NECTA Wasalimu amri, mitihan ya kidato cha 4 sasa kurudiwa upya.

NECTA Wasalimu amri, mitihan ya kidato cha 4 sasa kurudiwa upya.

Kutokana na ufahulu mbaya wa wanafunzi wa kidato cha 4 wa mwaka 2012, sasa mitihani hiyo kurudiwa upya na serkali itagharamia gharama zote na hii ni kwa ajili ya kuliepusha taifa aibu ambayo haijawahi tokea nchini kwa anguko la elimu.

Mods naomba msihamishe habari hii wala kunipiga ban, Mimi ni mjumbe tu na mjumbe siku zote hafi.
Mungu ibariki Tanzania.

Mjumbe anaweza kufa ila kwa hakika mjumbe hauawi.
 
tatizo sio kurudia mtihani kwanza ingekuwa vizuri watueleze sababu za kwanini matokeo haya yamekuwa mabaya, maana wanaweza sema paper irudiwe halafu wakawafaulisha wengi huku wakiwa hawana uwezo kama wanavyofanya huko darasa la saba na form 2, hicho kitakuwa kitu cha hatari sana kuliko hata haya matokeo maana tutakuwa na watu wengi wenye vyeti ila wasio kuwa na uwezo, bora ilivyo sasa tunatakiwa tuangalie tufanye nini kuboresha elimu sio tu watu kufaulu sana, ila je wankuwa na uwezo sawa kulingana na kiwango cha elimu?wasituchezee hao watatupa marks nyingi wkt kichwani ni zero wakati wao wanapeleka watoto wao kwenye ichi zenye elimu bora huku kwingine
je sisi tulifeli miaka ya njyuma itakuwaje? Au zero ya mwaka huu ni exceptioanl sana yaani wamepata 0 za point 38
 
Kama kweli mitihani itarudiwa hii itakua kali kuliko zote,maana ilitakiwa irudiwe kabla ya kutangaza.
Binafsi siungi mkono kurudia maana mdogo wangu alikua anapiga sana book na kapata 1:17 ilala sec,hivi ninavyoandika hapa yuko brussels kwa mapumziko ya miezi 4 na atarejea hapa two weeks before join advance.

Kwahiyo kama kuna mpango huo ntaenda mahakamani kupinga marudio ya mtihani!

Hahaa!ha CHAI CHUNGU bana. Eti yuko mapumziko. lini tutakesha tena kwa zile simulizi zako?
 
Last edited by a moderator:
je sisi tulifeli miaka ya njyuma itakuwaje? Au zero ya mwaka huu ni exceptioanl sana yaani wamepata 0 za point 38
Ndugu naomba usiwe mbinafisi sana na kujiangalia wewe tu, hapo hatuzungumzii zero ila tunazungumzia wingi wa ziro, yaani 60.7% ya watahiniwa wote unadhani ni hali ya kawaida hiyo
 
Mtoa mada kasema sorce ni habari leo uk-4.


Hiyo habari si yakweli walichokieleza kwenye hilo gazeti ni kuwa wanafikiria kuwa saidia kulipia ada ya mitihani na bado hawajaamua, fuata link hii,
http://www.habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/9168-waliofeli-kusaidiwa

mbona zote ndoto!!!! dancani kawafafanulia vizuri maana huwezi kurudia Mitihani
kuna shule za Kata huku Mbabala na Bihawana wanafunzi walipanga kwa wenyeji na wameshaondoka
Leo Aranblue ungeangalia kipindi cha Startv asubuhi usingeilaumu Wizara ya Elimu
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom