New administration under Samia Suluhu gives hope after 5 years of hopelessness

New administration under Samia Suluhu gives hope after 5 years of hopelessness

Hoja ya kudai kifungu namba 13 kinamhitaji Mwekezaji aendeleze ujuzi wa wafanyakazi halina namna likapimika



Ana waendeleza ili iwe nini?


Kwani yeye mkataba unamtaka awaandae TPA ili waje kuendesha hilo kampuni au kapewa fursa ya kuwadhoofisha hadi wafe?

Haya malengo ya kuwaimarisha TPA yana mgongano na mkataba mzima ulivyo.
 
Msiseme ukanda bali mseme ni masilahi binafsi yamewaunganisha
PSX_20230610_194526.jpg
 
Ikija kutangaza matokeo ya chaguzi huchukua wiki mbili ukiuliza wanasema nchi ni kubwa ikija bunge kukusanya maoni ya wananchi wachangie juu ya mkataba feki muda ni siku moja


Hakuna anayekumbuka nchi ni kubwa na haiwezekani watu watoke mikoani hadi wafike Dodoma na kuweza kufikisha michango yao.


Hapa ndipo tulipofikia
 
Na Deodatus Balile, Dubai

Wiki iliyopita nimepata fursa ya kusafiri kwenda Dubai. Nimetembelea maeneo kadhaa, ila moja ya maeneo hayo ni Bandari tatu zinazoendeshwa na Kampuni ya DP World.

Kampuni hii inamilikiwa na Familia ya Mfalme anayetawala Dubai. Kwa Dubai, kampuni hii inaendesha Bandari tatu ambazo ni Jebel Ali, Mina Rashid na Al Hamriyah.

Bandari hizi ziko kati ya umbali wa kilomita nane (8) na 46 kutoka Bandari moja hadi nyingine.

Takwimu nilizozipata, Bandari hizi zinasafirisha kontena milioni 22 kwa mwaka hapa Dubai. Kampuni hii inafanya kazi katika nchi zaidi ya 40 duniani na inaendesha magati 82 sehemu mbalimbali duniani kwa mwaka, ambayo hupokea na kusafirisha makontena milioni 70 yanayosafirishwa na meli 70,000 duniani kote.

Sitanii, ni vigumu mtu kueleza akaeleweka anamaanisha nini. Ukifika katika Bandari ya Jebel Ali, ndipo unaona kuwa kuna binadamu wanaofikiri.

Hoja si tu, makontena wanayosafirisha, bali pia mipango ya sasa na baadaye.

Katika Bandari hizo tatu, kuna mitambo mikubwa ya kushusha na kupakia hizo kontena milioni 22, lakini hawaridhiki.

Ndugu zetu wa hapa Dubai, kupitia DP World kwa sasa wanaendelea na mradi wanaotaraji kuukamilisha mwakani, ambao Bandari itaendeshwa kwa kutumia akili tarakirishi (artificial intelligence).

Kwamba mteja akiwa na kontena lake, hatalazimika kusubiri ‘winch’ ipangue makontena matano kufikia kontena lake la chini.

Kontena zitakuwa zinapangwa kwenye chanja (shelves) ambazo ukibonyeza kifungo (button) na kuweka namba ya kontena husika, hata kama litakuwa katikati ya kontena 30,000 litajichomoa na kutoka nje.

Hii si ya kufikirika au kusadikika, bali wameanza kujenga mitambo husika.

Sitanii, hawa DP World, wapo katika nchi kadhaa za Afrika. Wapo Senegal, waliyofanya Mungu anajua.

Wapo Somalia, nchi ambayo ipo vitani miaka yote tangu kifo cha Rais wao Mohamed Farrah Aidid Agosti 1, 1996, lakini kwa msaada wa DP World kuna habari sizizofurahisha katika masikio ya Wantanzania.

Kwamba kwa macho yangu nimeshuhudia kondoo, matikiti maji, vitunguu, nyanya, mchicha, viazi na kila chakula unachokiwaza kikiuzwa Dubai kutokea Somalia, ilihali sisi huu ni msamiati.

