nabiidaniel
JF-Expert Member
- Feb 25, 2014
- 1,937
- 2,678
MKOANI TABORA
Wasimamizi wa mitihani ya NECTA ya Darasa la nne,kidato cha pili na cha nne walioitwa kwenye semina maalumu pale AMUCTA tarehe 15 na pale Themi Hill tarehe 17 wamelalamika kutolipwa posho za semina na nauli kwa kisingizio eti muongozo wa malipo haujatoka kutokea NECTA.
Wanasemina hao waliotoka vijiji Mbali mbali vya kanda maalumu kijiografia wamesikika wakilalamikia Hatua hiyo iliyowakera Sana kwani wengi wao wanatokea mazingira tata kijiografia na kiusafiri na kujikuta wakitumia nauli kubwa Sana kufika mjini TABORA wamelaani kukopwa Fedha hizo!
Kilichowakera zaidi ni kauli ya katibu tawala msaidizi kulopoka eti kukopwa ni sehemu ya siri ya semina hiyo eti wasiseme seme!
Wanasemina hao wametaka Tabia hiyo ikome na kama hawana uhakika wa kulipa semina hizo ni bora wasiwaite kwenye semina hadi taratibu za malipo zitakapokamilika!!
USHAURI
NECTA MUDA umefika Sasa wa kunitumia teknolojia kulipa wasimamizi, Fedha ziwekwe kwenye akaunti moja kwa moja ili kuepuka sarakasi hizi!
Kwamfano mnaweza agiza majina ya wasimamizi mapema hata mwezi MMOJA kabla mkaratibu malipo yao kabla ya semina kwa KUTUMIA taarifa za kitumishi kuliko kuwaaachia Halmashauri ambapo huzitumia kwa mambo BINAFSI kabla ya malipo!!
Wasimamizi hao wameilaumu Sana kamati ya mitihani ya mkoa kwa uzembe huo,Hadi wengine wachache walisusia kufika kwenye semina ya tarehe 17 na kuombwa kufika tarehe 22 ya mwezi HUU oktoba!
Nimeifikisha kama nilivyoipokea!katibu wa Baraza la mitihani makinika, wasimamizi Wana hasira kabla hata zoezi la usimamizi kuanza!HII itaharibu zoezi zima.
Yaani kama Dar Jamani wamezidi semina 50k Ila msishangae kulipwa 40k mkaambiwa elf10 mtalipwa nadai elf 10 zangu km mbili hivi na elf 5 piaNa wenyewe ndiyo kipindi chao cha mavuno hicho.
Taasisi za serikali zinaogopa sana teknolojia katika kutekelezwa majukumu yao!NECTA, wakitumia teknolojia ya malipo itaiokolea serikali ya Tanzania zaidi ya Bilion 900 zinazoibiwa na ofisi Za elimu mkoa na wilaya nchi nzima.
Hiki ni chanzo kikubwa cha wizi wa fedha Za serikali.
Pili ifike mahali sasa mitihani ya darasa la saba ifutwe Ili Wanafunzi wakurane na mtihani wa kidato cha pili na Kuendelea.
Wizi mkubwa na upotevu wa fedha ni mtihani wa darasa la saba nchini Tanzania.
Nasikia kwenye mtihani wa darasa la saba walilipwa semina 40000/= badala ya 50000/= HUKO Tabora pia nauli sh. 5000 wakati kuna wale wa kanda maalumu!Yaani kama Dar Jamani wamezidi semina 50k Ila msishangae kulipwa 40k mkaambiwa elf10 mtalipwa nadai elf 10 zangu km mbili hivi na elf 5 pia
Kiukweli kama wanasoma hapa wajue kabisa Maafisa elimu mradi wao mkubwa ni necta walimu wanapigwa Sana
Kwenye usimamizi mikoani kama shule Ina siku 11 wasimamizi mtalipwa Pesa ya siku 11 yotee bil shida hata km mko 10 ,Ila dar Sasa mnapunguzwa Kila siku mnajikuta mmebaki wawili au Mmoja wakati Necta wanatoa Pesa Kulingana na idadi ya siku na idadi ya vyumba Vya mitihani vilivyopo shuleni...
Sijuagi Hawa Viongozi wanatuhi saa ngapi hizi dhulma
Kwani mleta mada kuja na mapendekezo ya Namna ya kuzuia upigaji na kuepusha malalamiko kama haya amedhalilisha nini katika taaluma yake hata kama ni Mwalimu kweli!!?Waalimu wanajidhalilisha sana, tujifunze kutumia vizuri mitandao, njaa ya sh 5000 unadhalilisha taaluma nzima, na umeambiwa pesa zipo utalipwa, we tayari kwenye mitandao. Inaonyesha JPM haku wa displine vya kutosha, mnasababisha watu watamani JPM mwingine