News:AJIRA ZA WALIMU....

Baba Lai

Member
Joined
Jan 23, 2014
Posts
36
Reaction score
3
Jamani wanajamvi wenzangu hivi kwanini hizi ajira mpya za walimu hazitoki?kila mtu anasema lake analojua,mara kesho,mara wiki ijayo....na hizo siku zinafika hakuna jipya.JAMANI KAMA KUNA MTU MWENYE TAARIFA KUTOKA CHANZO KINACHOAMINIKA ATUJULISHE KUWA NINI KINAENDELEA HUKO JIKONI.
 
hakuna mwenye uhakika humu ndan wote wanagues binafsi ikifika tar 20 ajira bado napotezea naanza mishe zangu nyingine.
 

Makuku Rey come this way.
 
Last edited by a moderator:
hakuna mwenye uhakika humu ndan wote wanagues binafsi ikifika tar 20 ajira bado napotezea naanza mishe zangu nyingine.

Kweli ndugu ila kuna haja ya kufika wizarani ''physically''kujua lini wanatoa ajira ili kama hawana mpango wa hivi karibuni watu tushike ustaarabu mwingine.
 
Wizara hata kama haina pesa irushe majina kwenye mtandao kisha irefushe muda wa kuripoti hata kama ni April 2014 si tatizo. Kusubiri bila kujua kama jina lako limo au la ni risk. Bora majina yarushwe, asie kuwemo ajipange mapema cha kufanya, ikiwa bado shule binafsi zinapokea walimu. Kuendelea kukaa kimya kwa wizara kunaleta matatizo kwa walimu watarajiwa katika hatma ya maisha yao.
 
Polen jaman dah wamewazingua sana na hili bunge lå katiba ase....mmh posho zao tuu kichwa kinawaka moto mjipe moyo lakin watawatoa as soon as wakiamua
 
Kweli mkuu,mfano mm nimemwambia mwajiri wangu(private school) kuwa sitaongeza mkataba tena ambao unaishia mwezi huu wa pili.Sasa nahisi kama hizi posts hazitatoka mwezi huu na hivyo kunipotezea mwelekeo.Kwakweli hawa jamaa wanadumaza na kupoteza malengo ya watu.ILA MIMI NAONA MPANGO NI KWENDA KWENYE WIZARA HUSIKA WATUAMBIE MOJA KUWA WANATOA HIZO POST AU LA.
 
Kweli kaka jamaa hapo juu hajatumia hekima. Japo anaweza kuwa na hasira lakini kwa mwalimu kutoa kauli kama hiyo sio sawa. Tambua ulilenga kufikisha ujumbe kwa wahusika wa ajira sasa waziri akisoma akakutana na tusi kama hilo inaleta shida kutafakali aina ya mwalimu mtarajiwa.
 

Baba Lai, wazo zuri, pia viongozi wetu wajifunze kutoa majibu ambayo yako clear na yenye uhakika. Itakumbukwa kwamba Mh. KASSIM MAJALIWA alisema ajira zingetoka januari sasa kimya bora kama mambo yamekwama angekuja hadharani akatoa ufafanuzi nini kimekwamisha na zitatoka lini. Wanafunzi wanatabika kwa uhaba wa walimu shuleni wakati walimu wapo mtaani!! Watuambie wanatoa lini posts? Kama pesa hazipo watoe majina kisha waextend muda wa kuripoti ili watu wa EFDs wakusanye amafaranga kwanza.
 
Mie nategemea kesho au keshokutwa,wakizngua naendelea na mambo yangu, nkafundishe kemia private.
 
Naungana na Mdau aliyependekeza kama itafika tarehe 20/02/2014 anapotezea.
Kwahiyo bila kupindisha maneno nasema kuwa mwisho wa kuvumilia kwa mimi binafisi ni tar;20/02/2014, baada ya hapo Serkali itakuwa imeshapoteza mwalimu mmoja wa Mathematics kutoka SUA.
 
jamani serikali haina pesa? ila inapesa za anasa za kuwalisha mafixadi na wanao jadili bunge la katiba @ mil 63 kwa siku ILA SIYO WALIMU,kapigeni Private,
 
huu mpango wao wa BRN utafanikiwa kwel kwa mtindo huu wa kushindwa kuwaajil walim kwa wakati?yaan pesa za walim kuwalipa hakuna lakin kupanga bajeti la bunge lao la kupeana ulaji ndo wanazo... sasa wanadhan hyo katiba yao itatekelezwaje kwa kuwa na watu mambumbumbu!
 
Wanahitaji taifa la mambulula iliwawaburute kwa kujinufaisha wao na wanao 2, siyo watanzania ila nawalaani kwa kula jasho la mwananchi asiyejua atalala wapi wala atakula nini?
 

hivi itafika mpaka lini? tuambiane ukweli siyo kubebana kwani waziri ni MUNGU au malaika,hata wao ni hawafai 2,wapo kama vivuli 2 hakuna lolote, kama wanajua umuhimu siwange wa ajiri walimu,ina bakia KASSIMU MAJALIWA na MH JK, kudanganya walimu kwamba ifikapo january 2014 watawaajiri walimu? na mpaka sasa hakuna lolote,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…