Nimeuliza inakuwaje sisi hatuwezi hili, nikapewa jibu la aina yake. “Shida si Watanzania, bali mifumo iliyowekwa na viongozi wenu. Kinachotakiwa ni kuwawezesha Watanzania. Kuwajengea maghala ya kuhifadhia bidhaa za kilimo karibu na Bandari, kuwaeleza viwango na mbinu bora za kilimo.

"Wananchi wakifahamu mahala penye fedha, masharti watayafuata na kutengeneza fedha. Watanzania wanaweza haya,” ameniambia Afisa mmoja niliyezungumza naye kwenye Bandari ya Jebel Ali.

Sikukomea hapo, nimeuliza imekuwaje Bandari tatu ziko pamoja zinasafirisha kontena 22,000 kwa mwaka hapa Dubai, ilihali sisi hapo Tanzania tumezungukwa na nchi nane, lakini tunasafirisha kontena 700,000 tu kwa mwaka.

Jibu nililopewa ni lile lile ujenzi wa mifumo. Tena, hawa DP World wakasema wanatafuta fursa ya kuja Tanzania kushirikiana na Tanzania, lakini miaka yote wamekwama.

Katika kukwama, wakaamua kwenda nchi jirani ya Rwanda. Wamejenga Bandari Kavu Rwanda.

Makontena ya nchi nyingine sasa yanapitia Bandari ya Dar es Salaam yanakwenda Rwanda, nchi hizo zinachukua makontena pale.

Kampuni ya vyakula ya KFC imefungua ofisi zake Rwanda kutokana na mifumo bora ya Bandari Kavu.

Ndugu zangu Watanzania. Nimesisimuka mwili. Manyoya yamesimama. Sikuamini nilichokiona katika wasilisho.

Rwanda imewapa DP World ardhi yenye mita za mraba 20,000 kuweka Bandari Kavu. Hizi mita za mraba zimekuwa ufuguo wa Rwanda kuingia katika biashara ya Bandari.

Hivi sisi tuna kilomita ngapi za mraba katika Bahari ya Hindi na nchi kavu, hadi leo tuzidiwe na Rwanda inayoanza kuwa nyota inanayong’ara ndani na nje ya Bara la Afrika?

Kwa masikitiko, hapa nchini kwetu tumeambiwa eti Bandari mpya ya Bagomoyo ikijengwa, itaimeza Bandari ya Dar es Salaam. Wajinga ndiyo waliwao.

Bandari zinapokuwa nyingi, ndivyo ushindani unavyoongezeka. Ndivyo mapato yanavyoongezeka. Bandari mbili hapa Dubai zinatenganishwa na kilomita nane (8), ila bado zinatengeneza fedha ndefu.

Sisi hapo kwetu TICTS imekaa hapo miaka 22, bado tunahudumia makontena 700,000 tu kwa mwaka wenzetu wanahudumia milioni 22.

Hapana. Tutafute wenye uwezo wa kutuvusha. Bila kuuma maneno, DP World wanayo nafasi ya kuivusha Tanzania.

Sitanii, nimelazimika kumkumbuka Mwenyekiti wa Chama cha Economic Freedom Fighters (EFF), Julius Malema wa Afrika Kusini.

Binafsi naamini wazee wetu wamepambana kupata uhuru wa nchi yetu, ila sisi hakuna tulichopambania.

Naamini wakati wetu sasa umefika tupambane kupata Uhuru wa Kiuchumi. Hapo kwetu chanzo muhimu cha uchumi ni Bandari.

Kwa miaka 22 tumekuwa na kampuni ya Tanzania International Container Terminal Services (TICTS).

Nasikia wiki hii mkataba wao umekwisha hapo nchini.

Tuwashukuru kwa kazi waliyoifanya kwa miaka 22, ila sina uhakika kama wameifikisha nchi yetu katika malengo tarajiwa.

Kwa mfano, Kampuni ya DP World inazalisha asilimia 33 ya uchumi wa Dubai.

Hii maana yake ni nini? Nchi yetu kama ikiitumia vyema Bandari ya Dar es Salaam, ina uwezekano wa kuzalisha si chini ya asilimia 45 hadi 50 ya bajeti ya taifa letu.

Tanzama imezungukwa na nchi za Uganda, Rwanda, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, Zambia, Zimbabwe na Malawi, ambazo zina uwezekano mkubwa wa kutumia bandari yetu.

Si hizo tu, hata sehemu ya Kenya na Msubiji, baadhi ya mikoa yao ni rahisi kutumia Bandari zetu.

Sitanii, mpendwa msomaji. Wiki hii niruhusu niishie hapa. Wiki ijayo nitaandika kwa kina wapi tumeteleza wapi na tunaweza kusahihisha nini.

Watanzania hatukuzaliwa kula shida. Nafahamu wapo watu wachache wenye vita yao mkononi wakitaka wapewe Bandari waendelee kuvuna.

Msitari huu tuuvuke. Tujenge nchi. Tanzania kwanza, masilahi ya mtu mmoja mmoja baadaye. Mungu ibariki Tanzania.


Tatizo kubwa la haya mawazo mgando ni kuweka mbele ufanisi bila kutafakari thamani endelevu ya uhuru wa kujitawala.

Inatosha kukumbushana jukumu kuu la serikali ni kutoa huduma na siyo kufanya biashara. Serikali yoyote ile ambayo inakasimu jukumu lake la usalama wa taifa halina uhalali wa kuendelea kutawala.

Tz hatujawekeza bandarini kama walivyowekeza Dubai. Kweli kuikana katiba yetu kwa uwekezaji wa $600 Mill ambazo ni kiduchu inathibitisha uwezo wa kufikiri wa mtanzania ulipogota. We name it as poverty mentality.

Sisi siyo Rwanda au nchi nyingine zinazowapa mataifa mengine ardhi wawafanyie wao kazi. Kazi tutafanya wenyewe siyo askari wa mamluki

Nchi zote zenye maendeleo zimeamini watu wao na kuwawezesha wakati sisi tunafungua fursa kwa mamluki.

Uzuri migogoro inakuja. Baada ya 2030 Rais atakayekuja atatengua huu mkataba. Na utashangaa wabunge hawahawa watalipitisha hilo azimio
 
Bunge la JMT limekiri limeshindwa kutunga sheria pale lilipoamua uuzwaji wa bandari zetu zote usisimamiwe na sheria zetu bali usimamiwe na sheria za mkoloni wa kiingereza.


Kutokana na huu ukweli, wazo na mikakati ya kuliuza bunge kwa waingereza ili warudi upya na kutunga sheria lina mashiko maana TPA imeporwa mamlaka ya kisheria kwa sababu za utendaji mbovu na sababu hizi hizi pia bunge linahusika.
 
Serikali hii yote iliapa kulinda na kutetea katiba yetu kwa kukubali kwao uuzwaji wa bandari zetu kwa waarabu na sheria za uingereza zitumike ni kuisigina katiba yetu kwa hiyo kwa umoja wao wameviasi viapo vyao na hivyo kupoteza uhalali wa kutawala na wawe waungwana wajiuzulu.


Tufike mahali tufute viapo maana watu wanaapa bora liende lakini hawana hata nia ndani ya mioyo yao kutii hivyo viapo.

Na ndiyo maana Maandiko yanatuagiza tusiape kwa sababu hatutavitii hivyo viapo na hivyo kuongeza uadui tu na Mwenyezi Mungu.
 
Wale mnaomsifia Mwendazake (JPM) mkumbuke sababu kuu hii serikali imetuingiza mkenge ni kwa sababu ya mazingira aliyoyajenga mwenyewe ya kuiba kura chaguzi za 2020 na hivyo tukawa na uwakilishi haramu ambao hauwajibiki kwa wapigakura bali unawajibika kwa CCM ambao ndiyo waliwachagua.

Uwakilishi haramu ndiyo unazaa hulka ya kuupinga utawala wa sheria maana hauwajibiki kwa wananchi na hapa ndipo tumegota.
 
