New Year ndio nimeona faida ya kufahamiana na wahuni wa mtaani

New Year ndio nimeona faida ya kufahamiana na wahuni wa mtaani

Hata mimi ilishawahi kunitokea Arusha!aissee miaka ya nyuma kidogo madisco ya Arusha yalikuwa na fujo sio ya nchi hii!mara nyingi disco lilikuwa linaisha inategemea na fujo itaanza muda gani na ukienda na demu haurudi nae anachukuliwa kwa nguvu!
Sasa mimi kipindi hicho ni bishoo hatari nimetoka Dar tena!sema kilichonisaidia wakati naingia niliwalipia wahuni kama saba hv nilikuta wanashangaa tu getini!Aisse kumbe nilicheza kama pele!
Sasa kuingia tu picha linaanza nacheza mziki nawaka sio mchezo jamaa anakuja kunivua kofia namfata namdai anasema usinizingue!nikaona usinitanie aisee mimi mwenyewe nimekulia A.town kwa wahuni!aisee kilinuka wale wahuni wakaja walimvua hadi suruali chojoa kila kitu na disco ndio likaishia hapo
Una bahati maana madisco ya chuga visu ni kawaida yani..Ungetiwa bero ya mbavu anytime. Chuga ndio sehemu pekee ambayo wahuni wakizingua nachill!
 
Mbona mzee kibajeti sana, halafu huyo muhuni mbona kakusaidia sana halafu ukamtoa bia moja
 
Habar za mwaka 2021 wadau

Twende kwenye mada nikiwa somewhere nausubir mwaka mpya nilipata msala nadhan weng mnajua maeneo unayoish mtu lazima kunakuwa na vijana wahun wanaokaa hapo mtaan hawa watu wakikuzoea sometime ni shida wanaombaomba usipime kila akikuona iwe baa iwe njian jiandae utasikia broo ninunulie bia moja bas ukimwambia sina pesa utasikia ninunulie sigara bas au nisaidie mia 6 yaan usiombe wakujue hawa wadau ni mwendo huo huo kila siku iendayo kwa MUNGU

Sasa kipind cha karibun nimekuwa mgumu sn siwapi hela kabisa hata 200 ya sigara siwapi sasa nikiwa nasubir mwaka mpya kuna eneo nilikwenda kiingilio ni bia kwa kuwa mm sinywi bia nakunywa GRAND MALT nikawaelezea mabaunsa wakanielewa nikapita kuna muhun mmoja niliongozana nae yy alikuwa hana ela ata ya bia huyu nilimuacha apo apo nje nikamwambia subir nakuja sikuja nikaja kumchek baadae nikakuta kashaondoka

Nikazama ndan nikakutana na wahun wa kitaa wananijua siku hz nilivokuwa mgumu kila wakiomba ofa ya bia nawatosa nawaambia sina hela mmmh jamaa wakachoka ikabid watulie kuna muhun mmoja hv huyu nafahamiana nae mda mrefu sn akaniomba mia 5 aongezee anunue bia dah nikaona isiwe kes nikampa sasa basi kipind nimetulia akapita mrembo mmoja hv nyuma yke kulikuwa na mshikaj mm nikajua hawapo wote nikamshika yule demu mkono aiseee !!!!!

Ile namsimamisha tu demu demu akakwepesha mkono kuonesha hatak duh kuchek nyuma shikaji limevimba uso mwekundu kakunja ndita km anataka kunirukia vile aisee ikabid nijichekeshe nikamwambia haaah shemej kumbe mpo na uyu dah heri ya mwaka mpya jamaa bado limekasirika likamwita yule demu wake likawa linaniladhimisha niongee nae nikamwambia mm sikujua km mpo wote nilikuwa nampa hi !!! Tu nakaongea na bra bra kibao ili kumtuliza mshikaji jamaa bado limekunja ndita linaniuliza "unadhan uyu MALAYA "

Nikamwambia hapana mm sitongoz malaya nikimchek shemej katulia kabisa mtotp kasettle huyu jamaa bado linaongea maneno ya jazba nikawa makin sasa maana nilianza kuhis lisije
Kunivaa tukazichapa pale pale kimuonekana anaonekana ana mazoez sio km nguvu za kuwekeana nae ubavu sina shida sikutaka kuguswa jamaa lenyewe macho mekundu lishabwia konyag nikawa namwelewesha haelewi lile li demu lenyewe sijui lilikuwa linataka tupigane liko pemben tu linarembua baada lije limchukie jamaa yke wasepe lipo pemben linajibedua dah nikasema ngoja nimpotezee maana sio target na hana madhara mwenye madhara ni uyu jamaa ikabid nimwombee msamaha jamaa bado halielew yaan lipo km linataka kunirukia dah

