Elections 2010 NEC kushurutisha wapiga kura kurudi majumbani badala ya kusubiri matokeo vituoni!

Elections 2010 NEC kushurutisha wapiga kura kurudi majumbani badala ya kusubiri matokeo vituoni!

nautabaki hivyo hivyo kuitwa dadakuona..................yaani wewe kweli ndio hujui haki yako..........na katika vyote umeenda kuona la kuwa damu lazima imwagike?!!!!!!!!!! Nakuhabarisha hivi mkiiiba kura na wewe ukiwemo lazima nikupe za USO za kutosha........umekalia uzembe,uwizi,uongo....na majungu tuuuu...Kazi hazifanyika, taifa chafu kama hakuna mwenyewe, viongozi wananuka rushwa kazi kuona yasiyo ya msingi. Unadhani kuna amani Tanzania...iba uone kama kuna amani...kama sijakushushia tofali.....mwaka huuu nakuambia CHADEMAAAAAAAAAAAA TUUUUUUUUUUUUUUUUUU
 
Nawapa salamu wana JF ASUBUHI YA LEO. Nina mengi ya kuwa- hint lakini leo nataka niwataadharishshe na huyu mtu anayeitwa Dr Slaa na wafuasi wake wa CHADEMA. NINAWAAMBIA HIVYO KWA SABABU WAMEKARIRIWA kwa mujibu wa gazeti la mtanzania la leo tarehe 29, Septemba ,2009. imewanukuu Dr Slaa na mpambe wake wa karibu Mbowe kuwa ni wachochezi.

MIMI NASEMA WATU HAWA HAWASTAHILI KUISHI NCHINI TANZANIA AMBAYO NI YA AMANI NA UTULIVU. Watu hawa ni hatari yafaa sote tuwaogope eti wanadiriki kusema wananchi wamwage damu ikiwa ni gharama ya kulinda kura. Kama hiyo haitoshi wazandiki hawa wanashawishi matokeo ya uchaguzi mkuu yakataliwe oktoba. Mimi nadahani hawa wanahitaji kwenda hodi ya magonjwa ya akili(Mirembe) wakachunguzwe akili zao kama zipo timamu.

Baada ya kuona wamepunguza umaarufu nchini na kuona waziwazi kuwa hawatashinda kwenye uchaguzi mkuu wanajaribu kushawishi watu wakatae matokeo hii ni laana au nini??? Nawashanga Mbowe na DR. SLAA!! .

Mgombea Urais wa CCM DR .JAKAYA KIKWETE wamejionea wenyewe kwa macho na kusikia jinsi mgombea huyu anayopeta kila anakokwenda kupiga kampeni. Ni wazi kila mtanzania ameona kazi zake alivyozifanya kwa umakini mkubwa katika kipindi cha awamu ya kwanza cha Urais. Hivyo wameamua kwa dhati kumchagua tena katika uchaguzi mkuu mwaka huu.

Watanzania wenzangu tumeshazoea kuishi kwa amani na utulivu tusishawishiwe na wazandiki Dr . Slaa na Mbowe kwa kuwa hawafai.

Chagua Kikwete chagua CCM tarehe 31 Oktoba ,2010 . Cha kufanya unachukua kura yako unaweka waa!!

Vote for Kikwete 2010

Asante kwa kunukuu stori katika gazeti linalomilikwa na fisadi papa Rostam. Kwanza ungepaswa kumuuliza: Jee karudisha zile hela za wananchi alizoiba kupitia kampuni yake ya Kagoda?

Yeye RA ndiyo anataka kuitumbukiza nchi hii vitani kwani ameiweka CCM yote mfukoni mwake huku wengi wana-CCM wakipinga chama chao kuwekwa mfukoni na mdosi. Kwa nini mnapata woga wa kumpeleka mahakamani mwizi huyu?
 
Huu wimbo wa amani na utulivu unakera sana. Inakuwa as if Watanzania wanakula kitu kinachoitwa 'amani na utulivu' Ni wazi kwamba mwizi yeyote anapenda kuwepo amani na utulivu wakati anaiba. Hapendi kusikia kelele za 'mwizi... mwizii..." kwani anajua watu wataamka na atakamatwa na pengine kuuawa. Gazeti la Mtanzania, ambalo sasa limejipambanua kuwa kipaza sauti cha mafisadi, limepotosha makusudi alichosema Mbowe ili ionekane anachochea vurugu. Kwani kusema watu walinde kura zao kwa gharama yoyote ni kuchochea machafuko? Badala yake mimi naona kauli ya chama cha mafisadi kwamba 'Ushindi ni Lazima' ndio inachochea machafuko kwani maana yake ni kwamba hata watakaposhindwa vibaya kwenye uchaguzi wa Oktoba 31 watataka watangazwe washindi. Hapo ndipo tunasema ' PATAKUWA HAPATOSHI.!"
 
Nawapa salamu wana JF ASUBUHI YA LEO. Nina mengi ya kuwa- hint lakini leo nataka niwataadharishshe na huyu mtu anayeitwa Dr Slaa na wafuasi wake wa CHADEMA. NINAWAAMBIA HIVYO KWA SABABU WAMEKARIRIWA kwa mujibu wa gazeti la mtanzania la leo tarehe 29, Septemba ,2009. imewanukuu Dr Slaa na mpambe wake wa karibu Mbowe kuwa ni wachochezi.

MIMI NASEMA WATU HAWA HAWASTAHILI KUISHI NCHINI TANZANIA AMBAYO NI YA AMANI NA UTULIVU. Watu hawa ni hatari yafaa sote tuwaogope eti wanadiriki kusema wananchi wamwage damu ikiwa ni gharama ya kulinda kura. Kama hiyo haitoshi wazandiki hawa wanashawishi matokeo ya uchaguzi mkuu yakataliwe oktoba. Mimi nadahani hawa wanahitaji kwenda hodi ya magonjwa ya akili(Mirembe) wakachunguzwe akili zao kama zipo timamu.

Baada ya kuona wamepunguza umaarufu nchini na kuona waziwazi kuwa hawatashinda kwenye uchaguzi mkuu wanajaribu kushawishi watu wakatae matokeo hii ni laana au nini??? Nawashanga Mbowe na DR. SLAA!! .

Mgombea Urais wa CCM DR .JAKAYA KIKWETE wamejionea wenyewe kwa macho na kusikia jinsi mgombea huyu anayopeta kila anakokwenda kupiga kampeni. Ni wazi kila mtanzania ameona kazi zake alivyozifanya kwa umakini mkubwa katika kipindi cha awamu ya kwanza cha Urais. Hivyo wameamua kwa dhati kumchagua tena katika uchaguzi mkuu mwaka huu.

Watanzania wenzangu tumeshazoea kuishi kwa amani na utulivu tusishawishiwe na wazandiki Dr . Slaa na Mbowe kwa kuwa hawafai.

Chagua Kikwete chagua CCM tarehe 31 Oktoba ,2010 . Cha kufanya unachukua kura yako unaweka waa!!

Vote for Kikwete 2010

Wewe dada kuona naona unakuwa dada kipofu tunajaribu kukufahamisha naona hufahamu au unajifanya hamnazo anyway sio mbaya pengine umeshakunywa maji ya bendera ambayo hata mie zamani niliyanywa for some reason nikaokoka mahali na kuona mwanga wa ubadhirifu nimeamua kuwa sina chama. Sasa tuje katika hoja zako ikiwa Dr Slaa na wenzake kama unavyosema wanachochea uvunjivu wa amani naomba nikuulize maswali yafuatayo:
a) JK na Kinana wanavyotaka kuharibu uchaguzi kwa kupitisha karatasi feki na kutaka kuongeza idadi ya wapiga kura katika majimbo ambayo wanafahamu fika watashindwa vibaya je hii ni utetezi wa amani?

b). JK na Kinana wanajua fika watanzania ni maskini na umaskini wao unasababishwa na ufisadi uliokubuhu ndani ya serikali ya CCM. Badala ya kuzungumzia ahadi za kuleta matumaini kama ni lini atawafunga mafisadi yeye analeta ahadi za ukalumekenge kwa kusema atajenga Airport, sijui Kigoma itakuwa kama Dubai unadhani dhihaka kama hizi wananchi wanafurahi? Na je unadhani hili halipelekei uvunjivu wa amani unaotokana na kugubikwa kwa lindi la umaskini miongoni mwa watanzania wengi?

c). JK na Kinana wametuma mashushushu wao kutandaza siasa za vitisho na woga kwa wananchi mikoani na sijui na wewe mmoja wao but wote wanaeneza siasa za vitisho na woga je nikuulize swali hili halisababishi uvunjivu wa amani? Kwanini kama JK muadilifu asiache wananchi waamue hatima yao badala yake anataka polisi, usalama wa taifa na Jeshi limsaidie? Anapindisha sheria za uchaguzi kila siku je huyu kweli ni mtu muadilifu?

