Uchaguzi 2020 NEC: Kila Chama cha Siasa kimeruhusiwa kuweka wakala kwenye kila kituo ili kulinda maslahi ya Chama na Wagombea

Vitu ambayo vipo kwa mujibu wa taratibu za Uchaguzi, wana viongelea kama vile wanalazimishwa kusema.
Mawakala lazima wawepo mwanzo mwisho. Ndio maana ya Uchaguzi na si vinginevyo.
Uchaguzi huu mkiuchezea tutaingia barabarani, lazima tupasuane matumbo tulane maini wenyewe kwa wenyewe.

#SASABASI
 
Kwa sababu wanaweza kuhongwa wakabadili matokeo au wakazidiwa nguvu na mawakala wengine wengi wa vyama tofauti lakini wenye mrengo mmoja.
Me nilifikiri hao mawakala Ni watu wanaoaminiwa zaidi na chama,swala la kuhongwa na kukubali linathibitisha kuwa wanasiasa wapo kwaajili ya matumbo yao na si masilahi ya wananchi,bila kujali wanatoka mrengo gani wa kisiasa.
 
Swala la kuzidiwa nguvu unalichukuliaje?
Me nilifikiri hao mawakala Ni watu wanaoaminiwa zaidi na chama,swala la kuhongwa na kukubali linathibitisha kuwa wanasiasa wapo kwaajili ya matumbo yao na si masilahi ya wananchi,bila kujali wanatoka mrengo gani wa kisiasa.
 
Je
Je baada ya kupita kura na matokeo kutangazwa mawakala wa vyama watapewa nalala ya matokeo ya wagombea wao?
 
Tukishapiga kura wananchi tunarudi nyumbani kupumzika kisha tunasubiri matokeo kwenye media.utaratibu sindio huu au nimekosea?
 

Huyu Mama Longway ni mwongo. Tatizo la kuziba kura (election fraud) limetengenezwa kwenye Kanuni za uchaguzi. Ebu angalia jinsi kanuni hizi hapa zinavyohatarisha uchaguzi kuwa huru na haki.

1. Kanuni [30(1)&(2)] za Uchaguzi Mkuu wa Rais na wabunge za 2020 na Kanuni [28 (1)&(2)] za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa (Madiwani za 2020 zinaruhusu Serikali (Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Msajili wa Vyama vya Siasa) pamoja na [maofisa wa] Tume (Mkurugenzi wa Uchaguzi, Msimamizi wa Uchaguzi na Msimamizi wa Uchaguzi Msaidizi) kuwekea wagombea mapingamizi. Kanuni hii inaifanya NEC kuwa partial. Ni mara ya kwanza tangu Tanzania ipate Uhuru, badala ya wagombea wao kwa wao, Serikali na Tume wanawekea wagombea mapingamizi. Hadi sasa kuna ushahidi wa kutosha kuthibitisha ukweli kuwa kupitia maofisa wake, Tume imeweka mapingamizi (tena kihuni huni tu) na kuwaengua wagombea wa vyama vya upinzani pekee kugombea viti vya ubunge na udiwani. Hata zimefanyika njama za wazi kabisa kuengua wagombea wa upinzani ili wagombea kupitia CCM wapitishwe kwa viti vya udiwani na/au ubunge (ikiwa ni pamoja na waziri mkuu) bila kupingwa. Matendo haya yanabainisha Tume kuonekana imeegemea upande wa Chama Cha Mapinduzi dhidi ya vyama vya upinzania. Kanuni hizi zinakiuka hata viwango na maadili ya uchaguzi yaliyowekwa na Umoja wa Afrika, Umoja wa SADC, Umoja wa Afrika Mashariki na hata Katiba ya JMT, 1977 [ibara 74]. Sasa Tume inayojidhihirisha namna hii inawezaje kuaminika kwa wananchi, vyama au wagombea?

2. Kanuni [50(4)] ya Uchaguzi wa Rais wa JMT na wabunge na Kanuni [43(4)] ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa (madiwani) zinatengeneza ombwe linaloweza kutumiwa vibaya kuhujumu mawakala wa vyama vya upinzani. Kanuni zinaelekeza mawakala wa vyama vya siasa kula kiapo na kukabidhi nyalaka za utambulisho kwa Msimamizi wa Uchaguzi kisha mawakala waende kwenye vituo vya kupiga kura walivyopangiwa na vyama vyao bila utabulisho wowote. Kwamba mawakala wa vyama vya siasa watajitambulishe kwa wasimamizi wa vituo vya kupiga kura bila kuwa utambulisho rasmi kisha yeye atawapokea na kuwaruhusu kuingia vituoni kutazama mchakato wa uchaguzi. Kanuni hii inatiliwa kuwa imeficha njama dhidi ya mawakala wa vyama vya upinzani; ni chanzo cha tuhuma dhidi Tume.

3. Kanuni 63(2) ya Uchaguzi wa Rais na Wabunge wa JMT inatamka bayana kuwa mawakala wa vyama vya siasa watapewa form ya matokeo ya uchaguzi vituoni (form namba 20) ‘iwapo kutakuwepo nakala za kutosha’. Vyama vya upinzani vinatafsiri kanuni hii kubainisha mawakala wa vyama kunyimwa forms za matokeo ya uchaguzi vituoni kwa kisingizo kuwa kituo hakina nakala za kutosha za forms za matokeo ya uchaguzi. Aidha, kanuni hii mahsusi haitaji chochote kuwa mara baada ya kura kuhesabiwa matokeo ya uchaguzi (form namba 20) yatabandikwa kwenye ubao wa matangazo nje ya kila kituo cha kupiga kura. Sasa katika mazingira ya kanuni hizi, kwa nini Tume isituhumiwe kuwa siyo huru? Kwamba inapendelea CCM. Tume inatakiwa kurekebisha kanuni hizi ili iweze kuaminika na kuaminiwa na wadau – wapiga kura, vyama vya siasa na hata wagombea kabla ya kutuhumu hata kuchukua hatua dhidi ya wagombea wanaoituhumu kwa kutokuwa huru au kutotenda haki.
 

kakae usubiri siku hiyo.

halafu uulize ni sheria ipi.umekaa unasema unalinda kura halafu unasema unajikalia tu!!!
 
Ole wake NEC iweke figisufigisu kwenye hili. Patachimbika. Kwa lugha ya Maalim Seif "ukhanithi sasa basi". ICC the Hague wataenda huku familia zao zikitangilia akhera.
 
Hawa NEC sio watu wakuwaamini sana maana kesho watakuja na sarakasi za kutokidhi viwango
Mpeleke mawakala wanaokidhi viwango vilivyowekwa na katiba, sheria, kanuni na maadili ya uchaguzi! Msipeleke wanywa viroba na wasiojua kusoma
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…