Nikiwa bado nahangaika nae muhun wangu wa kitaa alikuja fasta km mshale from no where akakaa kati kati yetu km shield na kuna mshikaji mwingine pia nae akaingilia ule ugomvi ikawa 2 shields na kuna wengine wakaja tukawa km 7 hv afu kuna watu pemben wanalichek hilo tukio km movie lile lidemu lipo pemben bado linarembua likawa linamwrlezea jamaa fulan pamoja na demu mwingine " kwan vp hapa " lile lidada " huyu kaka kataka kunishika mm mkono alijua mm sijui malaya akati mm nimekuja na mpenz wangu uyo apo "

Nikampuuza maana niliona yule dada aliona ule ugomvi unampaisha sn alijiona malakka ivo alitaman kuona ugomvi unakuwa mkubwa huku yule muhun wangu kamdhibit yule jamaa jamaa baada ya kuona kadhibitiwa akawa anataka km kupita katikati ya watu kwa nguvu ili aje anivae muhun wangu upo vzr alimdhibit vilivyo mpaka jamaa akatulia kisha akaniita tukaekana sawa yy akiwa km msuluhish gafla yy anaongea na watu wengine aisee jamaa likanivimbia tena linanishika mkono km mtuhumiwa "ww ulijua huyu MALAYA " nikamwita muhun wangu akawa anamsoundisha nikamwambia bro yameisha bwana tusameane tu mm naenda counter kuchukua vinywaji lengo langu hapo sio kuchukua vinywaj ni kumkimbia maana kuna msela mmoja aliininong'oneza hapo ondoka

Nikiwa naelekea counter gafla lile jamaa linanifuata likaja likanishika mkono km mtuhumiwa bado limekunja ndita yule muhuni wangu nae bila kupoteza mda akawa nae kafika akamwambia yule jamaa "MWACHIE KWANZA " akamtoa mkono
Lile lidenu lipo nyuma km kawaida anarembua tu

Muhun wangu akaniambia hapa cha kufanya ili haya yaishe tununulie bia mbili mbili mia na uyu jamaa nikwamwambia NO siwez kufanya UFALA huo yaan ni bora nikununulie ww lkn sio hili jamaa demu wake mwenyewe kavaa kihasara hasara saiz saa 5 usiku upo apa baa mm ntajuaje uyu demu uyu malaya akaniambia basi malizana nae mwenyewe nikamwambia nenda kawaite SECURITY

Haya maneno yote tuliongea kwa kunong'onezana jamaa hakujua kitu gafla likaja bado limeniganda nikimwangalia mikononi kashakunja ngumi duh muhun wangu kaja kat tena nikaona hii chance sipotez nikakinbilia kwa mabaunsa nikawaelezea sek 4 nying jamaa huyo nikawaonesha jamaa mwenyewe huyo apo mabaunsa wakamdhibit

Yule nuhun wangu akaja akaniambia twende ndan achana nae uyo mchumba tu nikamuuliza utaweza kupigana nae akaniambia uyu mchumba tu akapiga ngumi mbili ukutan km TEST au MKWARA

Nikamwambia akikuponyoka atanivaa akaniambia hawez nipo mm tukazunguka mlango mwingine ili jamaa tumpotezee aisee kumbe jamaa linatutafuta bado ile tunaingia tu mlango wa pili huyo nae kafika nikaona sasa hii hatat nikamwambia baunsa niliemkuta pale mlangon uyo jamaa analeta fujo bahat nzur kumbe yule mubun wangu na uyo baunsa wanajuana apa waLimdhibit vilivyo hakufurukuta

Kisha akaniita mm tukaekana sawa akaondoka na demu lake nikawanunulua bia moja moja yule baunsa na yule nuhun wangu nikasepa
Halafu we mwenyewe muhuni vile vile
 
Kupigana na mtu ni zaidi ya kufanya mapenzi na mwanamke bila kutumia condom.
Kupigana na huyo muhuni ni kama kufanya mapenzi kavu kavu na Huyo demu wake.