Naomba unijibu maswali yangu dada kuona kwani unaweza kuwa dada kipofu na Dr wako wa heshima asiyostahili
 
CHADEMA: Synovate wahini mahakamani
PostDateIconWednesday, 29 September 2010 04:38

*Slaa asema wanazo nyaraka za utafiti wao.
*Adai kuna mbinu za 'kuchakachua' matokeo.

Na Tumaini Makene

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeivaa kampuni utafiti ya Synovate kikisisitiza kuwa kina matokeo ya utafiti uliofanywa na kampuni hiyo ya kupata matokeo yaliyotoa ushindi wa asilimia 45 kwa chama hicho na mgombea wake wa urais, Dkt. Willibrod Slaa.

Synovate hivi karibuni ilikanusha habari kuwa haijawahi kufanya utafiti wala kuficha matokeo hayo yaliyodaiwa kuipa CCM na mgombea wake Rais Jakaya Kikwete asilimia 41, huku ikitishia kulishtaki gazeti moja liliwakariri viongozi wa CHADEMA wakieleza utafiti huo.

Akizungumzia matokeo hayo jana, Dkt. Slaa alisema "Synovate wakimbie haraka mahakamani, tunazo document (nyaraka), hata gazeti lililotishiwa kushtakiwa lisiwe na wasiwasi, huu ni wakati wa kuvunja heshima ya Synovate kitaifa na kimataifa.

"Walifanya utafiti na katika swali namba GP 06 waliuliza, 'uchaguzi ukifanyika sasa hivi nani utampigia kura kuwa rais wa Tanzania?' na majina yote yaliweka pale ya wagombea, sasa wanakanusha nini, waende haraka sana mahakamani, vinginevyo credibility (heshima) yao tutaivuruga nchi nzima na kimataifa, alisema huku akionesha nyaraka hizo kwa mbali.

Dkt. Slaa alisema katika nchi nyingine taasisi za maoni zinakuwa huru, hazipendelei chama chochote kile.

Katika hatua nyingine, CHADEMA kimemshutumu serikali ya CCM inanyoongozwa na Rais Jakaya Kikwete kikidai kuwa imepanga kutumia mbinu chafu ili kuhujumu Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu.

Kimesema kuwa kinazo taarifa za uhakika kuwa kati ya mbinu hizo chafu ambazo zinatumiwa au zinataka kutumiwa na serikali kukibeba Chama Cha Mapinduzi katika uchaguzi wa mwaka huu ni kutoa maelekezo kwa Usalama wa Taifa na kujipanga kuchapisha karatasi bandia za kupigia kura nje ya nchi.

CHADEMA kimesema kuwa njama hizo ni aina ya ufisadi kwa kuwa zinahusisha matumizi mabaya ya madaraka na raslimali za nchi kukisaidia chama kimoja cha siasa-CCM, hivyo hazipaswi kuvumiliwa kwani zina lengo la kuingilia maamuzi ya wapiga kura na kuvuruga amani ya nchi.

Kimesema kuwa iwapo mbinu hizo chafu zitafanikiwa kwa kuharibu uchaguzi na kupanga matokeo ya kuipendelea CCM na mgombea wake wa urais, "Rais Kikwete ndiye atabeba lawama na laana zote juu ya yale yatakayotokea. Usalama wa Taifa wakanushe kama hawajapewa maelekezo na kama sasa hawazunguki mikoani."

Hayo yalisemwa jana Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Willibroad Slaa alipokuwa akizungumza na waandishi ambapo alisisitiza kuwa siku zote chama hicho kimekuwa kikisema kuwa amani ya nchi wakati wa uchaguzi imekuwa ikivurugwa na chama tawala kwa nia ya kutaka kung'ang'ania madaraka, kinyume na maamuzi ya Watanzania.

"Leo tumewaita kuzungumzia juu ya mambo matatu, maamuzi ya Kamati Kuu ya CHADEMA hasa juu ya ubunge wa viti maalumu, uchaguzi mkuu wa mwaka huu na suala la Synovate (kampuni inayojihusisha na kura za maoni ya watu)...juu ya uchaguzi mkuu tunazo taarifa za uhakika kuwa Serikali imetoa instructions (maelekezo) kwa Usalama wa Taifa na sasa wako mikoani wakizunguka nchi nzima, kuhakikisha Kikwete anashinda kwa hali yoyote ile.

"Tunajua mikoa ambayo wamekwisha kwenda mpaka sasa hivi na wanachofanya huko tunakijua...hii ni sawa na ile barua tuliyoikamata hivi karibuni ikiwaelekeza watendaji wa Serikali kuhakikisha CCM inashinda uchaguzi wa mwaka huu kwa hali na mali. Tunatoa angalizo mapema lolote litakalotokea mwaka huu Rais Kikwete atabeba lawama na laana zote za Watanzania.

"Kwa hali wanayoionesha ya kuhangaika mpaka sasa Kikwete ameshashindwa. Ni kigezo tosha kuwa mpaka sasa wameshashindwa uchaguzi. Tunapenda kumwambia kuwa uchaguzi wa mwaka huu ni uchaguzi wa wananchi, hakuna cha Usalama wa Taifa, hakuna cha JWTZ wala FFU, waache wananchi wafanye maamuzi juu ya nchi yao," alisema Dkt. Slaa.

Dkt. Slaa ambaye pia ni Mgombea urais wa CHADEMA katika uchaguzi wa mwaka huu, lakini jana akitumia kofia yake ya ukatibu mkuu wa chama alisema kuwa wanazo pia taarifa za kina na za uhakika kuwa kuna karatasi za bandia zinachapishwa katika moja ya nchi za nje, ili zije zitumike wakati wa uchaguzi, akidai ni mwendelezo wa mbinu chafu za kuiba kura.

Alisema chama chake na Watanzania wengi wapenda haki hawatakubali mbinu hizo chafu, akisema matumizi mabaya ya madaraka na raslimali za nchi ni aina ya ufisadi ambao CHADEMA kimekuwa kikiupiga vita tangu kilipotangaza orodha ya aibu ya watu mafisadi wapato 11 nchini.

"Wanaonesha dhahiri kuelemewa...sasa wanafanya vitendo vya kuhatarisha amani ya nchi, hawaitakii mema nchi. Tunasema amani ikivunjika Kikwete atabeba lawama, hatuwezi kukubali udikteta na ubabe huu. Kutumia raslimali za serikali na matumizi mabaya ya madaraka ni aina ya ufisadi, ndiyo maana Kikwete tulimweka katika orodha ya mafisadi."

Akiongezea katika suala hilo, Mwenyekiti wa CHADEMA taifa, Bw. Freeman Mbowe alisema kuwa uchaguzi mkuu wa mwaka huu ukivurugika, Rais Kikwete, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini watapaswa kuwajibika mbele ya Watanzania.

Bw. Mbowe alisema kuwa kuna vitendo vinavyofanywa na baadhi ya viongozi hao kwa nia ya kubeba ushindi wa CCM vinaiweka matatani dhana nzima ya demokrasia na kuonekana kiini macho, hali ambayo haiwezi kukubalika.

"Tunapenda kutoa tahadhari kwa Rais Kikwete, kwa NEC na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, yaani kwa Makame (Jaji Lewis, Mwenyekiti wa NEC) na Tendwa (John, Msajili), watu hawa watatu ndiyo wenye mamlaka ya umma na wajibu wa kutoa haki, utulivu na amani katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu.

"Bahati mbaya sana watu hawa watatu wana mikakati ya kuchakachua kura badala ya kutenda haki, wanaliandaa taifa kuchakachua kura...tunatoa angalizo kwa jamii nzima na jumuiya ya kimataifa demokrasia nchi hii ni kiinimacho. Msajili kwa makusudi anabadilisha na kuvunja sheria iliyotungwa na bunge ili kumsaidia Kikwete, halafu hakuna mtu yeyote anayejali wala kuchukuliwa hatua...huu ni uwendawazimu.

"Jana Shinyanga Kikwete kahutubia mpaka saa 1, karibu kila mahali anazidisha muda...tunataka jamii nzima na jumuiya ya kimataifa ituelewe, hawa watu wameshindwa siasa za hoja, wameshindwa siasa za aina zote za maana sasa wanajiandaa kwa siasa za uchakachuaji...mwaka huu kitaeleweka, hapatatosha pale wananchi watakapoamua kulinda maamuzi na kura zao," alisema Bw. Mbowe.

Aliongeza kuwa chama hicho kitaandaa malalamiko ya kuwayawasilisha kwa NEC na Tendwa juu ya vitendo vya kuzidisha muda.

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Bw. Salvatory Rweyemamu alipoulizwa kuhusiana na tuhuma hizo jana, alisema hizi ni tuhuma za kisiasa na zinamhusu mgombea wa CCM, kwa hiyo aulizwe Meneja wa Kampeni wa chama hicho, Bw. Abdulrahaman Kinana.

Bw. Kinana hakupatikana kwenye simu yake ya mkononi ambayo mara kadhaa ilikuwa ikiita bila kupokewa.

Kuhusu suala la uteuzi wa majina ya wabunge wa viti maalumu wanawake ndani ya CHADEMA, Dkt. Slaa alijigamba kuwa chama chake kimeweka historia nchini kwa kuwa chama cha kwanza kutumia njia ya kisiasa na kisayansi kupata wabunge hao, huku akisema sheria ya uchaguzi inayolazimisha vyama vya siasa kuwasilisha majina hayo siku 30 kabla ya uchaguzi ni chanzo cha zoezi hilo kutofanyika kwa ufanisi mapema, hivyo watairekebisha wakipewa ridhaa ya kuongoza nchi.

"Njia ambayo consultant (mshauri) wetu atawaeleza vizuri imeondoa kabisa yale mawazo ya wabunge kutoka upande mmoja wa nchi, dhana ya mchezo mchafu mtu kumweka girlfriend wake, uswahiba na unafiki mwingine, hii ni kwa sababu CHADEMA tumedhamiria kuchukua dola na tunaenda kuchukua dola. Hivyo ilikuwa lazima tujipange vizuri kupata wabunge kutoka nchi nzima, maana hata katika majimbo tumesimamisha wabunge 185," alisema Dkt. Slaa.

Kwa upande wake mtaalamu mshauri aliyepewa kazi ya kuratibu utaratibu wa kuwapata wabunge wa viti maalumu, Dkt. Kitila Mkumbo alisema kuwa kwa uchanganuzi aliofanya kwa kutumia vigezo vya jumla kama vile umahiri, bidii, dhana ya uwakilishi wa wananchi kupitia wabunge wa viti maalumu na kila kanda kupata nafasi, itasaidia CHADEMA kupata wabunge makini kama ilivyokuwa katika bunge lililopita.

"Mbali ya vigezo hivyo vya jumla nilitumia vigezo vingine kwa sayansi ya takwimu ambavyo vilikuwa ni elimu, uzoefu wa uongozi kisiasa, uzoefu wa uongozi nje ya siasa, ugombea ubunge jimboni, mchango wa hali na mali katika shughuli za chama na kampeni zinazoendelea, umri katika chama, ambapo kila kigezo kilikuwa na sehemu ndogondogo tofauti ambavyo ndivyo tulitolea maksi.

"Kwa kweli kwa ukokotoaji wa vigezo hivyo CHADEMA imepata wabunge mchanganyiko wenye sifa mbalimbali kutoka karibu kila eneo la nchi katika kanda mbalimbali, kwa kweli ilikuwa lazima kuzingatia vigezo vingi kwani CHADEMA kinajiandaa kuunda serikali.

mwisho.

Source: Majira
 
nautabaki hivyo hivyo kuitwa dadakuona..................yaani wewe kweli ndio hujui haki yako..........na katika vyote umeenda kuona la kuwa damu lazima imwagike?!!!!!!!!!! Nakuhabarisha hivi mkiiiba kura na wewe ukiwemo lazima nikupe za USO za kutosha........umekalia uzembe,uwizi,uongo....na majungu tuuuu...Kazi hazifanyika, taifa chafu kama hakuna mwenyewe, viongozi wananuka rushwa kazi kuona yasiyo ya msingi. Unadhani kuna amani Tanzania...iba uone kama kuna amani...kama sijakushushia tofali.....mwaka huuu nakuambia CHADEMAAAAAAAAAAAA TUUUUUUUUUUUUUUUUUU

Hivi wewe unadhani CHADEMA wana muujiza?. Tanzania ni ile ile, watu ni walewale, mazingira ni yaleyale!!, ukiondoa Dr. Slaa what is new their at Chadema?? My friend that is just politics fanya kazi ulipo kutatua matatizo yako mwenyewe. Hakuna mtu anakuja na muujiza.
 
Nawapa salamu wana JF ASUBUHI YA LEO. Nina mengi ya kuwa- hint lakini leo nataka niwataadharishshe na huyu mtu anayeitwa Dr Slaa na wafuasi wake wa CHADEMA. NINAWAAMBIA HIVYO KWA SABABU WAMEKARIRIWA kwa mujibu wa gazeti la mtanzania la leo tarehe 29, Septemba ,2009. imewanukuu Dr Slaa na mpambe wake wa karibu Mbowe kuwa ni wachochezi.

MIMI NASEMA WATU HAWA HAWASTAHILI KUISHI NCHINI TANZANIA AMBAYO NI YA AMANI NA UTULIVU. Watu hawa ni hatari yafaa sote tuwaogope eti wanadiriki kusema wananchi wamwage damu ikiwa ni gharama ya kulinda kura. Kama hiyo haitoshi wazandiki hawa wanashawishi matokeo ya uchaguzi mkuu yakataliwe oktoba. Mimi nadahani hawa wanahitaji kwenda hodi ya magonjwa ya akili(Mirembe) wakachunguzwe akili zao kama zipo timamu.

Baada ya kuona wamepunguza umaarufu nchini na kuona waziwazi kuwa hawatashinda kwenye uchaguzi mkuu wanajaribu kushawishi watu wakatae matokeo hii ni laana au nini??? Nawashanga Mbowe na DR. SLAA!! .

Mgombea Urais wa CCM DR .JAKAYA KIKWETE wamejionea wenyewe kwa macho na kusikia jinsi mgombea huyu anayopeta kila anakokwenda kupiga kampeni. Ni wazi kila mtanzania ameona kazi zake alivyozifanya kwa umakini mkubwa katika kipindi cha awamu ya kwanza cha Urais. Hivyo wameamua kwa dhati kumchagua tena katika uchaguzi mkuu mwaka huu.

Watanzania wenzangu tumeshazoea kuishi kwa amani na utulivu tusishawishiwe na wazandiki Dr . Slaa na Mbowe kwa kuwa hawafai.

Chagua Kikwete chagua CCM tarehe 31 Oktoba ,2010 . Cha kufanya unachukua kura yako unaweka waa!!

Vote for Kikwete 2010



Gazeti: Mtanzania!!!!!!!!
Walewale akina Maralia Sugu, Mgonjwa Ukimwi, Karanaga, Kibunango, Mugongo Mugongo......................The list goes on and on and on!!!!!!!!!!!!!!!!!! Watoto wa walioshika utamu hao!!!!
 
Wafuasi wa Chadema naona mnapayuka tu! Amini nawaambia Tanzania ni nchi ya amani hatuhitaji wachochezi.


Chagua Kikwete tarehe 31 Oktoba 2010
 
Nawapa salamu wana JF ASUBUHI YA LEO. Nina mengi ya kuwa- hint lakini leo nataka niwataadharishshe na huyu mtu anayeitwa Dr Slaa na wafuasi wake wa CHADEMA. NINAWAAMBIA HIVYO KWA SABABU WAMEKARIRIWA kwa mujibu wa gazeti la mtanzania la leo tarehe 29, Septemba ,2009. imewanukuu Dr Slaa na mpambe wake wa karibu Mbowe kuwa ni wachochezi.

MIMI NASEMA WATU HAWA HAWASTAHILI KUISHI NCHINI TANZANIA AMBAYO NI YA AMANI NA UTULIVU. Watu hawa ni hatari yafaa sote tuwaogope eti wanadiriki kusema wananchi wamwage damu ikiwa ni gharama ya kulinda kura. Kama hiyo haitoshi wazandiki hawa wanashawishi matokeo ya uchaguzi mkuu yakataliwe oktoba. Mimi nadahani hawa wanahitaji kwenda hodi ya magonjwa ya akili(Mirembe) wakachunguzwe akili zao kama zipo timamu.

Baada ya kuona wamepunguza umaarufu nchini na kuona waziwazi kuwa hawatashinda kwenye uchaguzi mkuu wanajaribu kushawishi watu wakatae matokeo hii ni laana au nini??? Nawashanga Mbowe na DR. SLAA!! .

Mgombea Urais wa CCM DR .JAKAYA KIKWETE wamejionea wenyewe kwa macho na kusikia jinsi mgombea huyu anayopeta kila anakokwenda kupiga kampeni. Ni wazi kila mtanzania ameona kazi zake alivyozifanya kwa umakini mkubwa katika kipindi cha awamu ya kwanza cha Urais. Hivyo wameamua kwa dhati kumchagua tena katika uchaguzi mkuu mwaka huu.

Watanzania wenzangu tumeshazoea kuishi kwa amani na utulivu tusishawishiwe na wazandiki Dr . Slaa na Mbowe kwa kuwa hawafai.

Chagua Kikwete chagua CCM tarehe 31 Oktoba ,2010 . Cha kufanya unachukua kura yako unaweka waa!!

Vote for Kikwete 2010

Umechanganyikiwa au umetekewa kwanza umesoma gazeti linaitwa mtanzania la ra, Nashauri soma magazeti mengine pia. Lugha yako ndiyo ya uchochezi kabisa kwani wewe unamwakilisha nani hadi kutuambia tunaishi kwa "amani na utulivu". Kuwa mkweli tu wewe na mabwana zako wa ccm ndio mnaishi kwa amani na utulivu.

Mwisho unahofia dhuluma mlizozifanya zitawatokea puani hilo ni kweli jitayarisheni kupambana na wananchi wenye usongo na nyinyi.
 
Ninaloshangaa kuhusu Dr. Slaa ni jinsi anavyosema anataka wabunge wa viti maalum wanawake wachaguliwe baada ya Uchaguzi ,baada, ya Chama kuhahakikisha kama alivyosema''ni wanawake wepi wameonyesha heshima zote wakati wa Kampeni' 'Hii ni recipe ya hao wanawake kuwa wahuni.
Kwa sababu hata hizi Kampeni zote zinazofanyika sasa hivi hazihitajiki. Hawa watu wanaofanya Kampeni wanafahamika tayari;Kikwete,Dr. Slaa,na Mr. Lipumba. Sasa kwa nini CHADEMA washindwe kuwachaua wabunge wa viti maalum sasa hivi?
 
dadakuona,
Ebu soma na magazeti mengine basi:

Mwanahalisi ya leo ina haya kwenye maoni ya wasomaji (siyo maoni ya waandishi wanaolamba viatu vya mafisadi)::

Makamba: Nani muongo?
Mheshimiwa Yusufu Makamba, ni zipi ahadi za uongo kati ya zile zinazotolewa na Dr. W. Slaa na za JK? Ahadi tano za JK:
1. Kujenga barabara za juu dar ili kuondoa msongamano. 2. Kujenga daraja Dar - Kigamboni 3. Kujenga daraja kubwa Kilombero mwakani 4. International Airport - Misenyi BKB, 5. Umeme wa uhakika Kigoma

Ahaditano za Dr. Slaa
1. Kusimamia Katiba mpya withini 100 days! 2. Kuunda baraza dogo la mawaziri 20 waliothibitishwa na Bunge. 3. Kufanya elimu ya lazima kuwa hadi kidato cha sita (itatolewa bure) 4. Kupunguza baadhi ya kodi ambazo ni mzigo kwa walalahoi. 5. Kuhakikisha fedha za UPAU WA DECI ambazo zimeporwa na serkali kurudishwa kwa wenyewe.
 
Kwa nini mnampa kichwa malaria sugu a.k.a Tandale one a.k.a Kakakuona a.k.a Dadakuona a.k.a jeykey kwa kumjibu?!! Huyu unasoma halafu UNATUPILIA KULE!
 
Nawapa salamu wana JF ASUBUHI YA LEO. Nina mengi ya kuwa- hint lakini leo nataka niwataadharishshe na huyu mtu anayeitwa Dr Slaa na wafuasi wake wa CHADEMA. NINAWAAMBIA HIVYO KWA SABABU WAMEKARIRIWA kwa mujibu wa gazeti la mtanzania la leo tarehe 29, Septemba ,2009. imewanukuu Dr Slaa na mpambe wake wa karibu Mbowe kuwa ni wachochezi.

MIMI NASEMA WATU HAWA HAWASTAHILI KUISHI NCHINI TANZANIA AMBAYO NI YA AMANI NA UTULIVU. Watu hawa ni hatari yafaa sote tuwaogope eti wanadiriki kusema wananchi wamwage damu ikiwa ni gharama ya kulinda kura. Kama hiyo haitoshi wazandiki hawa wanashawishi matokeo ya uchaguzi mkuu yakataliwe oktoba. Mimi nadahani hawa wanahitaji kwenda hodi ya magonjwa ya akili(Mirembe) wakachunguzwe akili zao kama zipo timamu.

Baada ya kuona wamepunguza umaarufu nchini na kuona waziwazi kuwa hawatashinda kwenye uchaguzi mkuu wanajaribu kushawishi watu wakatae matokeo hii ni laana au nini??? Nawashanga Mbowe na DR. SLAA!! .

Mgombea Urais wa CCM DR .JAKAYA KIKWETE wamejionea wenyewe kwa macho na kusikia jinsi mgombea huyu anayopeta kila anakokwenda kupiga kampeni. Ni wazi kila mtanzania ameona kazi zake alivyozifanya kwa umakini mkubwa katika kipindi cha awamu ya kwanza cha Urais. Hivyo wameamua kwa dhati kumchagua tena katika uchaguzi mkuu mwaka huu.

Watanzania wenzangu tumeshazoea kuishi kwa amani na utulivu tusishawishiwe na wazandiki Dr . Slaa na Mbowe kwa kuwa hawafai.

Chagua Kikwete chagua CCM tarehe 31 Oktoba ,2010 . Cha kufanya unachukua kura yako unaweka waa!!

Vote for Kikwete 2010

September is full of crazy aliens here in JF.....
 
Ile kauli ya kulala kwenye vitua vya kupiga kura, ni dalili tosha ya kuonyesha kufilisika kwa slaa na Chadema yake...

Niambie umepewa shs. ngapi ama umeahidiwa cheo gani, maana nina uhakika hakuna mtz anayemkampenia kikwete bure. Kila mtu anaufahamu uozo wake ila kwa kuwa CCM wako tiyari hata kuua ili wabaki madarakani wanawatumia vidampa kama wewe kwa vijielfu tano na uharo mwingine. Nasubiri jibu la huo mshiko wako nikupe ushauri wa bure!!
 
Ninaloshangaa kuhusu Dr. Slaa ni jinsi anavyosema anataka wabunge wa viti maalum wanawake wachaguliwe baada ya Uchaguzi ,baada, ya Chama kuhahakikisha kama alivyosema''ni wanawake wepi wameonyesha heshima zote wakati wa Kampeni' 'Hii ni recipe ya hao wanawake kuwa wahuni.
Kwa sababu hata hizi Kampeni zote zinazofanyika sasa hivi hazihitajiki. Hawa watu wanaofanya Kampeni wanafahamika tayari;Kikwete,Dr. Slaa,na Mr. Lipumba. Sasa kwa nini CHADEMA washindwe kuwachaua wabunge wa viti maalum sasa hivi?

Viti maalum vinategemea sana matokeo halisi ya uchaguzi kutegemeana na % seats chama kilivyopata....CCM wamependekeza wao kwa assumption watashinda 100%...CHADEMA wanasubiri hali halisi..ni sualal la kujipanga tu
 
tunajua dadakuona we ni kibaraka wa hilo chama,sera zilezile hakuna utekelezaji ,ahadi zimezidi oh God forbid ikibidi iwe hivyo kwa sababu tumechoka,serikali ya si si em imezidi kutuogopesha kwa kutumia vyombo vya habari wanavyomiliki wao,wameuza mashirika tetu ya umma leo sisi tunasafa mtaani bado tukipata mkombozi kama DK SLAA NA AKINA ZITO wakituellimisha kuhusiana na style ya sisiem kuiba kura wanawaita wachochezi WE FADE UP NA PROMISE HEWA TUNATAKA M2 MWINGINE AMBAYE ni DK SLAA.SLAA ANAWEZA KUTURUDISHIA MATUMAINI
yaliyopotea kwa miaka zaidi ya AROBAINI,we have everything still we are poor we need somebody who is strong like DK SLAA,SOMEBODY WHO IS FOCUSED,WE DADAKUONA NA GHILO GAZETI MSHINDWE KTK JINA LA YESU,VOTE FOR SLAA VOTE FOR CHADEMA WE NEED CHANGES YES WE CAN ,MUNGU MBARIKI SLAA MUNGU IBARIKI CHADEMA,MUNGI IBARIKI TANZANIA,TUMECHOKA KUONGOPEWA NA VYOMBO VYAO VYA HABARI,::tea:
 
Back
Top Bottom