NECTA yatangaza matokeo ya kidato cha nne 2024. Yatazame hapa!
Wazo la kuanzisha Shule za kata ni zuri sanaa, na mimi ni moja ya zao hilo. Shida iliyopo ni kwamba zinatumika ku-accomodate wanafunzi wengi ambao hawajui wanafuata nini shuleni. Jaribu kufuatilia suala hili fungua matokeo ya shule nyingi za kata, utagundua wanafunzi wengi sanaa waliopata Div IV na Div 0 ni wale waliosoma Masomo ya Arts tuu. Lakini ukichunguza Div I hadi Div III , zilizo nyingi zinatoka kwenye masomo ya Sayansi au masomo ya Biashara
Kwani wanaosoma arts hawajui ni nini walifuata shuleni mkuu?
 
We need to see some invention from those schools that can impact the globe.
Hivi Kuna mdada yeyote st Francis akafanya wonders kweli jamani, mie naweza nikafundisha akawa innovative ama akafaulu ili nikazidi kuaminika na wateja wangu wazidi kuniletea pesa. Jamani pesa inatafutwa kwa namna yoyote Ile hata kuua unaua sembuse ku maintaining best performance kweli nizidi kuwa na wateja lukuki yaani wawe wananigombania, yaani ni biashara as usual, otherwise show us st Francis wamefanya nini la ajabu la ku reflect matokeo yake, badala yake tunaona kayumba waki make ndege ama helicopter
Huna Akili....
Selfish and Self Centered..
🚮🚮🚮

Baki na upumbavu wako
 
Kila mmoja aangalie matokeo ya shule St. Francis girls.
Wote wana division one ya point 7 *****
 
Hivi kitendo cha serikali kudai kuwa eti wanafunzi waliopata divisheni foo wamefaulu, inatuchukuliaje sisi wananchi wakati uki score divishen foo hata cheti hupati?
 
Kuna shule hapo mtaani huwa inasifika kuwa wengi wa wanafunzi wake hutumia mibange, imezungusha haswa! 😥
Shule gani hiyo mkuu? Sio Kinyerezi Secondary School? Maana ile ni kama shule ya mazombie!
 
Nilisoma St. Kayumba, matokeo si haba, nimejaribu kufuatilia wale niliomaliza nao wapo wapi siku hizi nakuta almost wote tuliomaliza na kujitahidi si haba Mungu ametujaalia huko mbeleni hakuna aliyepotea kwenye Radar. Ujumbe wangu ni huu, hawa waliofaulu St. Kayumba wana-possibility kubwa sanaa ya kuja kufanya vizuri iwapo hawatozembea. Sizisemi vibaya shule za private lakini ninao ushuda wa jamaa wawili waliomalizaga St. Lakini walipokuja kujiunga kwenye St kayumba matokeo ya Six walizungusha. Nilishangaa sanaaa.
Tatizo ni kwamba shule za St huwa wana spoonfeed wanafunzi wao. Wanafunzi hawakuzoea kujitafutia wenyewe. So ukimleta mtoto wa aina hiyo kwenye shule ya A level ya Kayumba lazima atage (0). Ni sawa na kumchukua kuku broiler umchanganye na kuku wa kiswahili. Atakufa tu kwa kuwa hajazoea hustles.

Njia nzuri ya kudeal na mwanafunzi wa St, mwache asome huko huko hadi A level. Akifika UD atakuwa anajitambua, atapambana mwenyewe.
 
Trust me wengi wamesoma huko as Center of exam lkn sio sehemu ya kukusaidia kufaulu wengi hata hawaendi wanashinda tuition za mwenge,mchikichini na huko mitaani pia,kayumba ni kwenda kufanya mock exams/necta only
Kwa mzazi anayejitambua, hili ndilo jambo analotakiwa kulizingatia kama hataki mtoto wake atage kwenye mtihani wa mwisho.
 
Kwani wanaosoma arts hawajui ni nini walifuata shuleni mkuu?
Wengi wao ni wasindikizaji, fungua matokeo ya Shule yoyote ya Kata ambayo Ina masomo ya Sayansi na Arts, au yote(Sayansi, biashara na Arts) Kisha fuatilia ni wepi wamefaulu faulu na wepi wameongoza KWA ku-fail
 
Necta website ina shida gani wakuu, pamoja na webisite ya wizara ya elimu zinagoma kufunguka kabisa
 
Back
Top Bottom