Kuna mikasa ni heri kiepuka maana unaweza ingia ulingoni kumbe mpizani wako ana nyenzo viwembe, kisu, bisibisi akatumia akakutoa uhai....
kuna msala mmoja hivi ulishanitokea maisha club kitambo 2005 na nilikua vyombo tupo na mshikaji wangu nae mpenda fujo kichizi, katika kucheza mziki jamaa akawa anacheza vibaya anasukuma na kukunyagana nikamsukuma nikamwambia awe na adabu dah jamaa akarusha ngumi dah ghafla vurugu mimi na jamaa yangu tukauvaa ugomvi nakukumbuka mpinzani wangu aliingia club na viwembe, ile katika kupambana nae akatoa kiwembe ndani ya club na lile giza sikuona vizuri kama ni kiwembe, sema kwa kua nilikua na bia mkononi nikampasulia kichwani akazimia nikabebwa na mabaunsa nikawekwa kizuizini mpaka jamaa alipoamka nikawaeleza jamaa ana viwembe na alianzisha ugomvi na alificha viwembe kwenye soksi, ndiyo wakaniachia