Ndugu yangu amenipa sharti la kuacha kazi ya kuajiriwa ili anipe mtaji wa Tshs 200M nianze shughuli yangu mwenyewe lakini sijui nifanye shughuli gani!

Kama siyo daktari, nurse, mwalimu ama injinia wala asijaribu. Siyo rahisi hivyo. Marafiki zangu ambao ni madaktari walijaribu kuanzisha hospitali, wakashindwa.
ujenge chuo cha kufundisha nursing / medical assistants;

ujenge shule .a. level

ujenge hospital, private

Uwe na mtu wa kufuatilia vibali

Unless otherwise ... ukandarasi
 
Safi. Nadhani ningekuwa yeye ningekuuliza hiyo biashara ni biashara gani. Nadhani hili pia ndilo swali lake lake la msingi.

Hapo hakuna jibu la moja kwa moja mkuu. Kuna vitu vingi sana vya kuzingatia. Eneo alilopo, muda wake kwa sasa, uzoefu hata kidogo tu alionao, ubunifu wake na uelewa wa ujasiriamali.
Kuna wengine kama sie ukituweka kwenye biashara ni kama kumtoa samaki majini ukampeleka nchi kavu.
 
Huyu mtu ni muoga wa biashara
Like many employees
Msimuingize mkenge
Comments nyingi ni zenye kumsaidia na sio kumuingiza mkenge na in the end atachagua...but kumfundisha wizi, uongo-uongo, utapeli ili afanikiwe si sawa na ni kumuangamiza..trust ni kitu muhimu na ndio maana ndugu yake amekuwa open kwake.

Vijana tuache tamaa ya kupeana mbinu za shortcuts, wizi, uongo, ujanja-ujanja tukifikiri ndio tutapata mafanikio ya kudumu. Ndio maana tatizo la ajira tz ni kubwa kwa vijana kuwa na mawazo ya kufanikiwa kwa njia zisizo za halali hivyo kutoaminika kwenye kila fursa.
 
Kama hauko comfortable kuhusu kuacha kazi, chukuwa leave without pay ya miaka 2 hivi. Ktk miaka hiyo utaona mwelekeo na kama hali itaruhusu kuacha kazi basi utaacha. Na hiyo leave without pay usimfiche huyo ndugu yako.
 
Comrade!
Nimesoma uzi wako kwa makini na nimepitia commments zote.

Nimegundua mambo matatu (3)

1. Wewe ni mtu makini ( nimesoma comments zako)
2.Anayetaka kukupa pesa ni mtu makini sana na ameshakupima akaona kuna kitu ndani yako (Anataka aki push kibadilishe maisha yako)
3.Ushauri wa walioajiriwa na hawajawahi kufanya biashara kama wewe na ushauri wa wafanyabiashara "waliofanikiwa" una tofauti kubwa sana.

Ushauri wangu:
1.Usijaribu hata kwa bahati mbaya kumdanya huyo ndugu yako kwamba umecha kazi.
2.Usiombe zaidi ushauri kwa wafanyakazi wenzako ( tafuta watu nje ya mfumo wa kazi yako)
3. Muombe ( Ndugu yako) kabla ya fedha akupe muda atleast miezi mitatu kama unaweza kuchukua likizo bila malipo halafu
kabla ya kuomba ushauri wowote kwa yetote jifungie mahali tulivu ujiulize..

"hivi mimi ninaweza kufanya nini"

pambana uhakikishe unapata jibu la hilo swali wewe mwenyewe, ukishapata kile uwezacho tafuta mtu anayekifanya umwombe akusaidie uzoefu hata kwa kujitolea kufanya kazi zake bila malipo. Tafuta uzoefu kwa nguvu zote halafu anza kwa fedha zako hata kama ni milioni 1
Ukishaona changamoto, fursa, raha na karaha za hiyo kazi yako na kuzipatia ufumbuzi ndipo uache kazi na umwombe ndugu yako akupe hizo fedha.

