Ndugu yangu amenipa sharti la kuacha kazi ya kuajiriwa ili anipe mtaji wa Tshs 200M nianze shughuli yangu mwenyewe lakini sijui nifanye shughuli gani!

Hio ndio siri ya biashara mkuu inataka ujitoe 100% haitakiwi uwe na options, na huyo jamaa yako anajua vizur biashara ..kinachohitajika wew ni uchague ARE U YOU IN OR OUT biashara haihitaji mguu ndan mguu nje inakuhitaji muda wote hadi pale itakapotengemaa
Ushauri wangu wekeza ktk field ambazo znaendana na hio kaz ulioajiriwa nayo
 
Nadhani hapa unasema nichague kitu kimojawao, maana hospitali kwa mfano, hata Tshs 200m haitoshi.
 
Hicho kihunzi kimoja. Cha pili, niingie kwenye shughuli gani? Kuna mtu kaniambia Tshs 200m ni hela ndogo sana!

Mie mawazo yangu hao ilikuwa niingie kwenye Coaster, nianze na mbili.
Biashara ya Costa ni hasara tupu utafilisika, maana cost ya matengenezo sio ndogo, hafu inabidi biashara uanze mdogo mdogo huku ukipata uzoefu bila hivo utafilisika
 
Nimemuelewa sana. Na hapo kwenye kuwa IN or OUT ndio nimefikiria sana, nikaona ngoja nije huku kwa jamaa zangu wa JF nisikie maoni yao. So far naona wengi wanazidi kunichanganya 🤣

Ila kitu kimoja ninazidi kuelewa, kwamba tupo wengi sana tukipewa mtaji Tshs 200m hatutajua tufanye nini!
 
Nadhani ni 2.5 mil/month (yaani 15% interest rate).
Kama hii ni kweli that is the way to go, maana nikipata Tshs 2.5m kwa mwezi inazidi sana mshahara wangu wa Tshs 1.5m kwa mwezi. Lakini mbona naona kama it is too good to be true?

Ni kweli nikiweka Tshs 200m nitapewa Tshs 2.5 kwa mwezi? Kama ni kweli mie nitaendelea kuchukua 1.5m kwa mwezi na hiyo 1m nitairudisha kama capital gain ili kuongeza deposit

Wapi huko nitapewa 2.5 kwa mwezi?
 
Mkuu, Watanzania ambao waliukana uraia wanapata taabu sana kuwekeza nchini. Naa kuna kitu kimoja nimegundua, kwamba taasisi za Tanzania huwa haziamini kama mtu mwenye ngozi nyeusi ni muwekezaji wa kweli. Taasisi zetu, kuanzia TRA, wana mind set kwamba muwekezaji genuine ni mzungu tu, wengine wote ni matapeli tu. Watafanya facilitation kwa mzungu, lakini kwa mtu mweusi utakwamishwa katika kila hatua!
 
Kaongee na benki ama certified broker wa kununua bond za serikali. Faida kwa kawaida huwa inalipwa kila baada ya miezi 6 (2.5milx6months). Lakini sidhani kama huyo ndugu yako ataichukulia kuwa hii ni biashara. Hii kwa kawaida wanafanya watu wenye hela nyingi. Ni njia ya kutunza pesa ambazo hazina kazi ya kufanyia huku ukipata ka-faida kiasi.
 
Weka bank,nakuhaid utakula pesa umelala

Kwenye mil 10-20 hukos laki 3 kila mwez

Kwahyo hyo 200 mil hukos mil 3 kila mwez
Hii point ya Mil 2.5-3.0m kila mwezi kwa kuweka Tshs 200m ndio the best point nimeiona, with minimum risk. Nataka niifuatilie, na kama ni kweli basi hata kesho naacha kazi
 
Chukua 200m mia ziweke UTT zinazaa 14m per yr ambayo ni sawa na mshara wako na mia zinazobaki fanyia biashara mbali mbali kadri utakavyoweza ila mazao ndo iwe namba moja
 
This is serious, nitaifuatilia. Yeye hana tatizo na nibazifanyia nini, anachotaka ni kunipa fursa ya kuoneza kipato n kuondokana na kuajiriwa. So kama kweeli I can make an average of 2.5m kwa Tshs 200m kwa deposits za Benki, I am in for it. Kumbuka my salary is 1.5m, so this is a win option. Bado ninakuwa na capital gains nitakapokuwa naondoa 1.5m equivalent ya mshahara wangu wa sasa
 
Achana na hiyo ela fanya kazi kidogo kidogo huku ukilipia kodi na mafao yako, fedha za ngama hizo hazina garantee
 
Kama ni hivyo, hakuna haja ya kuacha kazi (sharti ambalo umepewa na sponsor). Kama mil 200 itakuwa kwenye bond za serikali na kuzaa 2.5 kila mwezi, kwa nini uache kazi sasa? Ili uwe unatizama TV nyumbani?
 
