NECTA Wasalimu amri, mitihan ya kidato cha 4 sasa kurudiwa upya.

Hahaha warudie hahaha haijatangazwa popote pale
 
Wakuu hebu msiwe walalamishi ktk kila jambo, kwa mwenye macho ataona kuwa ni kweli NECTA wamefanya uzembe ktk usahihishaji wa mitihani hiyo, kumbukeni hata madai ya waislamu ktk somo la islamic knowledge, ambapo baada ya kurudiwa tukashuhudia wanafunzi waliopata F wakapa B na wengine A kabisa na C, tukubali tukatae NECTA ni wazembe sana mfano pia kuna kituo cha mtihan kina wahitimu 600 lakin hakuna hata C zinazozidi 15.
 
wewe habari umezitoa wapi?

Mkuu usiwe mvivu wa kusoma, huko nyuma nimeandika source kuwa ni gazeti la habari leo uk 4, Pia kahama Fm wametangaza habari hii na kama we ni tomaso huamin mpaka uone subiria habari ya saa2 usiku uone.
 
Hata mimi napenda sana vijana wasiwe mitaani ni hatari sana, ila cha muhimu ni wao waje na SCIENTIFIC REASONS kwanini hali hii imejitokeza, kutokujua chanzo cha tatizo ni tatizo kubwa sana kuliko hata hilo tatizo lenyewe, hicho unachokisema kuhusu kushusha marks nahisi kimefanyika ila ndio hivyo tena bado hali ilikuwa mbaya wakaona hawana jinsi ni bora tu kutangaza kwanini huko chini wanaweza fanya hivyo washindwe kwa form 4, ila wasiwasi wangu wakifanya haya ya kushusha unaweza jikuta unaletewa wanafunzi sio tu kutokujua kuandika essay ila wasio jua kusoma kabisa kama tatizo hilo wanavyolalamika baadhi ya walimu wa sekondari, si unajua shule ni mwendelezo unapo mpitisha hapa ujue anakwenda ngazi nyingine
 
walekebishe na mishahara ya waalimau,pamoja na mazingira ya kufundishia,lasivyo watakuwa wanacheza malida each year! Chezea mateacheri ww.pamoja pamoja hadi kieleweke!

Mkuu hebu acha ujinga na harakati za kipumbavu yani we unasema hadi kielweke na wakati haya ni maisha ya watu, siku nyingine usirudie huu utumbo wako.
 

Inarudiwa kusahihishwa au kufanywa? Kama ni kufanywa huyo alieyamua hivyo atakuwa ana matatizo makubwa sana ya kimaamuzi
 
Hakuna uzembe wa kufanya wanafunzi zaidi ya 86% yaani Div 4 na ziro
 

Mkuu hapo umenena.
 
Kama hawataki kutatua matatizo ya waalimu wetu nina hakika bora ya leo make waalimu wameapa tena ama zao ama serikali ..
 
Mkuu hebu acha ujinga na harakati za kipumbavu yani we unasema hadi kielweke na wakati haya ni maisha ya watu, siku nyingine usirudie huu utumbo wako.
kwani hao walimu si watu ni ngendere? Cha msingi si quantity bali quality mnapenda matokeo kuwa yanachakachuliwa la saba wamechakachuo wakafaulu wengi kundi kubwa hawajui kusoma wala kuandika faida gani iliyopatikana?kwa mtu mwenye ufikiri mkubwa anaweza refer back matokeo ya form 2 kwa hao waliorudia ingekuwa wamepitishwa tu kuendelea kidato cha nne nini kingetokea zaidi ya hiki?
 

Vipi walioshinda ?, nao wapewe hii option au wasipewe.., ?, by the way wapewe wenye zero tu au wapewe wenye 2, 3 na four as well, na wawe na choice ya kuchagua ya mwanzo au ya sasa ?, By the way wapewe muda wa kujiandaa au wasipewe ?, this is not an easy task
 
Kama kweli mitihani itarudiwa hii itakua kali kuliko zote,maana ilitakiwa irudiwe kabla ya kutangaza.
Binafsi siungi mkono kurudia maana mdogo wangu alikua anapiga sana book na kapata 1:17 ilala sec,hivi ninavyoandika hapa yuko brussels kwa mapumziko ya miezi 4 na atarejea hapa two weeks before join advance.

Kwahiyo kama kuna mpango huo ntaenda mahakamani kupinga marudio ya mtihani!
 
Sijui kama wakirudia watafanya vizuri bila kuwepo maadalizi mazuri na ya muda wa kutosha ya kuwaandaa/kuwafundisha.
Hawawezi kurudia na mtoa mada katunga tu hana Source
Kinachoweza kufanyika ni kuteua ile % inayotakiwa kwenda Vyuoni na Vyuo Vikuu na hapo hawatajali Madaraja huenda wakachukua hata Div III na wale wa Div IV wakaenda vyuo vya kawaida

Kurudiwa kufanya Mtihani kusikowezekanika
Kuna baadhi ya Watahiniwa hawakufanya kabisa Mitihani, wako walioandika mitusi wako waliokosa Ada wakafutiwa matokeo sasa wote hao utawapata wapi saa hizi kwani wapo waliokuwa wakilala Mabwenini nk
 
Mtoa mada kasema sorce ni habari leo uk-4.
 
Hiyo habari si yakweli walichokieleza kwenye hilo gazeti ni kuwa wanafikiria kuwa saidia kulipia ada ya mitihani na bado hawajaamua, fuata link hii,
http://www.habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/9168-waliofeli-kusaidiwa
 

Mkuu Ukwaju acha kuishi kwa hisia.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…