kweli,km necta ni mkweli,basi waandishi ni makanjanja. Ilihitaji dk kama kumi tu na resources kidogo,kufanya research ya baadhi ya mambo.mfano kujua km mwanafunzi Y amewekewa matokeo au laa!,ni swala la pale news room kuconfirm kwenye mtandao. Pia mwandishi alipashwa kuwasikiliza na upande wa pili,yaani necta wao wana data gani! Kweli hapa wameingizwa cha kike!
Who to believe! Baraza la mitihani au Mkurugenzi wa shule.
Kama haya ya kwenye press release yatakuwa ni kweli kama inavyoonyesha. Huu utakuwa ni uzembe wa hali ya juu na kama sivyo, basi wahariri wanafahamu vizuri nia na madhumuni ya kuandika habari zilizopinda kwa manufaa ya wanaowafahamu wawo.
Inashangaza mambo ya msingi kabisa ya uandishi yanawekwa pembeni au kuwa overlooked. Kwani kulikuwa na gharama gani ya kuhakiki kama maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Mkurugenzi wa shule ni sahihi.
Tanzania Daima linaanza kuonyesha kama liko desperate kwa 'mission' mpaka wahariri wanasahau majukumu yao ya msingi kabisa. Katika wiki moja limekuja na madudu ambayo habari zake bado ni sensitive nchini.
Tanzania Daima kwa mara nyingine linajiingiza kwenye kuchapisha habari bila utafiti wa kutosha!!!
Rejea mleta mada amesema: "Kufuatia habari zilizoandikwa kwenye magazeti zikinukuu tuhuma za makosa ya NECTA katika mitihani ya wanafunzi wa shule hiyo. Baraza la mitihani limetoa jibu rasmi". Sasa wapi Tanzania Daima imetajwa?? Naheshimu sana sana mada zako Ze Marcopolo, lakini sasa naona unataka kutulisha maneno yako, hatudanganyiki!!!
Shikamoo mama yangu mdogo. Samahani kwa kuraise eye brows zako, lakini mpendwa mama mdogo naomba usome taarifa ya NECTA sentensi ya kwanza. Narudia tena mpendwa mama mdogo samahani kwa kukukwaza, sio lengo hata kidogo kumkwaza mama yangu mdogo.
Marahaba mdogo wangu!!! Ndiyo haswa umeenda nilikotaka useme, pale pametajwa gazeti la Tanzania Daima na Mtanzania, kwa nini umeshupalia Tanzania Daima??? Why? Why? Why?
Mkuu wangu mama mdogo, nakupa heshima yako kwa mara nyingine na kukuomba tena msamaha kwa kukukwaza. Katika post yangu ya awali kuhusu Tanzania Daima kuna neno TENA. Neno hili ndio key word (neno funguo). Gazeti hilo la chadema liko kwenye mahojiano na polisi juu ya habari ya uchochezi inayohusu vurugu za Geita. Kabla hata hayo hayajaisha linakuja tena na "technical error" nyingine.
Naheshimu sana michango ya vyombo vya habari katika kutoa ajira na habari kwa umma, lakini weredi ni jambo la msingi katika fani hii ya uandishi kama jinsi ilivyo kwa fani nyingine.
Hata hivyo najisikia vibaya kukukwaza mama yangu mdogo na nitajitahidi nisiwe nakukwaza tena. usichoke kunikumbusha mwanao ninapokukosea, ndio u-mama wenyewe huo. nakutakia weekend nyororo. Tuendelee kuwa pamoja...
Ze Marco Polo, sasa umeeleweka, kwa mchango wako wa kina changanya na hii kutoelewka kulikokuwa kumetokea, nakupa hii poster ya ujumbe wa leo ikupoze!!. Tuko pamoja!!
View attachment 84242
Acheni siasa/porojo za vijiweni
kwenye mambo ya kitaalam
kama elimu, tuachieni
wataalam tujadili na
kurekebisha dosari
zilizosababisha kufeli kwa form
four 2013! Nashangaa
MALUMPENI wamekurupuka
from no where kila mtu na
hoja zake dhaifu za vijiweni
mmesomea wapi ualimu au
mnadhani walimu
wanachaguliwa kwa kufumba
macho na kunyosha mikono
juu!!
Binafsi siwezi kuwapongeza NECTA moja kwa moja wala kumnyooshea kidole Mkurugenzi wa GREEN ACRES pia.
Ni juzi juzi tu tulishuhudia NECTA wakikosea utoaji wa matokeo ya somo la "Elimu ya Kiislamu", hivyo hata wao sio kuwa wapo makini kiasi cha kutoweza kukosea la hasha.
Pia kwa wale wenzangu mnaovinyoosha vidole vyenu kuyaelekea magazeti tajwa nadhani mtakuwa mnakosea kwa kiasi fulani. Radio, televisheni, magazeti n.k vyote ni vyombo vya habari. Kilichofanywa na magazeti haya ni kujaribu kuichokonoa NECTA ibainishe kupitia taarifa ya Bw. Julian, hivyo huwezi kuyatia hatiani magazeti hayo kwani wao hawakuwa chanzo kikuu cha Habari. Kwa kulitambua hilo ndio maqna hata NECTA imenyoosha kidole chake kukanusha taarifa iliyoandikwa(iliyotamkwa na Bw. Julian).
mitandao iko wazi kabisa wangeangalia dak 5 tu wange ignore press conference ya huyo Mkurugezi wa Shule hiyo!