News:AJIRA ZA WALIMU....

News:AJIRA ZA WALIMU....

hivi itafika mpaka lini? tuambiane ukweli siyo kubebana kwani waziri ni MUNGU au malaika,hata wao ni hawafai 2,wapo kama vivuli 2 hakuna lolote, kama wanajua umuhimu siwange wa ajiri walimu,ina bakia KASSIMU MAJALIWA na MH JK, kudanganya walimu kwamba ifikapo january 2014 watawaajiri walimu? na mpaka sasa hakuna lolote,

Wanapoitwa mawaziri mizigo wanakataa,sasa huu ni utaratibu gani wakushindwa kutimiza wajibu wao.Mimi naungana na baadhi ya wanasiasa waliosema ''Mawaziri Mizigo wamerudi tena.''
 
Kweli mkuu,mfano mm nimemwambia mwajiri wangu(private school) kuwa sitaongeza mkataba tena ambao unaishia mwezi huu wa pili.Sasa nahisi kama hizi posts hazitatoka mwezi huu na hivyo kunipotezea mwelekeo.Kwakweli hawa jamaa wanadumaza na kupoteza malengo ya watu.ILA MIMI NAONA MPANGO NI KWENDA KWENYE WIZARA HUSIKA WATUAMBIE MOJA KUWA WANATOA HIZO POST AU LA.

Serikali huwa inalalama kwamba inawapangia walimu vituo hawaendi hii inatokana pia na kucheleweshewa ajira. Mf. Mimi leo hii niitwe private school kwa mshahara mnono nitaacha kwenda eti nangoja ajira ambayo haieleweki inatoka lini? Hili halihitaji Phd kujua kama wanabisha waunde tume watapata majibu kama haya. Serikali ijipange jamani kumkalisha mtu zaidi ya miezi minane akisubiri ajira si sahihi. Bora ukamwambia hakuna ajira akajua cha kufanya. POLISI wakitoka CCP HUWA wanamaliza muda gani wanaajiriwa? WAZEE wa Kiwira(askari magereza je?) why not to teachers?
 
Yani hii idara...ajira unaipata kwa michosho,mishahara michosho,mazingira ya kazi magumu.Kweli Tanzania itazidi kuburuza mkiani katika viwango vya elimu duniani.
 
"tuvute subira ndugu zanguni. bado tuko kwenye upembuzi yakinifu wa mchakato wa mpango maendeleo wa ajira kwa walimu wetu wapendwa. majina yatatolewa sio mrefu sana wala sio muda mfupi sana."
hayo ndo majibu mtakayopewa wizarani. tena wanaweza kwenda mbali zaidi " penyewe hamjaajiriwa mko hivi, mkiajiriwa je?" teh teh teh ! polen sana bandugu! hii ndo sirikali yetu
 
huu mpango wao wa BRN utafanikiwa kwel kwa mtindo huu wa kushindwa kuwaajil walim kwa wakati?yaan pesa za walim kuwalipa hakuna lakin kupanga bajeti la bunge lao la kupeana ulaji ndo wanazo... sasa wanadhan hyo katiba yao itatekelezwaje kwa kuwa na watu mambumbumbu!

BRN ni mpango ulioshindwa kabla ya kuanza utekelezaji. Naamini mioyoni mwao wana slogan nyingine kabisa: BFN - Big Failure Now.
 
Kuna rafikiangu mmoja ni MWL. alinitumia ujumbe hivi karibu kwamba"alikutana na D.E.O. ktk maongezi yao akamuuliza kuhusu ajira akamwambia watatangaza FEBR 17, sasa huyu rafiki mara zote huwa hanipo stori za uongo labda iwe safari hii. TUSUBIRI TUONE
 
BRN ni mpango ulioshindwa kabla ya kuanza utekelezaji. Naamini mioyoni mwao wana slogan nyingine kabisa: BFN - Big Failure Now.

Kila kitu tunasingizia katiba mbovu jamani hata la kuajiri walimu hadi katiba ikae vizuri kweli? Hata kulinda tembo wetu tuiandikie katiba? Madai ya wafanyakazi hadi katiba mpya iyatatue kweli. Ifike mahali tuseme it is enough sasa.
 
nikiajiriwa itabidi nikae 2months bila kuteach, il kujijenga kisaikolojia vingnevyo nitaisema vbaya serikal darasani
 
kazi ni kufelisha wanafanzu nd' serikali ichukue hatua kutoa ajira mapema kwa walimu,mbona mwaka jana tareh 13-14 kama ya leo matokeo yalikuwa hewani
 
"ajira hadi april" taarifa nyingine kutoka kwa mzigo
 
OTE=Elias Ilomo;8683127]Kwan nyie bado hamja ajirwa, mbona wenzenu kitambo sana tu......[/QUOTE]

KAULI ZA KICHOCHEZI...wapi mods?
 
Yan 2naishi bila mwelekeo jaman waseme 2jue 1 bt pia walim wenzangu 2jipe moyo kwan wazir wa elim hajatamka lolote bdo
 
Back
Top Bottom