Zamani mimi nilikuwa najua neno tia linatumika bandarani tu(kutia nanga), baadaye nikaja kujua linatumika kama matusi pia, lakini kadri muda ulivyoenda nikaja kujua linatumika sana hasa na watu wa pwani katika mambo mengine mbambali mfano mapishi, "tia chumvi", "tia nazi", "tia mafuta" n.k
Siku za hivi karibuni nimeshangaa linatumika hadi na mashabiki kwenye mpira!, hivi majuzi nimesikia "toa Musonda, tia Pacome!"
Huu msamiati wa neno tia una maana gani hasa na unatakiwa utumike katika muktadha gani katika Kiswahili fasihi?