mjegejo
Member
- Jun 30, 2019
- 84
- 114
Niko 'frustrated' naomba mniwie radhi kama uandishi na mpangilio wa hoja yangu utashindwa kueleweka kwenu.
Ni hivi,
Mimi pamoja na kaka yangu mkubwa tumbo moja na baba tulikuwa tukiishi vizuri lakini uhusiano wetu ulianza kuingia doa baada ya mzee wetu kufariki.
Baada ya mzee kufariki kilikaliwa kikao cha ukoo na agenda kubwa ilikuwa ni kugawa mali za urithi ambapo katika kikao hicho walengwa wakubwa nilikiwa mimi pamoja na huyo kaka yangu.
Kwakuwa kifo cha mzee wetu kilitokea ghafla na hakuacha wosia wowote wa maneno wala maandishi, ukoo uliadhimia kugawa mali za urithi kwa utaratibu wa kimila. Ambapo iliamuliwa kuwa, kwakuwa sisi ni wa matumbo ili kuepuka mgogoro wa baade nyumba tuliyokuwa tukiishi na mzee iuzwe na pesa itakayopatikana tugawane kwa usawa. Nje na nyumba hiyo pia mzee aliacha viwanja viwili vya wazi ambapo tuligawiwa kila mmoja cha kwake.
Baada ya mgawanyo huo wa mali kaka yangu alienda kuishi kwao na mama yake mzazi na mimi nilienda kuishi na mama yangu kwenye nyumba ya kupanga. Baadae nilifanikiwa kujenga nyumba kwenye kiwanja changu cha urithi nilichokabidhiwa ambapo tunaishi hadi sasa.
Shida iliyojitokeza ni kwamba baada ya ule mgao wa viwanja kumalizika huyu kaka yangu yeye alimaliza akauza kiwanja chake na kwakuwa ni mtu wa 'tungi' pesa yote iliishia kusikojulikana na sasa ameanza kumendea kiwanja changu kwa madai kwamba ni cha kwetu wote na hiyo nyumba iliyomo ilijengwa na mzee. Katika madai yake anataka hicho kiwanja changu tukimiliki wote wawili au tukiuze alafu pesa tugawane.
Kufuatia sakata hilo nashindwa kabisa kumwelewa huyu kaka yangu. Hivyo basi nakuja kwenu wana jamvi kuomba msaada wa kimawazo na kisheria juu ya hatua nazopaswa kuchukua. Pia naomba kujua utaratibu wa kufuata ili niweze kutambulika/kumiliki kihalali ardhi ambayo haijapimwa.
Mawazo yenu ni muhimu wadau
Ni hivi,
Mimi pamoja na kaka yangu mkubwa tumbo moja na baba tulikuwa tukiishi vizuri lakini uhusiano wetu ulianza kuingia doa baada ya mzee wetu kufariki.
Baada ya mzee kufariki kilikaliwa kikao cha ukoo na agenda kubwa ilikuwa ni kugawa mali za urithi ambapo katika kikao hicho walengwa wakubwa nilikiwa mimi pamoja na huyo kaka yangu.
Kwakuwa kifo cha mzee wetu kilitokea ghafla na hakuacha wosia wowote wa maneno wala maandishi, ukoo uliadhimia kugawa mali za urithi kwa utaratibu wa kimila. Ambapo iliamuliwa kuwa, kwakuwa sisi ni wa matumbo ili kuepuka mgogoro wa baade nyumba tuliyokuwa tukiishi na mzee iuzwe na pesa itakayopatikana tugawane kwa usawa. Nje na nyumba hiyo pia mzee aliacha viwanja viwili vya wazi ambapo tuligawiwa kila mmoja cha kwake.
Baada ya mgawanyo huo wa mali kaka yangu alienda kuishi kwao na mama yake mzazi na mimi nilienda kuishi na mama yangu kwenye nyumba ya kupanga. Baadae nilifanikiwa kujenga nyumba kwenye kiwanja changu cha urithi nilichokabidhiwa ambapo tunaishi hadi sasa.
Shida iliyojitokeza ni kwamba baada ya ule mgao wa viwanja kumalizika huyu kaka yangu yeye alimaliza akauza kiwanja chake na kwakuwa ni mtu wa 'tungi' pesa yote iliishia kusikojulikana na sasa ameanza kumendea kiwanja changu kwa madai kwamba ni cha kwetu wote na hiyo nyumba iliyomo ilijengwa na mzee. Katika madai yake anataka hicho kiwanja changu tukimiliki wote wawili au tukiuze alafu pesa tugawane.
Kufuatia sakata hilo nashindwa kabisa kumwelewa huyu kaka yangu. Hivyo basi nakuja kwenu wana jamvi kuomba msaada wa kimawazo na kisheria juu ya hatua nazopaswa kuchukua. Pia naomba kujua utaratibu wa kufuata ili niweze kutambulika/kumiliki kihalali ardhi ambayo haijapimwa.
Mawazo yenu ni muhimu wadau