Mimi kabla sijakushauri uache au usiache kazi nataka kujua UMRI wako kwanza, kama ni late 40's ninashawishika kukwambia USIACHE kazi, upo kwenye umri HATARISHI, unakaribia kuanza kulipwa kikokotoo na kwa hiyo basic (sijui ni gross pay ) ya 1.5M ukistaafu utakua unalipwa vizuri tu na NSSF but kama upo kwenye 30's you have bright future with those 200M. Nijibie swali hilo kwanza ndio tuendelee.
 
Achana na hiyo ela fanya kazi kidogo kidogo huku ukilipia kodi na mafao yako, fedha za ngama hizo hazina garantee
Mkuu, hivi umeffikiria kwamba naweza kacha kazi, nikachukua hiyo hela, nisianye chochote, na nikawa na haliyangu ile ile y 1.5m kwa mwezi kwa muda wa miaka 11? Sasa utasemaje haina guarantee wakati entry level ya kuacha kazi na kuchukua hiyo hela na kuamua kula na kulala ni miaka 11? Hujafikiria sana ushauri unaonipa
 
Hicho kihunzi kimoja. Cha pili, niingie kwenye shughuli gani? Kuna mtu kaniambia Tshs 200m ni hela ndogo sana!

Mie mawazo yangu hao ilikuwa niingie kwenye Coaster, nianze na mbili.
Ni hela ndogo sana !!! Yeye anatengeneza sh ngapi kwa siku?
1.5 yako kwa nwaka ndio una milioni 18 kukusanya milioni 200 mpaka ufanye kazi miaka 15 tena bila kuitumia.
Acha ujinga. Watu wengi wana mitaji ya milioni 5, 10 ,20 , na 100.
Wenye milioni 200 ni wa kuhesabu kwenye wilaya zetu.
Hiki ni kipimo cha wewe geaduate ambacho tangu uanze shule mpaka upate master hujawahi ulizwa swali gumu kama hilo.
Are you educated or not yet? Jibu lako ndio litatoa litajibu umeelimika kiwango gani.
Nilichogundua humu wengi wetu hatujui what do we want, tupo tupo tu ndio maana kuna majibu ya ajabu ajabu?
 
Milioni 200 unapata trekta 3mpaka 4 mpya kabisa.
Think of importing.
Think of exporting.
Therecare milions of fuc%&ing paying ideas! Think about them and take risk.
Tafuta cilonsultant,au mentor umlipe akupe good business idea and good business plan then take risk.
 
Wewe jamaa sijui hujui kiswahili, kaambiwa achague kimoja tu.
Mshauri jambo moja tu aaache kazi au aziache milioni 200. Mwenye hela yake kesha toa masharti .
 
Hapa ndo Tanzania bro
Mtengenezee fake papers..

Akija unachuka likizo unakaa kwny ile biashara ndogo uloanzisha

Mfano mini supermarket...
Wenye uzoefu watasema
Wewe unaakili kumzidi mtu alie ulaya ? Unachokiwaza wewe yeye yuko mile 100 mbele.
Je akimwita huko ulaya akae miezi 5 hivi huoni utapeli wake utajulikana.
Yani mtu anakupa mill 200 halafu unawaza kumfanyia utapeli hujui kuwa utapoteza.
 
Mtaji wa 200m ni mkubwa sana kama akili yako imetulia na una vision ya nini unataka kufanya.Lakini pia uwe committed,serious and strong ndani ya miaka 3-5 unabreak even mtaji wako unarudi na kuanza kupata faida.Ndio maana baadhi ya wachangiaji hapa wameuliza umri wako,elimu au uzoefu kidogo kwenye biashara,umeoa/umeolewa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…