FRANCIS DA DON
JF-Expert Member
- Sep 4, 2013
- 38,920
- 44,970
- Thread starter
- #201
Hali ya mgao ni mbaya sana, zimebaki siku 39
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Lakini tumeshaambiwa hata likianza kuzalisha umeme hakuna kitakachobadilika hasa kuhusu bei ya umeme. Itabaki ile ile. Usishangae hata mgawo ukaendelea. Hii nchi haieleweki tunakwenda mbele au tunarudi nyuma.Kabla ya yote turudi darasani kidogo, maana sitaki tuanze kuulizana maswali obvious , mara sijui source ni ipi, nk. haya twende kazi.
Unit moja ya umeme hapa Tanganyika inauzwa kwa wastani wa shs. 600/=. Unit moja ya umeme ni kitu wanaita Kilowatthour (KWh). Kilowatthour ni nini hasa? Kilo inamaanisha ‘Maelfu’ (thousands , 000), Watt ni neno linalowakilisha kiwango cha nguvu (power), in this case ni nguvu ya umeme. Sasa hour ni lisaa (dakika 60).
Kwa mantiki hiyo, Unit moja ya umeme (1KWh), ni kipimo cha kiasi cha umeme ambacho kama utautumia kufanya kazi inayohitaji ‘power’ (nguvu) ya watts 1000 , basi unit hiyo itaisha baada ya lisaa limoja (dakika 60).
Haya sasa, tuliza akili halafu twende taretibu. Bwawa la Nyerere linatajwa kuweza kuzalisha Megawatt 2100. Hii inamaanisha nini?
Mega ni neno linalomaanisha millions (000,000), hivyo kwa tafsiri rahisi kabisa, bwawa hili linauwezo wa kuzalisha nguvu (power) ya umeme ya Watts ‘MILLION 2100’ , tukitaka kuiweka kati Kilowatts, tunagawanya hiyo namba kwa ‘1000’ , ambapo tunapata kwamba hilo bwawa linazalisha umeme wenye nguvu ya KILOWatts MILLION 2.1.
Hadi hapo tupo pamoja naamini, maana wewe unaesoma hapa naamini unaakili walau za kuemdea chooni, hivyo lazima hadi hapo umenielewa. Sasa basi , tubadilishe hicho kiwango kuwa ‘Killowatt hour’ (KWh) ambayo ndio unit moja ya umeme sasa.
Mashine za kufua umeme huo wa 2.1 million Kilowatts, zikizalisha umeme kwa muda lisaa limoja, maana yake tumezalisha Unit za umeme zipatazo Million 2.1 , yaani 2.1 million Kwh.
Unit moja ya umeme hapa Tanganyika ni 600/=; sasa kwa unit milioni 2.1, unapata milioni 1,260 ; ambayo ni bilioni 1.26 kwa lisaa. Hivyo basi kwa masaa 24 (siku 1), mitambo inazalisha umeme wenye thamani ya shillingi bilioni 30.24; kwa mwezi ni mara 30 ya hiyo, ambayo tunapata wastani wa Trillion 1 kwa mwezi.
Sasa kwa miezi 12 tunafanya mara 12, hivyo tunapata Trillion 12 kwa mwaka, ambayo ni 50% ya makusanyo yote ya TRA kwa mwaka mzima.
Sasa cha ajabu, huo umeme utauzwa nje, na bado watoto kule kondoa wataendelea kukalia vumbi darasani kwa ukosefu wa fedha za kununulia madawati, huku kesi za ICSD dhidi ya Tanesco wanazojishtaki wenyewe zikiendelea kupamba moto.
Bishana na data (Hoja), usibishane na mimi.
=========================
Serikali: Tumedhamiria kuzalisha umeme mwingi, ziada tutauza nje ya nchi
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa leo September 20, 2023 amefungua Kongamano la Tano na Maonesho ya Nishati Tanzania na amesema kwamba Serikali imedhamiria kuwa Mzalishaji mkubwa wa nishati na kuwa na umeme wa kutosha utakaopatikana kwa urahisi na nafuu na ziada itauzwa nje ya Nchi...www.jamiiforums.com
Lakini tumeshaambiwa hata likianza kuzalisha umeme hakuna kitakachobadilika hasa kuhusu bei ya umeme. Itabaki ile ile. Usishangae hata mgawo ukaendelea. Hii nchi haieleweki tunakwenda mbele au tunarudi nyuma.
Tufanye 400/=, bado ni kama Trillion 8 hivi..Umeme wq gharama bongo ni huu tunanunua 357 kwa unit,
Huko viwandan wenye matumizi makubwa wananunua kwa 150-80/unit,
Huo wastan wa 600 umeupata wapi ?
Mpuuzi tu yule,Hilo genge ni hatari Kwa nchi.Maharage asema Bei haitashuka hata bwawa likianza KAZI!!
1.) Ukame wa muda mfupi hauwezi kuleta athari katika uzalishaji hata kidogo, maana reservoir ni kubwa mno, infact lile ni ziwa, ni sawa na kusema ziwa victoria lipungue sababu ya ukame, its absolute nonsense.Mkuu sio kila uzalishaji utakuwa sawa kama hesabu zako .
