Ndugu watanganyika ninaombeni mumsamehe Luhaga Mpina kwa kupima samaki kwa rula, kila mwanadamu ana mapungufu yake

Ndugu watanganyika ninaombeni mumsamehe Luhaga Mpina kwa kupima samaki kwa rula, kila mwanadamu ana mapungufu yake

Ndugu zangu watanganyika,
Tumebaki yatima tusio na malezi kwenye hii nyika,
Tumetelekezwa kama bendi ýa Lesi wanyika, tumesahaulika,

Nakuja kwenu kwa unyenyekevu mwingi kumuombea msamaha Luhaga mpina mbunge wa kisesa kwenu. Hakika japo hajakili alilo lifanya lilikuwa na mapungufu makubwa kwetu watanganyika. Lakini ndiye mtu pekee anayeweza kutusemea kwa sasa. Ni mtu pekee aliye hatarisha maisha yake kwaajili yetu watanganyika.

Naombeni tumtie moyo katika safari yake. Isiishie njiani kama rafiki yake Deo filikunjombe. Tupate mawasiliano yake na tumtie nguvu wakati wote. Na muhimu kumshauri kwakuwa ni binadamu hawezi kuwa na ufanisi wa asilimia miamoja.
Nawaombeni sana mumsamehe. Waungwana husamehe. Wana CCM kama mimi wenye misimamo mikali tumsamehe, wana CHADEMA mumsamehe

Naombeni kuwasilisha.View attachment 2666001
View attachment 2666002
Haya yalishapita mkuu....
 

Attachments

  • 1640604801665_1.jpg
    1640604801665_1.jpg
    94.9 KB · Views: 2
Back
Top Bottom