Mtatoana damu muambukizane HIV kama mmoja wenu ni positive
 
Una bahati maana madisco ya chuga visu ni kawaida yani..Ungetiwa bero ya mbavu anytime. Chuga ndio sehemu pekee ambayo wahuni wakizingua nachill!
Chugga yaan huo ndo ushamba ulokua ukiniudhi. Yaan visu, masime, marungu. Hata fiesta ilikuaga changamoto. Unadhangaa mko na buridani ghafla someone be like unanijua mimi, anasoge,a shuka lake anatoa sime ama kisu ama bastola[emoji23]
 
Hata mimi ilishawahi kunitokea Arusha!aissee miaka ya nyuma kidogo madisco ya Arusha yalikuwa na fujo sio ya nchi hii!mara nyingi disco lilikuwa linaisha inategemea na fujo itaanza muda gani na ukienda na demu haurudi nae anachukuliwa kwa nguvu!
Sasa mimi kipindi hicho ni bishoo hatari nimetoka Dar tena!sema kilichonisaidia wakati naingia niliwalipia wahuni kama saba hv nilikuta wanashangaa tu getini!Aisse kumbe nilicheza kama pele!
Sasa kuingia tu picha linaanza nacheza mziki nawaka sio mchezo jamaa anakuja kunivua kofia namfata namdai anasema usinizingue!nikaona usinitanie aisee mimi mwenyewe nimekulia A.town kwa wahuni!aisee kilinuka wale wahuni wakaja walimvua hadi suruali chojoa kila kitu na disco ndio likaishia hapo
[emoji28][emoji28][emoji28]
 
Kuna mikasa ni heri kiepuka maana unaweza ingia ulingoni kumbe mpizani wako ana nyenzo viwembe, kisu, bisibisi akatumia akakutoa uhai....


kuna msala mmoja hivi ulishanitokea maisha club kitambo 2005 na nilikua vyombo tupo na mshikaji wangu nae mpenda fujo kichizi, katika kucheza mziki jamaa akawa anacheza vibaya anasukuma na kukunyagana nikamsukuma nikamwambia awe na adabu dah jamaa akarusha ngumi dah ghafla vurugu mimi na jamaa yangu tukauvaa ugomvi nakukumbuka mpinzani wangu aliingia club na viwembe, ile katika kupambana nae akatoa kiwembe ndani ya club na lile giza sikuona vizuri kama ni kiwembe, sema kwa kua nilikua na bia mkononi nikampasulia kichwani akazimia nikabebwa na mabaunsa nikawekwa kizuizini mpaka jamaa alipoamka nikawaeleza jamaa ana viwembe na alianzisha ugomvi na alificha viwembe kwenye soksi, ndiyo wakaniachia
Aiseeee.. ni hatari sana. Hatari mno. Ila maisha club jamani. Ndo maana sipendagi outing za sehen kama hizo.

Kuna siku wanafunzi tukaenda. Uzuri ama ubaya wala pombe siziwezagi kwahiyo nakua sober tu nashangaa shangaa. Sasa kuna jamaa alikua na nyoka wake. Yule jamaa alikuta nimekaa naangalia pochi za wenzangu wanacheza mziki. Wengine wako counter kufata vinywaji. Alikua na nyoka wake kama watano hivi. Tukasalimiana. Nikajua ananifahamu labda. Tukawa tunapiga story. Ana american English bana naona ananichanganya akili yangu tu[emoji23]
Sindo akaanza ning'ang'ania anataka tuondoke? Sijui yule kaka ni anaishi usa ama maigizo na ngeli yake. Acha aanze kunivutaaa. Namwambia sikujui. Machozi almost kutoka. Kama fujo hv ikaanza. Nikaona kama wale nyoka nao wanataka lianzisha. Nikawaza wasije kuwa na silaha maana hawa ni manyoka. Jamaa haelewi anataka tuondoke wote. Ubaya hata sikumwuliza ni nani. Mbaya zaidi meza ile nalinda pochi za wenzangu. Machozi si yakanianza maana nguvu sina za kupigana. Good thing akatokea mkaka tunajuana na crew lake akaona akaja akanishika mkono. Yule kaka naye akapoa. Akameuliza are u with her akamjibu yes, she is my girl. Akawa mpole akamwambia cool man, am sorry. Jamaa akaondoka na nyoka wake. Nililiaaaaa[emoji23][emoji23][emoji23] sikuwahi kurudi tena maisha sijui 2009 ileee. Ila niliwaza kama wewe mambo ya viwembe. Maisha pa kishenz sana. Nilienda tu kwaajili ya jina
 
Chugga yaan huo ndo ushamba ulokua ukiniudhi. Yaan visu, masime, marungu. Hata fiesta ilikuaga changamoto. Unadhangaa mko na buridani ghafla someone be like unanijua mimi, anasoge,a shuka lake anatoa sime ama kisu ama bastola[emoji23]
Hiko ndio kilinifanya nipachukie chuga for life!
 
Aiseeee.. ni hatari sana. Hatari mno. Ila maisha club jamani. Ndo maana sipendagi outing za sehen kama hizo.

Kuna siku wanafunzi tukaenda. Uzuri ama ubaya wala pombe siziwezagi kwahiyo nakua sober tu nashangaa shangaa. Sasa kuna jamaa alikua na nyoka wake. Yule jamaa alikuta nimekaa naangalia pochi za wenzangu wanacheza mziki. Wengine wako counter kufata vinywaji. Alikua na nyoka wake kama watano hivi. Tukasalimiana. Nikajua ananifahamu labda. Tukawa tunapiga story. Ana american English bana naona ananichanganya akili yangu tu[emoji23]
Sindo akaanza ning'ang'ania anataka tuondoke? Sijui yule kaka ni anaishi usa ama maigizo na ngeli yake. Acha aanze kunivutaaa. Namwambia sikujui. Machozi almost kutoka. Kama fujo hv ikaanza. Nikaona kama wale nyoka nao wanataka lianzisha. Nikawaza wasije kuwa na silaha maana hawa ni manyoka. Jamaa haelewi anataka tuondoke wote. Ubaya hata sikumwuliza ni nani. Mbaya zaidi meza ile nalinda pochi za wenzangu. Machozi si yakanianza maana nguvu sina za kupigana. Good thing akatokea mkaka tunajuana na crew lake akaona akaja akanishika mkono. Yule kaka naye akapoa. Akameuliza are u with her akamjibu yes, she is my girl. Akawa mpole akamwambia cool man, am sorry. Jamaa akaondoka na nyoka wake. Nililiaaaaa[emoji23][emoji23][emoji23] sikuwahi kurudi tena maisha sijui 2009 ileee. Ila niliwaza kama wewe mambo ya viwembe. Maisha pa kishenz sana. Nilienda tu kwaajili ya jina
Yaan umepona chupuchupu apo alikutungia stor ili akubebe kibabe
 
Mbona mzee kibajeti sana, halafu huyo muhuni mbona kakusaidia sana halafu ukamtoa bia moja
Toka x mas mpaka new year nilishateketeza km laki 2 hv nilijua yule muhun angeomba tena nilimpa 1000 baadae nikampa nauli 1000 pia yule baunsa nikampa 1000 ya soda
 
Hata mimi ilishawahi kunitokea Arusha!aissee miaka ya nyuma kidogo madisco ya Arusha yalikuwa na fujo sio ya nchi hii!mara nyingi disco lilikuwa linaisha inategemea na fujo itaanza muda gani na ukienda na demu haurudi nae anachukuliwa kwa nguvu!
Sasa mimi kipindi hicho ni bishoo hatari nimetoka Dar tena!sema kilichonisaidia wakati naingia niliwalipia wahuni kama saba hv nilikuta wanashangaa tu getini!Aisse kumbe nilicheza kama pele!
Sasa kuingia tu picha linaanza nacheza mziki nawaka sio mchezo jamaa anakuja kunivua kofia namfata namdai anasema usinizingue!nikaona usinitanie aisee mimi mwenyewe nimekulia A.town kwa wahuni!aisee kilinuka wale wahuni wakaja walimvua hadi suruali chojoa kila kitu na disco ndio likaishia hapo
Hahahahs
 
Nhgfdsazzxcccvbpoiuytrewqdfghjklzqqqbvcuyr

Nilikuwa naangalia keyboard yangu kama inaweza kuandika bila shida
Hakika.
Eq3Vc5cW4AA8mcX.jpg
 
Back
Top Bottom