1. Kwanza kupata zote 2100MW kutategemea upatikanaji wa Mvua .Mvua isipokuwa ya kutosha hatuwezi kupata maxmum capacity .. Pia fahamu tukipata ukame kwa miaka kadhaa tunaweza kushindwa kuzalisha umeme kabisa . Mungu aepushie mbali.
2. Kuna Umeme unaopotea kutokana na mambo kadhaa , kutokana na machine losses kutokana na frinction, heat na conversion hizo zinaweza kuwa mpaka 10%.
3.Pia kuna umeme utakaopotea kutokana na upotevu kwenye miundo mbinu ya usafirishaji, Kwa sasa upotevu ni almost 25%.
4.Pia upo upotevu kwenye matumizi na wakati mwingine umeme kuzalishww bila kutumika.let say 10%
5.Pia kumbuka bei ya umeme sio 600Tshs kama ulivyosema .
6. Kuna Machine maintenance and operation time ambayo nayo itapunguza uzalishaji almost 5%
Kama JNPP itakuwa kwenye uzalishaji wake wa kiwango cha juu tutegemee kiasi cha 50% cha uzalishaji kuwa ni mapata … Less than 4T kwa mwaka
Fanya hesabu upya
Mkuu naomba nisome tena .1.) Ukame wa muda mfupi hauwezi kuleta athari katika uzalishaji hata kidogo, maana reservoir ni kubwa mno, infact lile ni ziwa, ni sawa na kusema ziwa victoria lipungue sababu ya ukame, its absolute nonsense.
2.) Losses za heat kuwa 10% zinaweza kupunguzwa significantly kwa kusafirisha umeme unaoenda mbali kwa kutumia higher voltages zaidi.., hili lifanyike.
3.) Unaposema 25% inapotea kwenye miundo mbinu unamaanisha wizi wa umeme sio? Kama unaibiwa hiyo haipunguzi thamani ya umeme uliozalishwa, uwe unaibiwa au kutumikaje its irrelevant, kikubwa umezalishwa umeme wa thamani hiyo.
4.) Upotevu kwenye mafumizi unamaanisha nini? Kuzalishwa bila kutumika ni jambo linaloweza kuepukika kwa kushusha bei ya umeme, hadi vijijini kule Haubi kwenye baridi wachemshe maji kwa kutumia heater za umeme, tuone huo utakaobaki bila kutumika ni upi..
5.) Bei ni generaliseation.., wapo wanaolipa chini ya hapo pia, huo ni wastani..
6.) Kuna mashine redundant ambazo huwashwa ili kuziba pengo la zile zinazofanyiwa maintanance..
Ikipungua sana ni Trillioni 10, tunataka tuone hizo pesa zimeenda wapi!!!!
1.) & 2.) Sawa, ila hiyo 10% kama ni Tranmission losses kama ulivyosema, inaweza kuondolewa kwa kusafirisha umeme unaoenda mbali kwa kutumia msongo mkubwa zaidi. Na hiyo 25% inayopotea kutokana na voltage drop ya uchakavu wa miundombinu ni kitu kinachorekebishwa tayari, matrillion yalishatengwa kwa ajili ya kuboresha miundo mbinu chakavu, sio kitu inherent kwamba lazima kiwepo.Mkuu naomba nisome tena .
1. 2100MW ni maximum capacity ya 9 Engine Turbine , Ambayo kila moja inakadiliwa kuwa na max 235MW. Ukiambiwa hivi maana yake uzalisha mara nyingi unakuwa 90% ya kiwango cha juu. wasomi wa umeme tunajua tunaita power factor
2. Utafiti uliofanywa na wabobezi kutoka chuo kikuu cha Dar es salaam ulibaini kuwa 25%ya kile kinachozalishwa kinapotea njiani kama losses na voltage drop kutokana na miundo mbinu chakavu na iliyopitwa na wakati.
3. Sio kila kinachozalishwa kipo kinachopotea bila kutumiwa.
Kuhusu bwawa kukauka na kushindwa kuzalisha umeme kwa kiwango kinachohitajika pia inawezekana. Maana kuna minimum level ya maji inahitajika ili kuzalisha umeme, chini ya hapo hata kama maji yapo hawawezi zungunsha turbine
Hii ni kitaalamu zaidi inahitaji shuke kuelewa. so almost 50% ya kinachozalishwa kitapotea bila kuwa mapato.
karibu mkuu
W we 3nUnamwambia nani sasa, mimi ndio Tanesco? Mimi nimeleta hoja yangu kama mwananchi mfuatiliaji, jadili hoja yangu..
Hilo Bwawa likifanya kazi hata kwa 50% ya uwezo wake unidai!Hali ya mgao ni mbaya sana, zimebaki siku 39
Nadhani lengo ni kuhakikisha bei haishuki kwa kulimit supply isizidi current demandHilo Bwawa likifanya kazi hata kwa 50% ya uwezo wake unidai!