New administration under Samia Suluhu gives hope after 5 years of hopelessness

Tozo ilipaswa ijenge madarasa lakini inaliwa huo ndiyo ukweli wenyewe. Tulisema mfumo mzima wa muundo wa serikali ya mitaa ufumuliwe na kusukwa upya wahusika wamedinda.

Rais kuteua wakuu wa mikoa, wilaya na wakurugenzi wa halmashauri ndiyo chimbuko la wizi na ubadhirifu kwa sababu wateuliwa hawa hawawajibiki moja kwa moja kwa wananchi na hivyo kudhoofisha uwajibikaji.


Kulingana na rasimu ya marekebisho ya katiba ya Warioba wananchi walishauri mamlaka ya Rais yapunguzwe na kurudishiwa wananchi wenyewe lakini uroho wa madaraka na hulka ya kuwazawadia ajira makada wa CCM umesitisha mageuzi muhimu katika uendeshaji wa nchi. Wizi huu wa kutisha unafanywa na makada wa CCM waliopewa dhamana kwenye nyadhifa tajwa! Tungependa kukolezea kwa kutamka hadharani hakuna mteule hata mmoja wa Rais anachagulika na wapigakura kwenye eneo analolihudumia leo. Huu ni uwakilishi haramu. Pale penye uwakilishi haramu hakuna uwajibikaji na kujenga mazingira hatarishi ya watumishi kujichotea hela watakavyo!


Hata mkamue wananchi vipi kama ni Rais ataendelea kutubandikia maswahiba wake na jamaa zake wa karibu nyadhifa za wakuu wa mikoa, wilaya na DEDs basi hakutakuwa na maendeleo bali tutakuwa tunafukuzana na kashfa za wizi na ubadhirifu.


Tulisema Waziri Mkuu atimuliwe kwa kushindwa kuongoza mabadiliko ya muundo wa serikali za mitaa lakini hakuna mwenye masikio.

Hivi mna matatizo gani?


Hoja ya ukabila imesambaratishwa na ugatuzi Kenya.

Ukelele wa ugatuzi utaidhoofisha serikali kuu pia imegalagazwa na ugatuzi Kenya.

Tatizo la TZ ni kufanya kazi kwa mazoea. Mifumo ya uongozi aliyoiacha mkoloni miaka 60 iliyopita inakumbatiwa ili kulinda ajira za makada wa CCM ambao ndiyo viwavi jeshi.


Bila kuwawezesha wapigakura kuwaajiri wakuu wa mikoa, wilaya na madiwani kuwa waajiri wa watumishi wote kwenye halmashauri zao na kuendelea na huu mfumo wa Rais kuwateua watu ambao hata hawajui ila kwa kushauriwa na wasaidizi wenye masilahi yao tuendelee kutegemea uwajibikaji kwa wapigakura kukosekana na kuwa kichocheo cha wizi na ubadhirifu
Your browser is not able to display this video.
 
The word of the day




Sent from my SM-A715F using JamiiForums mobile app
 
Tunajiuliza tu kwanini kazi ya usambazaji wa gesi Kenya ifanywe na kampuni ya watu binafsi badala ya shirika la umma?

Na huko nako ni waislamu tu hakuna wamiliki wa kikristu wa hii kampuni ya Taifa Gas


Kama tumekosea tutafurahi kusahihishwa.


Umiliki wa hii kampeni binafsi ya Taifa gas tunamwona JK ndiye mwenye hisa kubwa kuliko hata kinara wa kampuni hiyo au tumechemsha?
 

American appetite for Russian products knows no bound. Despite sanctions, Russian raw materials are still vital to keep the American jobs alive.

Biden effort to tax those products will never hurt Russia, but American consumers who buy them after being processed.
 
Hoja siyo tukishindwa tuhalalishe ikiwa hivyo madawa ya kulevya tumeshindwa kwa hiyo tuhalalishe?

Hoja ya kuhalalisha hawana madhara kwenye jamii waruhusiwe na wajisajili walipell kodi.

Hata bangi turuhusu walipe kodi.


Pia, gongo tusilisahau halina tofauti na vikali vya wazungu
 
Mafanikio ya kibiashara ya Rostam Aziz na akina IPTL Harbinger Singh na James Rugemalira yalitokana na miaka 10 ya Urais wa JK.

Kama JK asingelikuwa Rais kwa hiyo miaka 10 watajwa hawa wasingekuwa wanatamba na biashara kubwa kubwa.

Na JK hatoi "free lunch" ni lazima naye ana hisa humo hata ukitafakari sana Rostam Aziz alipataje hisa za Vodacom bila mkono wa JK?

Halafu utuambie JK hakuwa na hisa katika hizo za Rostam Aziz kule Vodacom tukukubalie!

Rostam Aziz alipoziuza hisa zake Vodacom tuna kila sababu ya kuhisi JK alipata mgao wake kimya kimya.


Au tumeteleza?
 
Ukitafakari sana utaona Lowassa alibebeshwa zigo la JK la kashfa ya Richmond na baadaye Dowans.


Wahusika na hii michoro hawakuwa maswahiba wake bali wa JK.

Lowassa bunge limwombe msamaha ingawaje tunajua hawatafanya hivyo kwa kukhofia kupoteza ajira zao.


Hili tuna uhakika nalo [emoji817]
 
BARUA YA WAZI KWA EWURA: MNA SABABU GANI YA KUTONUNUA MAFUTA MOJA KWA MOJA KUTOKA URUSI HADI MPITIE KWA WACHUUZI WA INDIA?



Kwa nini hatununui mafuta ya urusi moja kwa moja tunapitia wachuuzi wa kihindi?

Jibu ni ufisadi wetu ndiyo unatutesa.


Bei ya mafuta ingelikuwa chini sana na kutoa ahueni kwa watu wote kama mafuta tungeliyanunua sokoni Urusi!


Uzuri wa Mrusi yeye ni mwongofu mno na ndiyo maana anauza mafuta bei ya kutupwa.

Kila pipa la mafuta ukilinunua moja kwa moja Urusi unapewa ruzuku ya $ 30 chini ya bei ya soko la dunia na hivyo kununua kiwese kwa bei poa kabisa!

Sisi EWURA hawataki tupate ahueni maana mkakati wao wa "bulky suppliers" wanaolangua bei ya mafuta huwakatia kidali chetu na hii inaelezea kwa nini hawako tayari kuwageuzia kibao wahindi.


Huko India hilo punguzo la $ 30 muhindi anaweka kibindoni khalafu anakugonga kama vile mafuta aliyachimba yeye!

Wahindi hawana hata tone la mafuta lakini ni wauzaji wakubwa wa mafuta ya warusi.


 
Tulichojifunza kwenye demokrasia ya vyama vingi ni kuwa ukubwa wa pua siyo wingi wa kamasi...


Huwezi kupima umaarufu wa chama cha siasa kwa mahudhurio kwenye mikutano yao ya kisiasa.

Sababu ya kadamnasi kuhudhuria mikutano husika ni.kujionea burudani ama vioja na wakati mwingine kuona kama kuna jipya

Sent from my SM-A715F using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…