New administration under Samia Suluhu gives hope after 5 years of hopelessness

New administration under Samia Suluhu gives hope after 5 years of hopelessness

Walisema watoto wetu ni wezi, wabadhirifu, hawana ujuzi wa ngazi za juu na kati.

Sasa huku tumefikaje?

Mlisema hatuendi mbali hizi tuzo tumekwapua?

Mnyonge msimnyonge haki yake mpeni.

Utendaji wa mamlaka ya bandari ni wa KUTUKUKA. Mengine ni ufisadi wao tu ndiyo unawatesa
 

Attachments

  • PSX_20230820_234603.jpg
    PSX_20230820_234603.jpg
    126 KB · Views: 3
Kama wanasiasa hawajui namna ya kumwezesha mzawa akaendesha bandari zetu kisayansi kama hamjui basi imekula kwenu mtupishe.

Sisi tupo tumejaa tele
 
Matoto yetu ni mijizi, haina ujuzi na mzigo kwenye bandari zetu.

Sasa huku tumepata tuzo ya kimataifa mnaonaje mkituomba msamaha kwa kutukosea adabu?
 

Attachments

  • IMG-20230821-WA0014.jpg
    IMG-20230821-WA0014.jpg
    77.6 KB · Views: 2
Ukiona bendera yako inapeperushwa na Dubai ujue wanakutafuna. Hawepepereshi bendera yako bureee
 

Attachments

  • PSX_20230821_180409.jpg
    PSX_20230821_180409.jpg
    134.2 KB · Views: 3
Mnaona bandari za wenzenu ni kubwa mno lakini hakuna cha kumwamini wakuja awatatulie matatizo yao.

Wanagangamala tu mpaka KIELEWEKE.
 

Attachments

  • PSX_20230821_184948.jpg
    PSX_20230821_184948.jpg
    203.7 KB · Views: 3
Huyu kesha umizwa na masahibu ya bandari
 

Attachments

  • PSX_20230821_202432.jpg
    PSX_20230821_202432.jpg
    125.4 KB · Views: 3
Waghana hawataki watoto wao waende vitani Niger.

Hawataki kuwaona watoto wao aidha wanawauwa au kuuawa na Waafrika wenzao wa Niger kwa masilahi ya mabeberu

Kama viongozi wao bado wanataka majeshi yao kujiunga na ECOWAS basi wawapeleke watoto wao.
 

Attachments

  • 1692656328473.mp4
    591.9 KB
Tatizo la Mkapa hakuwa mkweli. Alijua hatutapata kitu ila kwa vile yeye alihongwa aliona inatosha.

Kwenye kampeni za urais wa JPM 2015 hakuwa madarakani na alitutusi tuliokuwa tunampinga akatuita wapumbavu. Na you tube hii video ipo.

Viongozi wetu ni walafi wanajidanganya wataishi kwa mkate tu wakati hauwapeleki popote.

Hata huyu mama akistaafu atajitetea kama Mkapa.

Bila watanzania kujisimamia mambo yetu wenyewe hakuna maendeleo ila migogoro itazuka na hawa wawekezaji feki tutaishia kuwafidia mabilioni
 

Attachments

  • IMG-20230822-WA0005.jpg
    IMG-20230822-WA0005.jpg
    57.8 KB · Views: 3
Busara za Nyerere zilipuuzwa na sasa vijana hawana ajira na wanao wapora ajira hawaachi kuwasisitizia wajiajiri huku wakijua hawawezi kujiajiri kwani ajira zao wamewatunuku wakuja kwa ujira si haba
 

Attachments

  • 1692687215807_1692687215807.mp4
    4.6 MB
“TANESCO yatumia Sh75 bilioni kukodi software kwa miezi 30”


Ndg January Makamba umetumia (Sh75 bilioni) kukodi ERP software, wakati kuna vitongoji 37,610 kati ya 64,760 havijapata umeme? Nchi isiyo na umeme wa kutosha tunazo 1,605MW tu unatumia US$30M kukodi Enterprise Resources Planning (ERP) software kwa Tech Mahindra? eGA kazi yake? Matusi!

Lengo la TANESCO kusaini mkataba huo wa Sh75 bilioni (US$30 million) na kampuni kutoka India, Tech Mahindra wametueleza kwamba ni kusaidia kuboresha utoaji huduma kwa mtandao. Wakati huo serikali ina huduma yake inaitwa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA).

Enterprise Resources Planning (ERP) ni mfumo wa mipango wa rasilimali za biashara kazi yake ni kutambua kwa haraka masuala yanayowaathiri wateja na wafanyakazi na kuyatatua kwa haraka. Kazi ambayo inafanywa na Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA).

Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) tayari walishatengeneza mfumo kama huo na unatumiwa na Taasisi mbali mbali za Serikali, unaitwa Enterprise Resources Management Suite (ERMS). Huu mfumo mwingine wa January Makamba na wahindi wa Tech Mahindra una kipi cha ziada?

Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) ambao ndiyo wenye jukumu la kusimamia pia Enterprise Resources Management Suite (ERMS) ipo chini ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Rais analifahamu jambo hili, na kama hafahamu wanamficha.

Wahindi hawa wenyewe wanaiita Corporate Management System (CMS). Software ya aina hii inaunganisha vitengo vyote vya taasisi katika software moja kwa ajili ya urahisi wa kuendesha taasisi. Kwa kuwa TANESCO wamekodi, waendeshaji ni wahindi.

Kumbuka, hizi Sh75 bilioni ni fedha ambazo zimetumika kukodi Enterprise Resources Planning (ERP) software kutoka Tech Mahindra kwa miezi 30 tu. Kwamba wahindi wamekodisha (siyo kuuza) mifumo kwa miezi 30 kwa faida ya Sh75 bilioni.

Ukiingia katika tovuti za selecthub na betterbuys, wamekupa gharama (cost) ya ERP and budget guide. Bei ya juu ya kununua Enterprise Resources Planning (ERP) software ni US$10 million (Sh25 bilioni). Kununua siyo kukodi. TANESCO wamekodi kwa US$30 million (Sh75 bilioni)

Zabuni hii ilitangazwa nyakati za mwisho za utawala wa Jakaya Kikwete, haikufanikiwa. Alipoingia Rais John Magufuli akasitisha mpango huo. Alipoingia Rais Samia Suluhu Hassan na kumteua January Makamba kuwa waziri wa Nishati, mpango umefufuliwa na nchi imekodi software.

Kama Enterprise Resources Management Suite (ERMS) ya Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) haijaunganishwa (integratable) na mifumo mingine ya taasisi za serikali hadi tutumie Sh75 bilioni kukodi software kwa miezi 30 ni wazi nchi yetu hatuna programmers. Nchi mfu.

Lakini, ukisoma specifications za Enterprise Resources Management Suite (ERMS) ya Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) inaeleza wazi kuwa ni shirikishi (interoperable) na mifumo mingine ya taasisi za serikali. Ghafla tu tuelezwe mifumo haisomani tena? Hapana.

Hatuwezi kuendesha kila kitu wenyewe, tunakodi wataalam kuendesha hadi mifumo ya shirika la umeme? Wakati fulani TANESCO ilibinafsishwa kwa makaburu wa Afrika Kusini kwa hoja kwamba shirika limeshindwa kujiendesha hivyo wapewe wageni, nchi ikaingia gizani ikazaliwa RICHMOND na IPTL.

PS; Software kama hizi kwanini serikali isiwezeshe wataalam wa ndani kupitia Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) kutengeneza, kama vile mfumo wa malipo serikalini (GePG) ulivyotengenezwa na wataalam wetu wa ndani kwa kuwezeshwa na serikali.

University of Dar es Salaam - College of Engineering and Technology (CoET) wanafundishwa nini kama Shirika la umeme (TANESCO) linaweza kwenda kutumia Sh75 bilioni kwa miezi 30 tu kukodi Enterprise Resources Planning (ERP) software kwa Tech Mahindra?

Ushauri; Kukodi ni mbinu mpya ya software developers ili uwe mteja wao wa milele. Kuna software nyingi unanunua mara 1 na unapata free lifetime upgrades and updates. Ukikodi, mfumo ukisumbua kidogo wataalaam wanakuja unawalipia kila kitu ikiwepo perdiem kwa rate za dollars. Akili.

MMM, Martin Maranja Masese, Mtikila
 
Haya ni maagizo ya Mwenyezi Mungu atakayekiuka ni adui wake na HATAFANIKIWA.
SASA MSIJE KUJITETEA HAMKUJUA KAMA MKAPA ALIVYOJARIBU KUJINASUA HAKUFANIKIWA
 
Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe; Bali achukiaye zawadi ataishi.
Mithali 15:27 SRUVDC
 

Attachments

  • 1692706529003.mp4
    2.5 MB
Wakati India wamewasili Mwezini kwa kutumia rasimali wao wenyewe sisi watawala wetu uchwara badala ya kuandaa vijana wasimamie angalau kwa kuanzia uchumi wao sisi tunakaza buti kuwazuia hata kuendesha bandari zao wenyewe ila watawala wanaona hayo ndiyo mafanikio miaka 61 tangu tupate uhuru
 

Attachments

  • PSX_20230823_161034.jpg
    PSX_20230823_161034.jpg
    97 KB · Views: 2
Back
Top Bottom