Nina uhakika bila shaka, NGOs nyingi wako kwenye mikakati ya kuwaburuza hawa wakora mahakamani.

Okoeni muda na vijisenti vyenu msiende huko maana mahakama zetu teuzi zake zina macho na wengi wa hao waheshimiwa ni makada wa CCM.

Wamebebwa ili kulinda dhuluma na mkienda huko watanukuu hukumu ya kifisadi ya Mtikila dhidi ya Mwanasheria Mkuu inayosema kama Bunge lina koramu mahakama haiwezi kutengua maamuzi yao.

Kwa lugha nyingine, kama Bunge lina koramu likaamua majaji wote wachinjwe itabidi tu wachinjwe na hata kama kesi itakuja mbele ya hawa waheshimiwa watakuwa hawana jinsi bali kuamua hawana mamlaka ya kutengua maamuzi ya Bunge kwa hiyo wachinjwe tu teh teh teh.

Tunajua watatengua fasta kwa mwendokasi ambao hata nuru hautashindana nao. [emoji2] [emoji3] [emoji1] [emoji16] [emoji1787] [emoji23] [emoji2] [emoji3] [emoji1] [emoji16]

Hebu fikiria, wastaafu walipodai sheria ya mafao iliyowapora hata wale waliohitimu miaka 50 malipo yao yakasitishwa na bunge Mahakama ya Rufani ilipotengua uamuzi wa mahakama kuu wa kurejesha haki za wastaafu walisema pensheni siyo ujira hivyo hailindwi na katiba wakati mkataba wa ajira ni uleule!!!!!!!!!!!!!

Kwenye marejeo, mahakama ya rufani ikasema sheria hii mpya pamoja imekuwa mshindo nyuma (retrospectivity) haikiuki katiba wakati inakiuka.

Uamuzi huu ulilenga kuwanyima malipo ya pensheni wastaafu walio na miaka 50-55.

Pia uamuzi huu ni pigo kwa sheria ya jinai kwani sasa bunge linaweza kutunga sheria zenye adhabu kubwa kuliko za awali na kuamuru waadhibiwe hata wale ambao walitenda makosa hayo kabla ya sheria hizo mpya kutungwa na hivyo kukiuka katiba yenye makatazo ya sheria za mshindo nyuma (retrospectivity).

Tunajua sheria ya pensheni itaendelea kubadilishwa kwa kupaaishwa umri wa kustaafu kwa kuwa mifuko hii inaliwa na inatafunwa kwa sababu wafanyakazi siyo wasimamizi wa hiyo mifuko.

Wanasiasa waandamizi wa CCM ambao siyo wachangiaji wa hiyo mifuko ndiyo wanayoisimamia na hawana uchungu nayo na hivyo huifuja sasa kufidia wizi na ubadhirifu unaoendelea kwenye hiyo mifuko ni kuzuia kwa kutumia sheria wastaafu kulipwa chochote na hata kuwaombea wafe mapema ili wasije kuikausha hii mifuko.


Sasa, tulitegemea mahakama ya rufaa itende haki kwa kusema kwa vile malipo ya kustaafu ni sehemu ya mkataba wa ajira basi chochote mfanyakazi anacholipwa kinatokana na mkataba ni ujira wa mfanyakazi na unalindwa na katiba. Lakini hawa nguli wa sheria wakaona hapana malipo ya uzeeni pamoja yanatokana na mkataba wa ajira siyo mshahara maana mfanyakazi hayuko kazini.

Mbavu zangu hoi, hivi mfanyakazi anapolipwa mshahara akiwa likizo na hafanyi kazi huo siyo ujira? Kama ni ujira kwanini malipo baada ya kustaafu yasiwe ni sehemu ya ujira kama siyo dhuluma dhidi ya wastaafu wanyonge.

Mbali ya teuzi za majaji kuwa zinalenga kulinda uozo serikalini lakini pia mafao ya kustaafu ya hawa waheshimiwa yana sheria tofauti na hizi za wafanyakazi wengine na ndiyo maana hawaguswi na maamuzi yao yaliyokithiri dhuluma.

Kwa hiyo, enyi wenye NGOs mtafakari hizi hoja labda kama mna wafadhili nje ya nchi basi mna ubavu wa kufika hadi Mahakama ya Haki za Binadamu ya Afrika maana kwenye mahakama zetu andikeni maumivu kwa haya masuala ya wazi ya kukiuka katiba ya nchi.

Vinginevyo, msijitese bure wenzenu tayari wamejipanga.
 
Tulichojifunza kwa wamarekani vuguvugu la kisiasa tu ndilo litatengua maazimio ya kibunge na mikataba feki.

Hakuna cha mikataba ya milele mbele ya nguvu ya umma.

Tutaendelea kuelimishana ili Rais ajaye wa 2030 afute huu upuuzi kama wataamua kwenda kwa msuluhishi waache waende lakini bandari zetu zitasimamiwa na makampuni ya umma ya watanzania na hakuna cha ubia bali kuongeza uwezekaji tu zaidi hata ya ATC ambako hakuna la maana linaloendelea huko.
 
Tulichojifunza kwa wamarekani vuguvugu la kisiasa tu ndilo litatengua maazimio ya kibunge na mikataba feki.

Hakuna cha mikataba ya milele mbele ya nguvu ya umma.

Tutaendelea kuelimishana ili Rais ajaye wa 2030 afute huu upuuzi kama wataamua kwenda kwa msuluhishi waache waende lakini bandari zetu zitasimamiwa na makampuni ya umma ya watanzania na hakuna cha ubia bali kuongeza uwezekaji tu zaidi hata ya ATC ambako hakuna la maana linaloendelea huko.
Free mason is real na hao ndio wanaongoza Nchi na wanapanga mipango ya Nchi nani awe raisi nani auwawe.
 
Here are benefits from TZ-UAE agreement.

Daily NewsJun 11, 2023 6:17 AM



THE government has highlighted a number of benefits to be obtained after the Parliament endorsed the Inter-Governmental Agreement (IGA) between Tanzania and the United Arab Emirates (UAE), focusing on social-economic partnership for developing and improving performance of ports in the country.

Minister for Works and Transport, Professor Makame Mbarawa, on Saturday outlined 14 expected benefits of the agreement, including application of modern technology and system that will make ports operations fast and effective, thus increasing revenue.

Prof Mbarawa also pointed out that the implementation of the document will assure ports workers of their employment security, because the agreement has set measures to increase employment opportunities from 28,990 in 2021/22 to 71,907 come 2032/33.

He told the Parliament that the increase in employment opportunities is set at 148 per cent.



The minister said average number of days for a vessel to stay at the port will be reduced to 24 hours from the current five days, thus increasing efficiency.

Furthermore, it will increase the number of ships docking at the Dar es Salaam Port from 1,569 in 2021/22 to 2,950 vessels by 2032/33.

Prof Mbarawa went on to argue that if implemented, the agreement will enable the port use only two days to offload containers from the ship, unlike present when the port spends up to four days.

On the part of bulk cargo, the port will have capacity of offloading within one hour while currently it spends 12 hours



“This is a result of improvement of the Information and Communication Technology (ICT) infrastructures,” the minister informed MPs.

For customers using the Dar es Salaam Port to ship containerised cargo destined for Malawi, Democratic Republic of Congo (DRC) and Zambia, the transport cost per container will be cut down by half from 12,000 US dollars to between 6,000 and 7,000 US dollars.

The number of customers using the ports are expected to double as well as increase in cargo volume from 18.41 million tonnes in 2021/22 to 47.57 million tonnes by 2032/33, an increase that is almost 158 per cent.

The cargo volume increase will see a rise in revenue and tax collection from 7.76tri/- in 2021/22 financial year to 26.7tri/- in 2032/33, equivalent to 244 per cent increase.

Moreover, the government will benefit from upgrading of the storage facilities to handle all types of cargoes.


Never forget Makinikia extrapolation, which nobody in the CCM wants to hear, let alone regurgitate.
 
Back
Top Bottom