Note;
Kwenye biashara mtaji si fedha pekee
Mtaji ni
1.Uaminifu
2.Ujuzi
3.Mtandao wa biashara husika
4.Fedha (ni ya mwisho)

Kosa wanalofanya watu wengi ni kuweka fedha mwanzo kabla ya vitu hivyo 3.
Usifanye kosa hilo.

All the best mkuu.!!







Sent from my SM-M115F using JamiiForums mobile app
 
Kwanza umeaniriwa binafsi au seeikali?
Na WEWE UMEAFIKI HILO WAZO
 
Mm binafsi niko tayari kuacha kazi kwa 100m tu.
Ktk hiyo 100m nawekeza 60m tu.
40m inasubiri.
Kikubwa ntahama Dsm na kuhamia Morogoro.
 
Ukitaka mjasiriamali uwe tayari kufeli

Sijui kwanini watu wanaogopa kufeli,
Ulikuja uchi utarudi uchi Fanya kitu moyo unapenda.

Hata upate training gani ,ushauri gani ,upate mentor bado failure is inevitable part of success.

Kufeli sio laana wala mkosi ni part ya success ambayo haikwepeki.

Kama unaogopa kufeli usifanye biashara.

"If you need motivation ,don't be an entrepreneur"-Elon Musk
 
Acha kazi tafuta location nzuri uwe wakala wa NMB au CRDB
 
Una muda gani kazini mkuu?
 
Hongera mkuu kwa kupata mtu wa kukusaidia kwa namna hiyo, japo unayo ajira tayari.

Je, ajira yako ni permanent? Yaani upo kwa mkataba mfupi au ni serikali ambapo una uhakika wa kustaafu (60yrs)?

200ml ni nyingi kabla hujaishika, Ila ukiikamata inaweza kuonekana ndogo sana(japo wengine hata 50ml hatujawahi[emoji23]), hasa kama huna strategy za nini unataka kufanya. Ninayo mifano ya mtu kakamata 400mil 2019, leo hii anaomba gari na mafuta ili aende mishe zake. So kuwa makini sana.

1. Wekeza kwenye teknolojia.
2. Wekeza kwenye hardware materials.
3. Wekeza kwenye automobile parts
Fanya research hapo uone wapi unaweza kujiweka.

Usiingize pesa yote kwenye kapu moja;

30% fungua biashara unayoamini na kuifanyia utafiti wa kina.
50% weka bond kama huko UTT, tafuta financial experts wakueleze hayo mambo.
20% iweke just in case.

Dedicate mda wako kwenye biashara, usiogope kujiajiri.
 
Alijisemea wa ukae akili za kuambiwa changanya na zako, Kuna washiliki wa bigbrother walishinda mipesa wapo wapi? Mmoja juz alikuja kwenye msiba wa ndugu yake, hata Mimi mchovu naafazari.
Kweli bana hela unaweza kupewa hata 500M lakin kama huna mipango thabiti unaweza kuja kuishia kua mchekeshaji mitandaoni
 
Mkuu, sijawahi kufanya hata biashara ya juice au ice cream. Toka nimalize chuo mie mtu wa kuajiriwa tu!
Hiyo 200m kama huna biashara ya kuendeleza unaenda kuanguka in just 1 year na utaikumbuka kazi yako ulioacha. Biashara unayoenda kuanzisha inaasilimia 75 ya kufeli kwa sababu nyingi sana ikiwemo uzoefu wa mtaani, aina ya biashara na kupump hela nyingi sehemu isipohitajika. Muulize Idris Sultan na ile 700m ilipoishia. Kimsingi mtaani ni tofauti sana hata kama unamtaji. Asilimia 25 ya kufanikiwa usiipuuze ni kubwa pia na ukitoboa umetoboa.
Omba likizo bila malipo umwambie umeshaacha kazi kisha ujaribu biashara ikikushinda unarudi.
Jaribu bahati yako na usiogope kufeli hasa kama upo below 40 yrs. Nasisitiza usiogope, ila 200m sio nyingi kama unavyoweza iona.

Retire young,retire rich
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…