Ndumbaro Adai Katiba Mpya ni hitaji la Watanzania kwa sasa

Ndumbaro Adai Katiba Mpya ni hitaji la Watanzania kwa sasa

Tuanze na haya.
1. Tanzania iwe nchi moja kama jina lake. zanzibar kuwe mikoa kama ukerewe na mafia.
Ndugu zetu wa Gando Chakechake sitaki tuachane, la wapemba wa dar na Tanga watatangatanga!
2. Mali zote zilizopatikana wakati wa ccm kikiwa chama kimoja, na ziko mikonon mwa ccm tu leo, zirudi serkalini hasa viwanja, majengo na vitega uchumi vingine maana walichangia raia wote kwa tozo na makato mbalimbali.
3. Tanzania ishikirie msimamo wa kutokuwa ya kijamaa wala kibepari ili tuwe salama na uhuru wa kibiashara. Leo hii tungeshukua mafuta russia!
...samahan nimechanganya matamanio na hali halisi!
 
Hii ndio Taarifa inayozunguka mitandaoni kwa sasa kutoka Dodoma , ambapo Waziri wa Sheria na Katiba Dr Damas Ndumbaro amewaambiwa Wafanyakazi wa Wizara yake na Waandishi wa Habari kwamba Katiba mpya haikwepeki , kwa vile ndio hitaji la Watanzania kwa sasa .

Ameendelea kueleza kwamba mchakato wa Katiba hiyo tayari ushaiva na kwamba Isipokamilishwa Wananchi watashangaa .
,

Amedai vipaumbele vikubwa ni kwenye Sheria ya Uchaguzi wa serikali za mitaa , Uchaguzi Mkuu na Tume ya uchaguzi , na mimi naongezea utata mwingine ni ( madaraka ya Rais )
Watanzania gani wamemtuma awasemee. Ajisemee mwenyewe.
 
labda apite bila kupingwa kwenye chama chake.
Hapana, nimesema kwa vyote. Sikiliza: tukiwa na mfumo mpya na mzuri wa uongozi utakaopatikana kwa mwongozo wa katiba mpya, na uchaguzi wa wabunge ukiwa wa kidemokrasia na bunge liwe na balance nzuri ya vyama na wabunge wenye kuwajibika, nafasi ya urais itakuwa siyo ya kimungu mtu kama sasa.
 
MICHAKATO YA MAKATIBA YAANZE 2026,ILI IJE KUTUMIKA 2030. A RIGHT TIME.
N. B~Tuwe makini sana wapo maadui,waliojificha kwa ndani sana wenye VINYONGO NA VISASI wanadhani huu ndio utakuwa mlango wao!
Hakuna urahisi wowote mtakaoupata nyie mafisadi, 2026 kwa misingi gani? Katiba mpya ni sasa. 2025 apatikane kiongozi wa kuchaguliwa kwa dhati ya wanachi. Dezo na kuwekana hatutaki tena
 
CCM imeishiwa mbinu zote na bila kuondoka madarakani nchi haitabadilika. Hata hivyo niko tayari kuunga mkono kwa moyo wote iwapo vyama vyote vya siasa na wananchi kwa ujumla watakubaliana kuwa rais Samia apite bila kupingwa 2025, ila asimamie uandikaji wa katiba mpya kwa muda uliobakia (sasa mpaka 2025) na mwaka 2025 tuanze ukurasa mpya tukiongozwa na katiba mpya. I mean uchaguzi wa wabunge na uundwaji wa serikali ufanyike kwa mujibu wa katiba mpya ila Samia ahakikishiwe nafasi yake 2025 mpaka 2030.
Hakuna kupita bila kupingwa hapa. Urais wa kurithi na dezo ndio umebakiza miaka miwili tu. Never again
 
Uwepo utaratibu wenye usawa katika kuwapata viongozi dizaini ya wakuu wa mikoa wilaya wakurugenzi nk nk.

Sio mtu anaamka tu kutoka usingizini anamteuwa mpwa wake kua mkurugenzi sehemu fulani.

Hizi kazi wanatakiwa wawe wanaomba na kufanyiwa usaili kama zilivyo kazi nyingine

Mkiona inafaa iingizeni kwenye katiba kabisa.
 
