Uchaguzi 2020 NEC: Hakuna uthibitisho wa kura feki, taarifa hizo zipuuzwe

Uchaguzi 2020 NEC: Hakuna uthibitisho wa kura feki, taarifa hizo zipuuzwe

mwanamwana

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2011
Posts
1,309
Reaction score
4,798
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage amesema Tume hiyo haijapokea taarifa za uwepo wa kura feki katika majimbo ya Kawe, Pangani na Kigoma.

Amewataka wananchi kuendelea kujitokeza kupiga kura katika muda huu mchache uliobaki.


Jaji Kaijage amesema ''Kuna taarifa kuwepo masanduku ya kura feki katika Jimbo la Buhigwe, Kawe na Pangani, taarifa hizo hazijathibitishwa na hazijawasilishwa rasmi tume. NEC inataka wananchi wapuuze taarifa hizo kwa kuwa hazijathibitishwa"
 
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage amesema Tume hiyo haijapokea taarifa za uwepo wa kura feki katika majimbo ya Kawe, Pangani na Kigoma...
Ulitegemea wakubali kwamba ni feki?
 
Hii mbeleko sasa Too much! Mwenyekiti kahaidiwa nini na watawala?
 
Yaani utengeneze kaclip ukarushe mtandaoni utegemee kila mtu aamini maigizo yako.

Hao watuhumiwa waliokamatwa nazo wako wapi.

Taarifa kwa tume?

Ushahidi wa hizo kura uko wapi?? Waliupeleka Polisi, yaani kwamba mtuhumiwa yuko polisi pamoja na hizo kura alizokamatwa nazo??
 
Habari nzuri sana kwa sisi Wananchi wazalendo

Magufuli ni kiongozi mzuri sana kuwahi kutokea mpenda na msimamia haki

tano tena kama kawa, Tanzaniainaendeda kushangaza dunia tena

Chaguo la Mungu

💛 💚 💛 💚 💛
 
Back
Top Bottom