Nembo ya Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam na maneno yaliyoko katika logo hiyo ni vitu vya kutazamwa upya kwani viko kisiasa zaidi kuliko kitaaluma

Nembo ya Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam na maneno yaliyoko katika logo hiyo ni vitu vya kutazamwa upya kwani viko kisiasa zaidi kuliko kitaaluma

Naomba ufafanue iko sawa kivipi.
Logo ya chuo kikuu haiwezi kuwa Kama ya shule ya msingi au shule ya upili ya kuanza kuongelea education tu au Maarifa tu. Chuo kikuu lazima ujumbe wa logo yake uwe na maana pana. Na ndivyo ulivyo ujumbe wa chuo kikuu. Kumbuka hiki ni chuo cha kihistoria nchini mwetu. Cha kwanza kutoa elimu kwa wazalendo bila ubaguzi.
 
Salary Slip ana hasira na CCM, Sasa anajisahau na kuleta hadi kwenye maswala yasiyohitaji CCM wala UKAWA.
 
“He who learns must suffer. And even in our sleep pain that cannot forget falls drop by drop upon the heart, and in our despair, against our will, there comes wisdom to us by the awful grace of God”
(Aeschylus)
 
Ahaha Wengi mtaani wanasemaga ni freemason mara blah blah kibao..

Skia ni ivi...


Wakati wana waisraeli walivyo kua Safarini kuelekea nchi ya Ahadi mnakumbuka Kuna kisanga kilitokea pale Musa akaambiwa achukue nyoka amtundike mtini iwe kama ishara ya Uponyaji na Kila aliye Mtizama Kwa imani ya Kupona Alipona na Kuishi


HES. 21:8-32

Bwana akamwambia Musa, Jifanyie nyoka ya shaba, ukaiweke juu ya mti, na itakuwa kila mtu aliyeumwa, aitazamapo ataishi. Musa akafanya nyoka ya shaba, akaiweka juu ya mti, hata ikiwa nyoka amemwuma mtu, alipoitazama ile nyoka ya shaba, akaishi
Hiyo alama ya nyoka kwenye nembo ya Tumaini ina maanisha nini?
 
Habari wakuu,

Binafsi napenda kushauri viongozi wa Chuo hiki kuitazama upya nembo ya chuo kama kweli nembo hiyo inastahili kubaki kama ilivyo au ifanyiwe marekebisho madogo ili iwezeke kusadifu zaidi maswala ya academic kuliko ilivo sasa ambapo,kwa mtazamo wangu,inasadifu zaidi siasa za miaka ya nyuma.

Naposema imekaa kisiasa zaidi simanishi haibebi ujumbe wowote wa kitaaluma, bali ni kwasababu imetoa nafasi kubwa kwa maswala ya kisiasa {mchoro wa Mwenge} kwenye nembo huku mchoro wa kitabu ukipewa nafasi ndogo wakati kazi ya msingi ya chuo ni kuzalisha wataalamu.

Nachojiuliza,mchoro wa Mwenge kwenye nembo ya taasisi inayotoa taaluma inasaidifu nini? Inawezekana nembo ya chuo hiki ni ile ile tangu uhuru hivyo kwa wakati huo, labda kulikuwa na sababu ya kuweka mchoro wa mwenge katika nembo ya chuo ila sidhani kama ni sahihi kuendelea kuwa na mchoro huo kwa wakati tulionao.

Ukiacha mbali swala la mchoro huo wa mwenge,hata maneno yaliyoko katika slogan hiyo nayo sidhani kama yana uhusiano wowote na chuo hicho ambacho kazi yake kubwa ni kuzalisha wataalam(wasomi).

Maneno yaliyoko katika nembo hiyo ni haya:hekima ni uhuru.

Nembo husika ni hii:


Kwa maneno hayo ambayo bila shaka ndio kauli mbiu ya chuo,ni wazi yanaturudisha kule kule kwenye mchoro wa mwenge wa uhuru jambo linalonifanya nijiulize ilitokea tu kama coincedence au ni jambo lililokuwa limekusudiwa?

Nadhani wakati umefika nembo hii itazamwe upya na ifanyiwe marekebisho madogo ingawa jambo hili nalo linaweza kuwa na changamoto zake ingawa sitaki kuamini changamoto hizo ndio zinaweza kuwa kikwazo zaidi tu ya kukosekana dhamira ya kuifanyia mabadiliko nembo hiyo na pengine ni kwakuwa tumeridhika nayo,tumeizoea na hatuoni kasoro yoyote katika hiyo nembo.

Hembu tazameni nembo ya chuo hki kichanga lakini inayosadifu zaidi taaluma kuliko mambo mengine yote katika nembo hiyo bila kusahau uchaguzi mzuri wa maneno yaliyowekwa katika nembo husika.


