#COVID19 New World Order: My COVID-19 Passport

Ukiwa mwongo uwe na kumbukumbu. Unayemnanga aliagiza Wizara ya Afya kujiridhisha kwanza kabla ya kupokea chanjo na dawa zozote kutoka ndani na nje ya nchi. Rais aliyeko madarakani ameongeza kwa kuteua rasmi Kamati ya kufanya uhakiki wa hiyo chanjo.

Katika mapendekezo ya matumizi ya chanjo nchini ni uhiari hasa watumishi wa afya, wanaosafiri, wazee na wenye magonjwa sugu.

Wasiwasi wangu ni ubora wa chanjo tutakayoipokea. Aidha uwepo wa vifaa vya uwezeshaji uhifadhi pia yaweza kuwa changamoto. Isitoshe kwa idadi ya watu nchini ni dhahiri kudhibiti maambukizi itakuwa mtihani. Ushahidi kuna nchi mbalimbali ambazo waliochanuwa wameathirika, ikiwamo Marekani.
 

Eti BBC inakoleza mjadala tu 😂😂😂😂😂 JIONGEZE MKUU mimi huwa siweki vyanzo vya habari vya uchochoroni. Naiheshimu sana JF hivyo siwezi kuokoteza habari za uchochoroni.
 
Wenye ndoto za kujilipua chanjo ikija fanya hima upate, Binafsi leo nimesherehekea report ya kamati.
Covid passport ni Kama ilivyokuwa kadi ya yellow fever, Huna chanjo hakuna Safari.

Wale wa dar, mbeya, Dodoma mnaweza endelea kukaa bila chanjo, Kamati imesema sio lazima.
 
Jesus!!! Umechanja??? Kama umechanja then repeat after me the following words:

" Inna Lilahi waina ilayhi rajioun*
 
Mkuu umemaliza kila kitu aisee mm na familia yangu hatutafanya ujinga huo
 
They got you nigga, Bill Gates has successfully installed Windows 666 in your blood stream. Get ready for updates it'll be a bumpy ride. LOL 🤣
 
Jamaa yangu nyani nakukubali Sana mwamba sema Nini Kama Kuna uwezekano naomba unisaidie pesa kidogo bongo pagumu najua huwez kufeli fanya muamala Kaka serious asee Nina shida kidogo hata dollar tano au kumi
Mkuu upo serious? Isije kuwa kweli halafu wana tunachukulia masihara ujue.
 
Mimi nitachanja baada ya miaka mitano kupita. Niwe na uhakika ulaya na usa wote wamechanja na maambukizi hayawapati tena baada ya kuchanjwa. Lakini hii ya kuchanjwa na bado barakoa ipo pale pale. Acha mwili ujijengee kinga wenyewe.
 
Experimental vaccine?
 
Gwajifix kazilishe chanjo zako. Usipangie watu wanaoumiza vichwa vyao kuleta ahueni duniani wakati wewe unakula kondoo zako.
Utachanjwa kwa chanjo zilizopo sasa zilizoidhinishwa na WHO.
Kwani tatizo lipo wapi kawe wa kwanza hapa Tanzania kuchanjwa mRNA vaccine - sisi wengine for some reasons we shall opt for chanjo za Kichina zilizo zalishwa kwa njia ya asili (attenuated covid viruses) - by the way Chanjo za kichina zimekwisha idhinishwa na WHO kutumika Duniani, hata hivyo kuna Mataifa yalisha anza kuzitumia chanjo za Kichina hata kabla ya kuidhinishwa na WHO, mfano: Misri na Mataifa ya Latin Amerika.

Wanao mbeza beza Askofu Gwajima hawajui walisemalo, kwao kila kitu ni siasa tu na kwa kuwa aliye toa tahadhali kuhusu chanjo za mRNA ni mswahili mwenzetu,basi wanamchukulia poa kabisa na dharau juu - kumbukeni majuto ni mjukuu.
 
Mkuu Toka tumeanza kupokea chanjo toka tupate uhuru, kuna chanjo yoyote iliyokwisha tuletea matatizo?
 
Gwajima hajui chochote kuhusu chanjo wala Corona na chanjo yake.Ni debe tupu tu lenye makelele mengi.
Kama unataka kujifunza Corona wasikilize wataalamu wa afya ya binadamu na magonjwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…