Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
Unajua ni too low, yaani Ikulu inajibu habari za wahuni wa Kigali! Halafu anashindwa kufafanua hata swali kwani kuoa mnyarwanda kuna tatizo gani au kunaondoa haki gani au kuvunja sheria gani. Halafu evidence gani iliyopo, lakini huko kote wala hakutakiwa kujibu alitakiwa kusema ni habari za mitaani aendelee na shughuli nyingine.Mkuu Nguruvi3 , Hawa watu huwa wananishangaza sana. Kwenye mambo ya msingi ambayo wanatakiwa kuwaeleza Watanzania wala huwaoni hata kutoa pua zao lakini wanakuwa very active kwenye mambo ambayo ni trivia.
Wanatumia nguvu kubwa kukanusha mambo ya kwenye mitandao na vijiwe vya kahawa Rwanda wakati tuna mambo muhimu nchini yanayohitaji clarification kama ya vile 'waharifu' kusafirishwa na helikopta ya serikali kwenda kusomewa mashitaka na kurudishwa tena mahabusu.
Kwani ni dhambi au kosa kuwa na uhusiano wa kindugu au kirafiki na Habyarimana?. Toka lini binadamu akapata uwezo wa kuchagua ndugu. Hizi political correctness zinawapeleka kubaya.
Huyu ametoka wizara ya mambo ya nje na hivyo ana exposure kubwa sana sasa sijui inamsaidiaje.
Tatizo la wasomi wa Tanzania ni kukosa kujiamini. Yeye anaamini kuwepo kwake Ikulu ni kwasababu amependwa na watu wa Ikulu wala soi qualifications. Matokeo ya hayo anafungia knowledge kabatini na kubaki kubweka kama mnyama mwingine katika animal kingdom. Alichotaka ni kumfarahisha bwana bila hata kuangalia rationale ya kufanya hivyo
Hawa wasomi kama akina Salva wanasikitisha. Tuna habari za askari kutoroka, kuna kumwagiwa tindikali, mashambuliz znz, matatizo ya inflation, mambo mengi ya kisiasa na kiuchumi wao wameona muhimu sana ni kuja kujibiozana na wahuni wa Kigali. Too low Ikulu, this is too low. Kwa nchi za wenzetu huyu bwana kaidhalilisha taasisi ya urais angekuwa kwenye dawati habari maelezo kesho. Shame on you Assah