Uchaguzi 2020 NEC: Wagombea muwe makini, tusilaumiane

Uchaguzi 2020 NEC: Wagombea muwe makini, tusilaumiane

Kwani Kuna wagombea vichaa?
Kama mgombea kiti cha urais hawezi kujaza fomu kwa usahihi, hafai
UKIKOSEA SPELLING TUU TUNAKUKNOCKOUT, MAANA UTAKUWA UNAUDHALILISHA UMMA WA WATANZANIA KUTOJAZA FOMU YAKO KWA UMAKINI
 
Hii tume haina Uhuru wowote, hawa wanapokea maelekezo kimyakimya toka ccm.kwa tume hii kazi bado mbichi...
 
Tume makini ingesema kuwa wagombea wanaweza kupata ushauri kutoka kwa Tume kuhusu ukamilifu wa fomu zao. Ili kulinda demokrasia, ni wajibu wa Tume kuhakikisha wagombea wengi iwezekanavyo wanapata fursa ya kugombea.

Ningetegemea msimamizi anapo pokea fomu aipitie pamoja na mgombea na kumpa nafasi ya kusahihisha dosari zozote zinazoonekana kabla ya dirisha kufungwa.

Lugha za tusilaumiane hazipendezi.

Amandla....
Hazipendezi na zinaashiria mwanzo wa jammbo fulani lisilopendeza!
 
Aliyekuambia kujaza fomu ni kama kufanya mtihani nani? Kujaza fomu ni swala la kuelekezana tu na wala halitakiwi kuwa swala la kukomoana. Unapolilinganisha na mtihani unataka kutuaminisha kuwa kwenye kujaza fomu ndio uchaguzi wa wananchi. Acheni kuanza kutengeneza mazingira ya kuhujumu upinzani kabla hata ya kura kupigwa.
Da jamaa wewe una akili na Roho nziri Sana.
Hivi vijamaa vya CCM vimekaa kudhulumu tu.
 
Sina la kuongeza, baba...
Tume makini ingesema kuwa wagombea wanaweza kupata ushauri kutoka kwa Tume kuhusu ukamilifu wa fomu zao. Ili kulinda demokrasia, ni wajibu wa Tume kuhakikisha wagombea wengi iwezekanavyo wanapata fursa ya kugombea.

Ningetegemea msimamizi anapo pokea fomu aipitie pamoja na mgombea na kumpa nafasi ya kusahihisha dosari zozote zinazoonekana kabla ya dirisha kufungwa.

Lugha za tusilaumiane hazipendezi.

Amandla....
 
Naam! Ni sahivi kutoa copy, au ku-scan fomu iliyojazwa kabla ya kuirudisha ili kubaki na nakala ngumu/ na laini kwa ajili ya kuja kuwaumbua mawakala wa shetani waliohujumu wagombea wa upinzani mwaka 2019 katika uchaguzi wa serikali za mitaa.

Ni vyema pia kuweka ushahidi wa video wa makabidhiano ya fomu, maana mawakala wa shetani wameshapokea maelekezo wazichome fomu waseme hawajapokea, mwaka huu tutaenda sambasamba mpaka home "nait kali" tutawazukia ikibidi

Hilo la kuweka copy ni lazima, maana Tume huwa inaagizwa kuchezea fomu za wapinzani. Halafu sioni mantiki ya kukosea fomu kisha uenguliwe, badala ya kupewa nyingine ili ujaze kwa usahihi. Sehemu zote huwa kuna makosa kwenye ujazaji wa fomu, lakini sijawahi kuona ukinyimwa huduma, badala yake hupewa nyingine ili ujaze kwa usahihi.

Ni vyema vyama vya upinzani waangalie fomu zote, kisha kutoa muongozo kwa wagombea wake ili wajaze kwa usahihi. Huo ujazaji wa fomu unawekwa wa kuchanganya, ili wagombea hasa wa upinzani waenguliwe.
 
Hahahaaaaaaaa kukosea ndio moja ya kuonesha huwezi kazi.

Mwanafunzi anayefaulu vizuri haimaanishi kuwa amepata asilimia 100. Sasa kama mtu anaenguliwa eti kwa kuandika jina la mtaa kwa spelling error, kama sio upuuzi ni nini? Kibaya zaidi makosa hayo yanatumika kwa wapinzani tu, lakini ccm haihusiki. Ingekuwa mtu kakosea kwa asilimia zaidi ya 50 japo sawa. Sio huo upuuzi unaofanyika, na wakati mwingine wasimamizi wa uchaguzi, huongeza herufi zao ili kupata sababu ya kumuengua mtu hasa wa upinzani.
 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imevitaka vyama vya siasa kuchagua watu makini ili kuepusha migogoro baina yao na Tume, pindi wanapotakiwa kukamilisha mchakato wa kupitisha majina ya wagombea.

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Semistocles Kaijage, wakati akizungumza na wadau wa vyama hivyo leo Agosti 1, 2020, jijini Dar es salaam, ambapo wamejadili Maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020, na mambo ya kuzingatiwa.

Amesema kuwa fomu za uteuzi zitaanza kutolewa Agosti 5, 2020, kwenye makao makuu ya ofisi za Tume jijini Dodoma kwa wagombea wa kiti cha Urais huku Wabunge na Madiwani watafuata fomu hizo katika makao makuu ya Halmashauri ya Majimbo na Kata husika.

