Tunasema jinsi sheria ya uchaguzi ilivyo inaitaka Tume ya uchaguzi itangaze matokeo ya kila jimbo lakini msingi wa hayo matamko wapigakura hawawezi kuyahakiki na hivyo kwa kupitia sheria mbovu za uchaguzi utendaji wa tume ya uchaguzi hauwezi kuhakikika.
Wapigakura wanayo haki ya kikatiba kuhakiki jinsi tume ya uchaguzi inavyotekeleza majukumu yake ya kisheria lakini sheria za uchaguzi ni kikwazo kikubwa kwa sababu wapigakura hunyimwa taarifa za majumuisho ya kura kwa kila kituo