CCM imeishiwa mbinu zote na bila kuondoka madarakani nchi haitabadilika. Hata hivyo niko tayari kuunga mkono kwa moyo wote iwapo vyama vyote vya siasa na wananchi kwa ujumla watakubaliana kuwa rais Samia apite bila kupingwa 2025, ila asimamie uandikaji wa katiba mpya kwa muda uliobakia (sasa mpaka 2025) na mwaka 2025 tuanze ukurasa mpya tukiongozwa na katiba mpya. I mean uchaguzi wa wabunge na uundwaji wa serikali ufanyike kwa mujibu wa katiba mpya ila Samia ahakikishiwe nafasi yake 2025 mpaka 2030.
Ni wewe mkuu, 'Macho...', au kunamwingine kachukua jina?

Nimesoma, lakini sijakuelewa usemacho!

Ngoja nipumzishe akili, halafu nirudi kukusoma vizuri, huenda nimechanganya mambo.
 
Uzi wako ule wa SUKUMA GANG umeukimbia mkuu, watu wanatema Nyongo kuhusu ushamba wenu wasukuma.
Mkuu DINHO , ukiuliza kitu nje ya mada iliyo mezani unaanza kwa kutaka radhi kwenda nje ya mada.

Ule uzi Je, tukemee udini, ukanda na ukabila au? Je, neno Sukuma Gang si neno la kibaguzi? Mnaonaje tukiungana kukemea ubaguzi wowote kwa jina lolote? sijaukimbia bali nimeepuka kuchangia chochote mule kuepuka kuparuana na watu ila ni kweli kabisa Wasukuma sisi ni washamba sana!, hilo halina ubishi, na ukikuta Msukuma ambaye sio mshamba ujue ameokolewa na moja ya mawili haya, ama ameoa makabila ya wajanja, hivyo kubadilishwa, ama amezaliwa mjini na kukulia mjini or both. Ila pamoja na ushamba wote wa Wasukuma, ndilo kabila tunaloongoza kwa kupenda, upendo na kuwa roho mzuri!, akitokea Msukuma mwenye roho mbaya, sisi Wasukuma wenyewe original lazima tujiulize huyu ni Msukuma wa wapi?, ndio maana nilipandisha nyuzi mbili hizi kuhusu Wasukuma, kwanza niliwafundisha watu humu kuhusu kabila la Wasukuma ili watu wawafahamu Wasukuma wenyewe halisi wakoje Tuhuma za Ukabila: Wasukuma si Miongoni mwa Makabila yenye Ukabila, tatizo ndio walio wengi! kisha nikamuulizia Blaza asili yake halisi ni wapi Kauli ya Kakobe "Magufuli atubu", yaibua mambo! Je asili halisi ya Rais Magufuli ni Msukuma, Mhaya au Muha wa Kakonko? na mwisho nikashauri Ili kuepuka possibility ya kutawaliwa na wageni, kuna haja kutumia DNA kuthibitisha asili halisi za viongozi wetu wakuu?
P
 
Hii ndio Taarifa inayozunguka mitandaoni kwa sasa kutoka Dodoma , ambapo Waziri wa Sheria na Katiba Dr Damas Ndumbaro amewaambiwa Wafanyakazi wa Wizara yake na Waandishi wa Habari kwamba Katiba mpya haikwepeki , kwa vile ndio hitaji la Watanzania kwa sasa .

Ameendelea kueleza kwamba mchakato wa Katiba hiyo tayari ushaiva na kwamba Isipokamilishwa Wananchi watashangaa .
,

Amedai vipaumbele vikubwa ni kwenye Sheria ya Uchaguzi wa serikali za mitaa , Uchaguzi Mkuu na Tume ya uchaguzi , na mimi naongezea utata mwingine ni ( madaraka ya Rais )
Kuna Wajinga wapo CCM wanadhani ni HITAJI la CHADEMA
 
Ni wewe mkuu, 'Macho...', au kunamwingine kachukua jina?

Nimesoma, lakini sijakuelewa usemacho!

Ngoja nipumzishe akili, halafu nirudi kukusoma vizuri, huenda nimechanganya mambo.
Ni mimi mkuu. Nataka kuonyesha kuwa mfumo wetu wa uongozi ndiyo adui yetu mkubwa na kiti cha urais kwa katiba ya sasa hata kikikaliwa na nani, kama hakuna mabadiliko ni bure. Kwangu mimi niko tayari ku-sacrifice katiba mpya na bora kwa kiti cha urais (siyo na wabunge lakini). Nina uhakika Samia akiwa rais chini ya katiba nzuri yenye kupunguza madaraka yake na mambo mengine yanayompa umungu mtu tume ya uchaguzi ikiwa huru na wabunge wapatikane kwa uchaguzi huru, na mihimili mingine ijitegee, tutakuwa tumefanya sacrifice nzuri.
 
Back
Top Bottom