Jambo hili inawezekana liko hata katika taasisi nyingine lakini haimanishi tukae kimya.

Kama wahusika mpo humu,basi tupeni ufafanuzi wa hiyo logo na hiyo kauli mbiu(moto) labda tunaweza kuelewa.
Kwani shida nn apo uhuru ama nn
 
Hekima inasomewa darasani?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi unaelewa nini unapoambiwa tunatarajia wewe msomi uwe na busara na ustaarabu kuliko mtu mwenye elimu ndogo au ambae hajasoma?

Kwani inategemewa msomi afanye maamuzi kwa hekima kubwa kuliko mbumbumbu?

Endelea kusoma commet zangu zilizo fuata uone nilivyo fafanua zaidi tafsiri ya hekima(widom) na maarifa (knowledge) kwa kuangalia tafsiri ya hekima kama zilivyo elezewa na wana falsafa wakubwa.
 
Hekima haifundishwi popote! Kazi ya msingi ya chuo kikuu chochote ni kufundisha, tafiti, na ushauri. Nani duniani humu amewahi kufikia "Hekima ya Sulemani"? Alisomea chuo kikuu kipi kuipata hekima ile? UDSM ijikite kwenye majukumu yake ya msingi badala ya kuambatana na siasa uchwara!
Mafundisho unayopata chuo kikuu huleta au huongeza maarifa(knowledge), maarifa huongeza hekima.
Hekima inaenda sambamba na uhuru wa fikra.
 
Kweli wazungu walileta mfumo wa vyama vingi kutugawa hasa hiki kizazi cha sasa ambacho hakina misingi ni shida, alafu wamedakwa kule Ufipa ndiyo balaa kwenye GPA za 32.
Nembo hii inashida gani jamani maneno ya uhuru, mwenge wa uhuru, maji. Nakama tukiwasikiliza hawa wapumbafu walah tutakosa hata historia yetu hatutaijua.
Na ukishindwa kujiharalisha kisiasa utajiharalisha kwa nembo ya chuo, kweli kifo cha mende kimekaribia tutasikia mengi mara nembo ya taifa ina siasa na ukabila, kesho utasikia bendera ya taifa ina siasa za CCM rangi ya kijani ibadirishwe iwekwe ya nyekundu ya ufipa.
Ni upumbafu na ulofa katika ubora wake (Ben William Mkapa hakukosea)
Kwa muktadha wa maelezo yako unaonekana uliwahi kwenda shule, lakini haijakusaidia. Badala ya kuangalia hoja na hitaji la mtoa mada wewe unakimbilia kwenye mrengo wa siasa na kudhalilisha watu. Yeye alitoa dukuduku lake lililohitaji maelezo au majibu. Kama huna jibu ya nini kum-attack mtoa hoja? Una matatizo gani? Kama unafahamu hata mambo ya GPA unashindwaje kudhibiti mihemko yako? Nini tatizo lako? Wewe katika maisha sharti ujue kuna kutofautiana. Watu wotw hawawezi kuwa CCM wale CUF kwa wakati mmoja. Huoni wengine walikuwa Chadema na sasa ni CCM na kinyume chake? Unatakiwa ukue kiakili
 
Ama kweli Hekima ni Uhuru. Ukikosa hekima kama aliyeandika mada hii akili yako haiwezi kuwa huru.

Hekima ni byproduct ya knowledge. Ninamashaka na elimu uliyonayo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acheni hizo, mnataka tuweke alama ya msalaba na nyoka? Km ulaya? Wakati tuna waislamu?

Hayo ni yetu wao wazungu ndo watuige siyo sisi tuwaige tuuu!
Tatizo mnaongea sana kwanza tumejitahidi

Siasa ni kila kitu Duniani. Huwezi jitenga na siasa daima dumu.
 
Kwa maoni yangu mwenge hauna shida hapo.Mwenge ndio unaowakilisha dhana ya hekima maana unaangaza. Hapo hakuna kitu chochote kibaya.Mwenge hauna shida yoyote,kuweka alama ya kitabu haina maana yoyote endapo bado tutakuwa kwenye hali hii hii ya mfumo huu wa elimu.

Suala hapo ni kubadili sera na mifumo elimu ili iendane na wakati lakin mwenge hauna shida.Maneno hayo ni mazuri zaidi ya slogani zote unazozijua duniani hii chini ya mbingu.Kama hekima ingewekwa mbele kama wenzao walivyofanya awamu za nyuma mambo yangekuwa vizuri.Lakini awamu ya 5 wao kwao hekima ni upuuzi ndio maana kila siku wanaonekana kama midori wasio hata na haya wala soni.
Inasikitisha



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom