New administration under Samia Suluhu gives hope after 5 years of hopelessness

New administration under Samia Suluhu gives hope after 5 years of hopelessness

Kifupi na inatosha kusema hatuwezi kumilikisha wageni utajiri wa nchi hii ambao tumepewa na Mwenyezi Mungu kwa ajili ya vizazi vijavyo
 
Kama Nyerere angelikuwa mlafi kama hawa watawala wa sasa wangelikuta kuna cha kujimilikisha wao na watoto wao kwa mgongo wa uwekezaji?
 
Tuendelee kujipigapiga vifua TUNAWEZA

Mzee Jomo Kenyatta alikuwa na tabia ya kusema tutembee kifua mbele na matako nyuma.

Wakati umefika wa kujivunia kuwa watanzania wenye uwezo wa kujitawala wao wenyewe
 
Ikifika mahali tukaona hatuwezi turudi UN na tukiri hatuko tayari kujitawala tukabidhiwe tuwe koloni la nchi yoyote ile UN itaona inafaa
 
Wizi na ubadhirifu siyo miliki ya mashirika ya umma tu bali ni saratani ya utumishi wote wa umma
 
Acheni kunyoshea vidole wenzenu wakati usafi wenu hatuoni.

Kumbukeni kama mmesahau samaki mmoja akioza wote wameoza
 

View: https://youtu.be/WIO8uBaEibc

Kubadilisha sheria ili kumnufaisha mwekezaji mmoja tu ni kumpendelea na kwa kufanya hivyo ni kukiuka katiba kwa kuondoa usawa kwa wote


Si bunge au mahakama inaheshimu ukatiba kwenye hili sakata kwa kuwa huu sasa ni mlo wa wanasiasa wa kitaifa.

Hata ukiwapa maoni yako bunge watayatupilia mbali maana hawako kukutumikia wewe bali kuyatumikia matumbo yao.

Na kukaribisha maoni ya wananchi wakati tayari wana azimio lao la kibunge kiganjani ni uthibitisho wa uwazi wa unafiki wao.

Hata ukienda mahakamani wataikana katiba ili mradi wezi wa mali ya umma waendelee kula.

Hii ndiyo Tanzania ambayo tunajaribu kuijenga ambayo viongozi wa kitaifa wapo madarakani siyo kwa masilahi ya wengi bali ya kwao na wawapendao.

Sisi wengine ni kulishwa maneno matamu matamu tu ya kutupa matumaini hewa.

Lakini hii sasa ni laana yao ya ulafi. Watakula na kuvimbiwa lakini hawatashiba. Kila mlo watateswa na uroho wao. Watalala vitandani lakini hawatapata usingizi kwa sababu watateswa na ulafi wao.


Watalindwa na askari lakini mioyoni mwao watakosa amani na maisha yao yote watagubikwa na khofu ya ghadhabu ya Mwenyezi Mungu.

Uzao wao utabughia madawa ya kulevya na watazama kwenye ngono hadi magonjwa yasiyosikia tiba kuwatoa uhai wao.

Mafisadi watakesha misibani na mahospitalini wakishindiliwa madawa na hata kwenye sherehe watajisikia wana majonzi na wanaumwa kwa sababu wamemkana Mwenyezi Mungu ambaye angeliwafariji kama wangeliikana hii dunia na mambo yake yote.

Watajiita ni matajiri kumbe ni masikini wa kutupwa na wapweke.
 
SERIKALI IJIANDAE KUWATETEA DP WORLD PALE MAPATO NA AJIRA ZA BANDARI ZITAKAPOSHUKA!

Hawa siyo wawekezaji bali ni mchwa. Pigo la kwanza mapato yatashuka kinyume na matarajio yao.

Pigo la pili baada ya TPA kuporwa ugali itabidi wapunguze ajira kutoka wafanyakazi 600 hadi 100. Serikali iliahidi ajira kutoathirika lakini ukweli zitapungua mno.

Pigo la tatu, mizigo haitaongezeka bali itapungua. Wao wanadai ufanisi utaongeza tashwishwi ya kutumia bandari ya Dar lakini uhalisia sababu kuu ya kupanda matumizi ya bandari ni kasi ya kukua GDP. Na kila kipimo kinaonyesha mapato ndani ya SADCC yatashuka.

Wajiandae kumtetea mwekezaji kwa kushindwa kuongeza mapato na kukaza buti kutukamua kwa kodi kufidia pengo la mwekezaji hewa.

Sisi wengine ni mbavu zetu tu zitakazo kuwa hoi pale matutusa watakapobainika.

Mfupa ulilolishinda jimbo la Delaware Marekani sisi ndiyo kabisa tusubirie chali tu yaani hakuna jinsi.
 
SERIKALI IJIANDAE KUWATETEA DP WORLD KWA SABABU AJIRA NA MAPATO YA BANDARI YATAKASHUKA MNO!

Hawa DP WORLD siyo wawekezaji bali ni mchwa. Tuna mapigo matatu yanahusiana na huu uwekezaji wa kifisadi yanakuja bila kuchelea.

Pigo la kwanza mapato yatashuka kinyume na matarajio yao. Mapato ya wateja wa bandari ya Dar-es-Salaam yatashuka kutokana na kudorora kwa uchumi wa dunia na hawatasafirisha mizigo mingi.

Pigo la pili baada ya TPA kuporwa ugali itabidi wapunguze ajira kutoka wafanyakazi 3, 450 hadi 600 tu. Serikali iliahidi ajira kutoathirika lakini ukweli zitapungua mno.

Pigo la tatu, mizigo haitaongezeka bali itapungua. Wao wanadai ufanisi utaongeza tashwishwi ya kutumia bandari ya Dar lakini uhalisia sababu kuu ya kupanda matumizi ya bandari ni kasi ya kukua GDP. Na kila kipimo kinaonyesha mapato ndani ya SADCC yatashuka.

Wajiandae kumtetea mwekezaji kwa kushindwa kuongeza mapato na kukaza buti kutukamua kwa kodi kufidia pengo la mwekezaji hewa.

Sisi wengine ni mbavu zetu tu zitakazo kuwa hoi pale matutusa watakapobainika walidhani wanajua kumbe hawajui kitu.

Mfupa ulioishinda bandari ya Wilmington ya jimbo la Delaware Marekani sisi ndiyo kabisa tusubirie porojo za kwanini mapato na ajira zimetoweka.

Jimbo la Delaware lina mkataba bora kuliko huu wetu wa kitumwa lakini hadi sasa miaka 6 imepita hawajalipwa hata senti moja na DubaiTainer pamoja na mizigo yao kuwa karibu mara tatu ya bandari ya Dar-es-Salaam. Mara wamesingizia kovid na sasa wanajitetea uchumi wa dunia umeyumbishwa na vita vya Ukraine, vikwazo vya uchumi dhidi ya Urusi na Uchina n.k
 
KUKEMEA DHULUMA SIYO KUCHANGANYA DINI NA SIASA.

Sina uhakika kukemea dhuluma na maovu ni kujiingiza kwenye siasa. Kama ingekuwa ni hivyo Yohana Mbatizaji asingemkemea Herode kwa kumuoa mke wa kaka yake hadi akauawa kwa kukatwa kichwa. Inamaana kukemea maovu Yohana Mbatizaji alikosea? Yohana Mbatizaji aliitwa na Yesu Kristu ni Nabii Mkubwa kuliko wote waliozaliwa na wanawake
 

Attachments

  • IMG-20230820-WA0013.jpg
    IMG-20230820-WA0013.jpg
    205 KB · Views: 1
  • IMG-20230820-WA0012.jpg
    IMG-20230820-WA0012.jpg
    235.9 KB · Views: 2
Spika wa bunge alipokea kwa mikono miwili tamko la kiroho la baraza la maaskofu wa kikatoliki.

Tunasubiria mrejesho kama atalitii au la
 

Attachments

  • IMG-20230820-WA0011.jpg
    IMG-20230820-WA0011.jpg
    88.3 KB · Views: 4
Asante Makamu wa Rais kwa kupendezwa na Tamko letu la kiroho siyo kama Tulia kanuna huku akilipokewa kwa mikono miwili
 

Attachments

  • IMG-20230820-WA0032.jpg
    IMG-20230820-WA0032.jpg
    28.7 KB · Views: 3
  • IMG-20230820-WA0031.jpg
    IMG-20230820-WA0031.jpg
    38.2 KB · Views: 3
Pray for Nape Nnauye cause he is heading to a dark alley so to speak to a cul del sac
 
Back
Top Bottom