“Fomu zitaanza kurejeshwa muda wowote pindi mgombea anapomaliza kujaza kwa usahihi hadi Agosti 25 saa 10 jioni, ambayo ndiyo itakuwa siku ya uteuzi, naomba mjaze kwa usahihi bila dosari yoyote ili usijekosa sifa na usiteuliwe na kuanza lawama”, amesema Jaji Kaijage.

Jaji Kaijage ameongeza kuwa, “Wale wote wenye malalamiko na tume tunaomba mtuletee wenyewe tutayafanyia kazi, ila sio kulalamikia mitandaoni hatutajihusisha na malalamiko ya mitandaoni”.

Ameongeza kuwa Tume imekamilisha uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura ambapo waliojiandikisha ni zaidi ya Milion 29 na kusisitiza kampeni za uchaguzi kwa Zanzibar zitaisha Oktoba 26,2020 ili kupisha upigaji kura ya mapema ya Rais wa Zanzibar, Mwakilishi na Diwani.
Mtuhakikishie kuwa wakurugenzi wa halmashauri hawatakimbia ofisi zao wakati wa kuchukua na kurudisha fomu, maana tunajua utawala wa awamu ya 5 ni waoga sana wa uchaguzi.
 
Tume makini ingesema kuwa wagombea wanaweza kupata ushauri kutoka kwa Tume kuhusu ukamilifu wa fomu zao. Ili kulinda demokrasia, ni wajibu wa Tume kuhakikisha wagombea wengi iwezekanavyo wanapata fursa ya kugombea.

Ningetegemea msimamizi anapo pokea fomu aipitie pamoja na mgombea na kumpa nafasi ya kusahihisha dosari zozote zinazoonekana kabla ya dirisha kufungwa.

Lugha za tusilaumiane hazipendezi.

Amandla....
Huu ni mtego wa panya sitoshangaa ya UCHAGUZI SM YAKIJIRUDIA UCHAGUZI MKUU...
 
Mfano wako mzuri sana. Nchi zilizoendelea mwalimu anahakikisha wanafunzi wana vifaa vya kuandikia. Na anakueleza mahitaji ya swali kwa sababu lengo la mtihani sio kukufelisha bali kupima uelewa wako.

Ndio maana mara nyingi unaruhusiwa kuingia na vitabu na calculator kwenye mtihani. Kwenye uchaguzi hatutafuti bingwa wa kujaza fomu bali mtu ambae wananchi wataona anafaa kuwawakilisha na kuwapigania.

Kumtoa mgombea kwa sababu ameandika Fundi Mchundo badala ya F Mchundo sio haki.

Amandla...
Inamaana hao wa Nchi zilizoendelea Walimu huwasaidia hadi kujibu mitihani?
 
Ndiyo,CHADEMA kuna mgombea chizi.
Angalia waweza kuwa unataka sifa au unasifiwa... ila ukichunga mdomo wako yaweza kuwa vema ili usitukanishe watu wenye hishma zao.
Je wanaojinadi ukichaa ni vichaa?
 
Inamaana hao wa Nchi zilizoendelea Walimu huwasaidia hadi kujibu mitihani?
Sijasema hivyo. Wanachofanya ni kuwaeleza wanafunzi mahitaji ya mtihani. Kwa mfano, kama mwanafunzi anatakiwa kutumia penseli badala ya peni kujibu maswali atawaambia hivyo na atahakikisha kila mwanafunzi ana penseli, na akikuona una tumia peni atakwambia usitumie na atakupa penseli. Kama mwanafunzi anatakiwa kuandika namba badala ya jina, atakusahihisha akiona umeandika jina lako. Hatakusaidia kujibu maswali kwa sababu hata kama umekosea kujibu swali ushiriki wako katika mtihani utatambulika.

Amandla...
 
Hivi tunachagua viongozi waende kutufanyia kazi za kujaza fomu au kuongoza na kuwaletea maendeleo?

Dosari za kujaza Fomu hazipaswi kuwa kigezo cha kuengua watu mahiri katika kutafuta nafasi za uongozi.

Kosa ktk fomu iwe Kama mjaza fomu kadanganya, au kaacha wazi maeneo muhimu. Lakini habari ya spelling ikipewa nafasi inatunyima haki ya kupata viongozi Bora. Na uwezekano wa fumu kiharibiwa Ni mkubwa.
 
Mchakato Huu ni sawa na ule wa uzabuni (Tendering). Bahasha haifunguliwi mpaka siku maalumu ya ufunguzi na ukaguzi iliyopangwa. Ndio maana wagombea wengine wanarudisha fomu siku ya mwisho wa mchakato kuzuia uwezekano wa siri zao za uongo walizojaza zisionekane wakawekewa mapingamizi. Vyama ndio vinatakiwa kuweka watu wa kuwasaidia wagombea wao kujaza fomu inavyotakiwa sio tume. Hiyo itakuwa sawa na kuitaka tume, ili kura zisiharibike, iweke watu wao vituoni kuwaelekeza wapiga kura namna ya kupiga kura zao. Mnataka kiingiza tume kwenye mgogoro wa kisiasa.
 
Back
Top Bottom