Nembo ya Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam na maneno yaliyoko katika logo hiyo ni vitu vya kutazamwa upya kwani viko kisiasa zaidi kuliko kitaaluma

Nembo ya Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam na maneno yaliyoko katika logo hiyo ni vitu vya kutazamwa upya kwani viko kisiasa zaidi kuliko kitaaluma

Hekima haifundishwi popote duniani! Kazi ya msingi ya chuo kikuu chochote ni kufundisha, tafiti, na ushauri. Nani duniani humu amewahi kufikia "Hekima ya Sulemani"? Alisomea chuo kikuu kipi kuipata hekima ile? UDSM ijikite kwenye majukumu yake ya msingi badala ya kuambatana na siasa uchwara!
Mkuu samahani kwa kauli hii, ningependa kujua elimu yako ni kiwango gani?
Kama umefikia elimu ya shahada ya kwanza kuna kitu hakiko sawa ktk mfumo wako wa kujifunza ukiwa shuleni na vyuoni.

The wisdom in philosophy
From the Latin sapientia, it relates to intelligence, in the opinion, common sense, prudence, knowledge, science, philosophy. Wisdom is commonly used to describe the character of that which is reasonable, or to exercise moderation in desires.
Source: What is Wisdom ? Philosophical Definition

Ukisoma hapo kwenye nini maana ya wisdom(hekima) utaona inahusiana na vitu vingi ikiwemo na knowledge, science na phylosophy.

Je elimu ya chuo kikuu lengo lake sio kukupatia knowledge?
Je kazi ya chuo kikuu sio kukupa mbinu za kisayansi na kutambua asili ya vitu kisayansi?
Au kutafuta majibu ya vitu mbalimbali au changamoto mabalimbali zinazo ikabili jamii au dunia kwa njia za kisayansi kupitia hizo tafiti (research) unazo sema?

Go back to the college mkuu wangu.
 
hiyo picha ya mwenge ni uchuro tu hapo na ndiyo maana inazalisha wazee wa jalalani.
Huelewi hapo maana yake Ni the book that has strong light that shines.

Ukiweka litabu kubwa mwanga mdogo maana yake Ni hopeless the book that has no light and that does not shine

Wasomi wa UDSM wanna shine Sana maraisi wengi wameputia UDSM was kwetu na was nchi zingine

Nembo la chadema halina mwenge ndio maana ha li shine
 
Mkuu samahani kwa kauli hii, ningependa kujua elimu yako ni kiwango gani?
Kama umefikia elimu ya shahada ya kwanza kuna kitu hakiko sawa ktk mfumo wako wa kujifunza ukiwa shuleni na vyuoni.

The wisdom in philosophy
From the Latin sapientia, it relates to intelligence, in the opinion, common sense, prudence, knowledge, science, philosophy. Wisdom is commonly used to describe the character of that which is reasonable, or to exercise moderation in desires.
What is Wisdom ? Philosophical Definition

Ukisoma hapo kwenye nini maana ya wisdom(hekima) utaona inahusiana na vitu vingi ikiwemo na knowledge, science na phylosophy.

Je elimu ya chuo kikuu lengo lake sio kukupatia knowledge?
Je kazi ya chuo kikuu sio kukupa mbinu za kisayansi na kutambua asili ya vitu kisayansi?
Au kutafuta majibu ya vitu mbalimbali au changamoto mabalimbali zinazo ikabili jamii au dunia kwa njia za kisayansi kupitia hizo tafiti (research) unazo sema?

Go back to the college mkuu wangu.
Naomba nitofautiane na wewe; lengo la msingi la chuo kikuu ni kupata KNOWLEDGE not WISDOM! Ni kupata MAARIFA sio HEKIMA! Hakuna mahali popote darasani uliwahi kukaa ili ufundishwe HEKIMA; tunaingia darasani kupata MAARIFA. Huwezi kuniambia wote ambao hawajafikia elimu ya chuo kikuu au ambao hawajasoma (darasani) kabisa hawana HEKIMA!

"Where is the wisdom we have lost in knowledge? Where is the knowledge we have lost in information?" —T.S. Eliot. Knowledge is gathered from learning and education, while most say that wisdom is gathered from day-to-day experiences and is a state of being wise. Knowledge is merely having clarity of facts and truths, while wisdom is the practical ability to make consistently good decisions in life.
 
Huelewi happy maana yake Ni the book that has strong light that shines.

Ukiweka litabu kubwa mwanga mdogo maana yake Ni hopeless the book that has no light and that does not shine

Wasomi wa UDSM wanna shine Sana maraisi wengi wameputia UDSM was kwetu na was nchi zingine

Nembo la chadema halina mwenge ndio maana ha li shine
umeandika ugoro mtupu
 
Habari wakuu,

Binafsi napenda kushauri viongozi wa Chuo hiki kuitazama upya nembo ya chuo kama kweli nembo hiyo inastahili kubaki kama ilivyo au ifanyiwe marekebisho madogo ili iwezeke kusadifu zaidi maswala ya academic kuliko ilivo sasa ambapo,kwa mtazamo wangu,inasadifu zaidi siasa za miaka ya nyuma.

Naposema imekaa kisiasa zaidi simanishi haibebi ujumbe wowote wa kitaaluma, bali ni kwasababu imetoa nafasi kubwa kwa maswala ya kisiasa {mchoro wa Mwenge} kwenye nembo huku mchoro wa kitabu ukipewa nafasi ndogo wakati kazi ya msingi ya chuo ni kuzalisha wataalamu.

