigania Mali za urithi wakati mama yao bado yupo ujue hapo ipo shida kubwa sana. Mbaya zaidi mama yako ameshindwa kuwa upande wako.

Babu yangu alipofariki hakudema kitu chochote kuhusu mgawanyo wa Mali
Baada ya mazishi taratibi zikifanyika na mjomba wangu ambae ni kitinda mimba aliwekwa rasmi kuksimamia mirathi. Kufupisha story hivi karibuni alibadikisha nyumba moja na kuiweka kwenye majina yake.

Baada ya kufanya hivyo dada zake na kaka wakaanza kulalamika chini chini. Ni mkubwa alinisimulia lakini akaniomba nisiulize kuhusu hilo swali. Kwa sababu mimi ni mjukuu kipenzi wa bibi siku moja nikamuuliza. Akasema yeye ndio msimamizi wa urithi hivyo lazima nyumba iwe kny majina yake japokuwa haimaanishi ni ya kwake peke yake.

Nadhani utakuwa umenielewa.

Mwisho niseme inaonekana huna mahusiano mazuri na mama yako ndio maana anashindwa kuingilia hilo suala either ameshakuona inaanza u mimi.

God save us
 
Muhtasari wa mawazo ya kaka zako kwenye hizo nyumba 3 zilizosalia upoje?
 
Yenye jina lako ni ya kwako mwenyewe ndio mana wanataka muuze ili zibaki za mgao ... Nyumba zilizobaki ni za mama ako kama wote mumevuka miaka 18 ... mkitaka kuuza lazima mgawane zenye majina ya Baba ... yenye jina lako ni ya kwako ( sijui sheria za Mirathi just common senses )
sawa sawa. Sasa Hawa wanaingiliwa na mapepo na kutaka kuvunja maamuzi ya mzee.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama hakuna wosia kuandikwa jina lako haina maana kuwa ndo umekabidhiwa mali hiyo.

Wala kuwa wa mwisho haina maana wewe kuwa mrithi wa mali za baba labda kama alisema hivyo yeye mwenyewe. Mara nyingi baadhi ya makabila, baba akifariki, mtoto wa kwanza ndiye mmiliki, lkn kwa kuwa wengi tayari wanakuwa wanamaisha yao, mtoto wa mwisho ndo hubaki nyumbani kama mwangalizi wa mali za nyumbani lakini siyo mmiliki wa mali hizo.

Mnatakiwa mkae kikao cha kuamua kuhusu mali za marehem, mji ambao ndipo nyumbani ibaki kuwa nyumbani na wewe utakaa hapo lkn haina maana ni kwako, ni kwenu nyote. Maana yake ni kuwa yeyote maisha yakimshinda, atarudi kwao ambapo ni hapo unapoishi wewe kama mwangalizi.

Mwisho pambana kuwatafutia wanao urithi usiwaze kuwarithisha jasho la babu yao


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukishaona watu wanapigania Mali za urithi wakati mama yao bado yupo ujue hapo ipo shida kubwa sana. Mbaya zaidi mama yako ameshindwa kuwa upande wako.

Babu yangu alipofariki hakudema kitu chochote kuhusu mgawanyo wa Mali
Baada ya mazishi taratibi zikifanyika na mjomba wangu ambae ni kitinda mimba aliwekwa rasmi kuksimamia mirathi. Kufupisha story hivi karibuni alibadikisha nyumba moja na kuiweka kwenye majina yake. Baada ya kufanya hivyo dada zake na kaka wakaanza kulalamika chini chini. Ni mkubwa alinisimulia lakini akaniomba nisiulize kuhusu hilo swali...
oh God save me...[emoji26][emoji26][emoji26][emoji26]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama hakuna wosia kuandikwa jina lako haina maana kuwa ndo umekabidhiwa mali hiyo.

Wala kuwa wa mwisho haina maana wewe kuwa mrithi wa mali za baba labda kama alisema hivyo yeye mwenyewe. Mara nyingi baadhi ya makabila, baba akifariki, mtoto wa kwanza ndiye mmiliki, lkn kwa kuwa wengi tayari wanakuwa wanamaisha yao, mtoto wa mwisho ndo hubaki nyumbani kama mwangalizi wa mali za nyumbani lakini siyo mmiliki wa mali hizo...
Asante Sanaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama hakuna wosia kuandikwa jina lako haina maana kuwa ndo umekabidhiwa mali hiyo.

Wala kuwa wa mwisho haina maana wewe kuwa mrithi wa mali za baba labda kama alisema hivyo yeye mwenyewe. Mara nyingi baadhi ya makabila, baba akifariki, mtoto wa kwanza ndiye mmiliki, lkn kwa kuwa wengi tayari wanakuwa wanamaisha yao, mtoto wa mwisho ndo hubaki nyumbani kama mwangalizi wa mali za nyumbani lakini siyo mmiliki wa mali hizo...
Hati ya nyumba ikiwa na jina lako maana yake nyumba ni ya kwako hata baba ake angekuwepo hai na hati ya nyumba amemwandika mtu mwingine hiyo nyumba ingekua ya huyo mtu maana yake ni kwamba hata baba ake angekuwepo nyumba bado ya mwanae mana ndio aliyemuandika kwenye hati.
 
Hiyo ndo akili ya kiumeni
Dah nashukuru mungu sijawahi kuiwazia nyumba yetu japo mie ndo last borne na kwa mila zetu mtoto wa mwisho ndie mrithi wa mjengo.

Kwa sasa mshua anauboresha mjengo kila uchao nawaza tu zogo lake kati ya first borne brother na mama wa kambo litakuwaje japo sidhani kama ntashiriki kugombania. Nataka nijenge kwangu tu ili ile nyumba niipangishe huko mbeleni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom