Uchaguzi 2020 NEC tumieni mafuriko mikutano ya Lissu kusoma alama za nyakati

Uchaguzi 2020 NEC tumieni mafuriko mikutano ya Lissu kusoma alama za nyakati

onjwayo

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2020
Posts
1,356
Reaction score
1,309
Ni muda Sasa NEC kupitia picha na video kurudia rudia mafuriko na mikutano ya Lissu kusoma alama za nyakati. Mikutano ambayo haipewi matangazo ya kutosha, mikutano isiyorushwa live, mikutano isiyopewa kipaumbele kwenye taarifa za habari redioni, magazetini na vituo vya televisheni, mikutano isiyo na makundi makubwa ya wasanii, mikutano isiyokuwa na wanafunzi wanaolazimishwa kufunga shule na mikutano isiyo na mabasi na malori ya kusomba watu. Mtu anayepita na kuomba michango kuendesha kampeni kubwa ya kutisha. Mtu aliyekosa mabango makubwa, lakini umashuhuri na nyomi Ni wali wa kushiba mfungwa aliyetoka jela.

Kama NEC watakuwa makini Basi wasichezee hisia za umma. NEC watimize wajibu wao Kama wasimamizi wakuu wa uchaguzi unaoelezwa Ni wa kihistoria. Juhudi au njama za kutaka au kuwaza kupindua matokea haiwezi kuvumiliwa na umma wa wapenda amani. Hili zoezi linaweza kuingia doa endapo tu hiyo NEC ikaboronga kwa namna itakavyoshindwa kuusimamia vizuri.

Yapo Mambo mengi ambayo yanasemwa na kauli hizi sijui kwa Nini NEC haijazisikia na kutoa ufafanuzi. Upo uvumi usiothibitishwa kuwa CCM kupitia kwa makatibu wakuu wake wanakutana na makundi ya watumishi na kuwahimiza waombe kusimamia uchaguzi kwa lengo la kubadili matokeo vituoni. Kama hili wazo lipo Basi wahusika wakome Mara moja kuendelea kuratibu huo hujuma na NEC wapeleleze na kukemea au kutoa onyo.

Kwa namna wapiga kura walivyo watulivu na kuhudhuria kampeni za Lissu na Magufuli basi ni wazi uchaguzi huu ni vuta nikuvute. Nia mbaya za upendeleo hazitavumilika, kauli na uvumilivu Ni kitu muhimu Sana. Siyo busara kwa NEC kusema ukiukwaji na taratibu watumie nguvu za kipolisi Kama ilivyotumika Nyamongo. Muda Fulani kwa sababu za kijografia Ni kuketi na wadau meza moja kutazama juu ya ratiba.

Polisi wakae Kando maana kujikuta uko kituo A badala ya B siyo makusudi Bali Ni kosa la kawaida tu. Hivyo isije kuwa suluhu ya polisi na NEC Ni kuagiza watu kupigwa mabomu. Uchaguzi huru, Kama umakini utakuwepo utawezekana. Vifaa visambazwe mapema na mawakala wote wapewe fomu na kuruhusiwa kusimamia vyama vyao. Itambulike eneo muhimu Ni hapa kwenye vifaa na mawakala toka vyama vyote.

Uchaguzi na maandalizi mema. Niwatakieni busara na lugha Safi wagombea. Si kila tuhuma dhidi ya NEC Ni tusi au khasifa Bali Ni maono ya njama zilizopita. Pia NEC irahisishe rufani za wagombea waliobaki kwa kuwekewa pingamizi. Hii inaichafua NEC kitaifa na kimataifa, haikuwahi kutokea wakati wa kina Mkapa na Kikwete Sasa iweje kipindi hiki?

Uoga wa CCM isije kutafasiriwa kuwa Ni kutaka kubebwa na NEC . Kikubwa Ni kuwa atakayeshindwa ndiye atangazwe toka kituo Cha kupigia kura Hadi kituo Cha kutolea matokeo. Vyama pia visiingiliwe kwenye talling centres zao. Waachwe kuwa huru maana Ni haki yao kuwa na matokeo na kufuatilia vyama vyao. Narudia polisi na watumishi toka NEC wasikipendelee chama Chochote.

Amani idumu Tanzania
 
Watu wanataka umeme, barabara, na reli. Bwana Mahela.. NEC
IGP ataanza kuwa piga mabomu msishangae. Mahela NEC. Anadhani tunaishi kwa matisho ili amfurahishe bwana wake
 
Hakika mkuu..paragraph ya Mwisho ya andiko lako ndilo lililobeba "Uchaguzi kuwa huru na wa Haki "Lakin kuna dalili ya wala Kodi za wananchi kufanya hila katika uchaguzi huu"

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
 
Taifa la watu wajinga hawajifunzi bali kwa kuvuruga na kumwaga damu ndipo akili zao hutambuwa ukweli
 
NEC walishaandaa mshindi wao Kama ilivyo kawaida yao ili nyomi awakulitegemea thus mahera anasoma barua za maagizo huku akitetemeka pale mabeberu, Robert Amsterdam, watz wanatumbua macho kila kitu wanataka wanaona ufanyacho hapa wamechanganyikiwa kabisa ni sawa na kutafuta kichaka Cha kujisaidia jangwani. Nec wakubali matokeo tu janja janja mwisho ilikuwa 2015 kuepusha lawama waache uchaguzi uwe huru kila kitu kiwe wazi ili wananchi wachague wawatakao na sio kuwanyima haki zao ikiwemo kupita bila kupingwa.
 
Mafuriko yake yanazidi yale ya Lowassa?

Je wanaokuja tena kwa idadi ndogo ni wapigakura?

Sisi wapiga kura tupo majumbani tunasubiri tarehe tukampigie Magu tena
Umenifurahisha Sana eti wapiga kura mko majumbani, kweli watoto wa shule na wasanii siyo wapiga kura
 
Mashabiki wa chadema ni wajinga sana!

Hayo mafuriko Magu hana?

Kwanini huu uchguzi mmeshajiaminisha kwamba mna shinda? Kwa vigezo vipi?

Hivi mnafikiri hao mabwana zenu wao ni wajinga hawaoni uhalisia?
 
Mashabiki wa chadema ni wajinga sana!

Hayo mafuriko Magu hana?

Kwanini huu uchguzi mmeshajiaminisha kwamba mna shinda? Kwa vigezo vipi?

Hivi mnafikiri hao mabwana zenu wao ni wajinga hawaoni uhalisia?
Watashangaa wakipata asilimia 2 kwa 98 kwa Magufuli... sipotezi tena kura yangu kwa mbelgiji....[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Lisu sio Lowasa wa kumuachia Mungu,pili hoja ya awajaajiandikisha ni hoja mufilisi kabisa,kwani hao nyomi wa ccm wamejiandikisha.
Siyo Lowasa wa kumuachia Mungu?

Atafanya nini sasa? Acheni ujinga!

Lissu hana kura za kuifanya tume kupindisha matokeo, hana, atapata chini ya 20%

Mtu wenu kafeli sana! Hata wale waliokuwa na imani nae wamesharudi nyuma kwamba kumbe wanamchagua Amsterdam na si Lisu
 
Mwogope sana mtu anayehubiri AMANI na wakati huo huo hataji kile kiletacho amani. Hata viongozi wa dini utawasikia tunaomba uchaguzi huu upite kwa amani.....Amani bila kuifanyia kazi HAKI ni sawa na kupenda kuwa mtoto lakini hupendi kuzungumzia MIMBA.

Amani ya kweli itakuwepo bila hata kutishiana wala kutolea misuli pale HAKI ikizingatiwa katika uchaguzi.
 
Back
Top Bottom