Nachojiuliza,mchoro wa Mwenge kwenye nembo ya taasisi inayotoa taaluma inasaidifu nini? Inawezekana nembo ya chuo hiki ni ile ile tangu uhuru hivyo kwa wakati huo, labda kulikuwa na sababu ya kuweka mchoro wa mwenge katika nembo ya chuo ila sidhani kama ni sahihi kuendelea kuwa na mchoro huo kwa wakati tulionao.

Ukiacha mbali swala la mchoro huo wa mwenge,hata maneno yaliyoko katika slogan hiyo nayo sidhani kama yana uhusiano wowote na chuo hicho ambacho kazi yake kubwa ni kuzalisha wataalam(wasomi).

Maneno yaliyoko katika nembo hiyo ni haya:hekima ni uhuru.

Nembo husika ni hii:


Kwa maneno hayo ambayo bila shaka ndio kauli mbiu ya chuo,ni wazi yanaturudisha kule kule kwenye mchoro wa mwenge wa uhuru jambo linalonifanya nijiulize ilitokea tu kama coincedence au ni jambo lililokuwa limekusudiwa?

Nadhani wakati umefika nembo hii itazamwe upya na ifanyiwe marekebisho madogo ingawa jambo hili nalo linaweza kuwa na changamoto zake ingawa sitaki kuamini changamoto hizo ndio zinaweza kuwa kikwazo zaidi tu ya kukosekana dhamira ya kuifanyia mabadiliko nembo hiyo na pengine ni kwakuwa tumeridhika nayo,tumeizoea na hatuoni kasoro yoyote katika hiyo nembo.

Hembu tazameni nembo ya chuo hki kichanga lakini inayosadifu zaidi taaluma kuliko mambo mengine yote katika nembo hiyo bila kusahau uchaguzi mzuri wa maneno yaliyowekwa katika nembo husika.


Jambo hili inawezekana liko hata katika taasisi nyingine lakini haimanishi tukae kimya.

Kama wahusika mpo humu,basi tupeni ufafanuzi wa hiyo logo na hiyo kauli mbiu(moto) labda tunaweza kuelewa.
Wivu tu kwa ambao hawakubahatika kusoma UDSM.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tasfiri yake MTU aliyeelimika huwa na hekima hekima maana yake ukiwa na maarifa utakuwa huru.MTU aliyesoma apaswi kutembea gizani bali nuruni,ukiwa na hekima upo nuruni
HEKIMA inachangiwa na vitu vingi sio elimu ya darasani peke yake; na wala hakuna shule au chuo chochote kinachofundisha HEKIMA. Jukumu la msingi la chuo kikuu chochote ni kutoa MAARIFA so slogan ya UDSM iendane na jukumu lake la msingi - MAARIFA. HEKIMA ni matokeo ya vitu vingi katika maisha na sio elimu ya darasani peke yake!
 
Wale ambao hamjakutana na mtaara wa hekima piteni kimya kimya m like hapa.
Mengine tutajua mbele kwa mbele.
 
HEKIMA inachangiwa na vitu vingi sio elimu ya darasani peke yake; na wala hakuna shule au chuo chochote kinachofundisha HEKIMA. Jukumu la msingi la chuo kikuu chochote ni kutoa MAARIFA so slogan ya UDSM iendane na jukumu lake la msingi - MAARIFA. HEKIMA ni matokeo ya vitu vingi katika maisha na sio elimu ya darasani peke yake!
Una hoja ya msingi sana mkuu.Wahusika waitafakari.
 
Hata hiyo ya tumaini ni same kwa muktadha wako maana msalaba ndio mkubwa kuliko vyote hivyo ni kisiasa za kidini au?!
 
Kuhusu alama ya mwenge wa uhuru (Torch of Freedom) au (Uhuru Torch)
Nyerere alikuwa anawaza mbali sana.
Yule mtu alikuwa mwanafunzi wa falsafa ktk maisha yake.

Ukiachana na maneno yake kuhusu sababu za kuwasha mwenge siku ya Uhuru na Mzee Nyirenda kwenda kupandisha juu ya kile cha mlima Kilimanjaro, kulikuwa na ujumbe mwingine Nyerere anautuma kwa lugha ya picha ya mafumbo.

Naweza kusema ule mwenge ni ujumbe katika lugha hiyo hapo juu ambayo niite ni metaphorical kwa kimombo.

Kwa kufupisha ule mwemge unatoa mwanga, mwanga katika fikra. It is a symbol of enlightenment.
Ni kwamba Nyerere alikuwa anaturudisha kifikra ktk zama za Enlightenment (Age of Enlightenment).
Enlightenment maana yake ni UFUNUO wa fikra.

Enlightenment (Ufunuo wa fikra) ni muunganiko wa dhana mbalimbali zilizo jikita katika masuala ya uhuru wa kuhoji au kudadisi (reasoning) na ushuhuda wa hisia kama vyanzo vya msingi vya maarifa na dhana za juu kabisa kama za Uhuru, maendeleo, uvumilivu, undugu, serikali za kikatiba na kutenganisha serikali(dola) na dini.

Kizungu tunasema:
"The Enlightenment included a range of ideas centered on the sovereignty of reason and the evidence of the senses as the primary sources of knowledge and advanced ideals such as liberty, progress, toleration, fraternity, constitutional government and separation of church and state." source : Age of Enlightenment - Wikipedia

Utaona hayo yote juu ni maaana au tafsiri ya University wakati huo zina anzishwa kule dola ya kirumi. Sisi tumeiga tu.

Natamani sasa wabobezi kama akina Prof Mukandala waje wanirekebishe na kuichambua vizuri hii hoja yangu.

Maana mimi ni mchanga sana kielimu na ni mtu wa sayansi hii ya hisabati, na tehama sio haya mavitu makubwa.
 
Back
Top Bottom